Je umewahi kukutana na mtu ambaye ni nguvu ya kusikilizwa
mahali pote aendapo? Baadhi ya sifa za mafumbo, zisizoelezeka kirahisi
zimemtenga mbali na watu wengine wote. Kwa hakika, hivyo ndivyo ilivyokuwa miaka
elfu mbili iliyopita kwa Yesu Kristo, lakini hiyo haikuwa tu tabia ya Yesu
pekee iliyowavuta hao waliomsikia. Kwa hao walioshuhudia maneno na maisha yake
wanatuambia jambo fulani kuhusu Yesu wa Nazareti kuwa alikuwa tofauti na watu
wengine wote.
Sifa pekee za Yesu zilikuwa ni yeye mwenyewe. Hakuandika
kitabu, hakuamrisha jeshi, hakushikilia ofisi ya kisiasa, wala hakumiliki mali.
Hasa, alisafiri karibu maili mia moja za kijiji chake, akiwavuta makundi ya
watu walioshangazwa kwenye maneno makali na matendo yake ya kushangaza.
Na pia ukuu wa Yesu ulikuwa wazi kwa hao waliomuona na
kumsikiliza. Na wakati watu wengine maarufu hatimaye husahaulika kwenye vitabu
vya historia, Yesu bado ni kitovu cha maelfu ya vitabu na majadiliano yasiyo na
kifani kwenye vyombo vya habari. Na mengi ya majadiliano hayo yanazungukia
kuhusu madai ambayo Yesu aliyafanya – madai ya msingi ambayo yaliwashangaza
wote, wafuasi wake na maadui zake.
Hasa ni madai ya kipekee ya Yesu yaliyomsababishia aonekane
kama tishio kwa Mamlaka za Kirumi na Tawala za Kiyahudi. Japokuwa alikuwa mgeni
asiye na sifa wala nguvu za kisiasa, lakini ndani ya miaka mitatu, Yesu
amebadilisha dunia kwa karne 20 zingine zijazo. Viongozi wengine wa kimaadili
na kidini wameacha mfano – lakini si kama huo wa mtoto huyo wa Seremala wa
kawaida kutoka Nazareti.
Ni kitu gani kuhusu Yesu Kristo ambacho kimeleta mabadiliko?
Alikuwa ni mtu mkuu tu, au kuna kitu cha zaidi?
Maswali haya yaelekea kwenye kiini kwamba Yesu alikuwa ni
nani hasa. Wengine wanaamini alikuwa tu ni mwalimu wa maadili makuu; wengine
wanaamini alikuwa ni kiongozi tu wa dini kubwa duniani. Lakini wengine
wanaamini zaidi ya hayo. Wakristu wanaamini kuwa Mungu kwa hakika alitujia
duniani katika umbo la ubinadamu. Na wanaamini kwamba ushahidi unathibitisha
hilo.
Mwalimu wa Ajabu
Hata hao toka katika dini zingine wanakiri kwamba Yesu
alikuwa Mwalimu wa Maadili Mkuu. Kiongozi wa wahindi, Mahatma Gandhi,
aliongelea mno maisha ya Yesu na maneno yake makuu ya busara.[1] Vile vile
msomi wa Kiyahudi Joseph Klausner aliandika, “Inakubalika pote kwamba Kristo
alifundisha maadili safi na makuu mazuri sana… ambayo yanapita mafundisho na
maneno ya watu wa busara wa kale, wote waliowahi kutokea.”[2]
Mafundisho ya Yesu mlimani, yameitwa ni mafundisho bora ya
binadamu, yaliyowahi kutamkwa na binadamu. Kwa kweli, mengi ya tujuayo leo kama
“haki sawa” kwa kweli ni matokeo ya mafundisho ya Yesu. Mwanahistoria Will
Durant, si-Mkristu, alisema kwamba Yesu aliishi na alipambana vilivyo bila
kukoma kwa ajili ya ‘haki sawa’ katika nyakati za sasa angepelekwa Siberia.
Aliwahi kusema yeye ambaye ni mkuu
miongoni mwenu , na awe mtumishi wenu”
hii ni kinyume na maono ya kisiasa ya ufahamu wote.[3]
Wengi kama Ghandi, wamejaribu kutofautisha mafundisho ya
Yesu ya maadili kutoka katika madai yake kuhusu yeye mwenyewe, wakiamini
alikuwa ni mtu tu mkuu ambaye alifundisha maadili lukuki – mengi. Hii ilikuwa
ni njia ya mmoja wa Baba Waasisi, Rais Thomas Jefferson, ambaye alikariri na
kunakili Agano Jipya, akiondoa sehemu zilizomzungumzia Uungu wa Yesu, akiacha
vifungu vilivyojali mafundisho ya kiimadili ya Yesu.[4] Jefferson aliendelea na
kukopi kwake na kunakili Agano jipya akimheshimu Yesu kama labda ni mwalimu
mkuu kuliko wote wa maadili wa nyakati zote.
Kwa hakika, maneno ya kukumbuka ya Jefferson katika Tangazo
la Uhuru yalijengwa ndani ya misingi ya mafundisho ya Yesu kwamba kila mtu ni
wa umuhimu mkubwa na sawa kwa Mungu, bila kujali jinsi, taifa, rangi wala
nafasi yake katika jamii. Andiko maarufu
laweka wazi, “Twashikilia kweli hizi kuwa ushahidi kwamba watu wote wameumbwa
sawa, kwamba wamebarikiwa na Muumbaji kwa haki fulani sawa zisizohamishika na zisizotwalika/twaliwa na
mtu mwingine…”
Lakini kitu kimoja Jefferson hakukijibu: Ikiwa Yesu si kweli
alidai kuwa Mungu, asingekuwa mwalimu mzuri wa maadili. Lakini ni kweli Yesu
alidai Uungu? Kabla hatujaangalia kitu gani Yesu alidai, twahitaji kuchunguza
uwezekano kwamba alikuwa tu kiongozi mkuu wa dini?
Kiongozi wetu mkuu wa dini?
Cha kushangaza, Yesu kamwe hakudai kuwa yeye ni kiongozi wa
kidini. Hakuwahi kamwe kujiingiza au kulazimisha agenda za tamaa, na muda wote
alihubiri nje ya idara za kidini.
Mtu anapomlinganisha Yesu na viongozi wengine wa kidini,
tofauti kubwa yajitokeza. Ravi Zacharia, ambaye alikulia katika utamaduni wa
ki-Hindu, amejifunza dini za duniani na amegundua tofauti kubwa kati ya Yesu
Kristo na waasisi wa dini zingine.
”Katika yote haya, kunajitokeza, ufundishaji, mwenendo wa
maisha. Na Si Zoroaster unayemgeukia; ni Zoroaster ambaye unamsikiliza. Si
Buddha anayekukumboa; ni ukweli bora unaokuelekeza. Si Mohammad
anayekubadilisha, ni uzuri wa Koran unaokuvutia. Tofauti na hayo, Yesu
hakufundisha tu au kueleza ujumbe wake. Alifanana na ujumbe wake.”[5]
Ukweli wa Zakariya ‘kumweka unatokana na idadi ya mara
katika Injili kuwa Yesu’ mafundisho ujumbe mara tu “Njoni kwangu” au “Nifuate”
au “Mt’iini yangu.” Pia, Yesu aliweka wazi kwamba kazi yake ya msingi ilikuwa
kusamehe dhambi, jambo ambalo Mungu pekee anaweza kufanya Katika dini kubwa za
duniani.
Huston Smith aligundua, “Watu wawili tu ambao
wamewastajaabisha wafuasi wao sana kiasi kwamba swali walilozingatia halikuwa
‘Ni nani Yeye?’ bali ni nini Yeye?’ Watu hao walikuwa ni Yesu na Buddha. Buddha
alisema waziwazi kwamba alikuwa ni mtu tu, sio Mungu – kama vile aliwahi au
alishaona majaribio ya kumwabudu yeye [Yesu]. Yesu kwa upande mwingine, alidai
kuwa Mungu mtakatifu.[6]
Na hilo linatuongoza sisi kwenye swali la nini Yesu alifanya
kudai mwenyewe; je, Yesu alidai kweli kuwa Mungu Mtakatifu
Yesu aliwahi kudai kuwa Mungu?
“Marafiki na maadui
wa Yesu waligawanyika tena na tena na kile alichosema na alichofanya [Yesu].
Alikuwa alitembea barabarani, dhahiri kama mtu yeyote, kisha akageuka na kusema
kitu fulani mfano ‘Kabla ya Abraham kuwako, nipo.’ Au iIkiwa umeniona, basi
umemuona baba. Kisha kwa utulivu baada ya kulaumiwa kukufuru, alisema, ‘Mwana
wa Adamu ana mamlaka duniani kusamehe dhambi’ Kwa wafu, alisema ‘Njoo mbele’,
au, ‘Inuka’ na walitii. Kwa tufani baharini aliweza kusema ‘Tulia’ na kwa
kipande cha mkate, alisema ‘Kuwa vipande elfu moja’ na vilifanyika mara
moja.”[7]
Lakini ni kitu gani Yesu alimaanisha kwa hayo maneno? Je,
inawezekana Yesu alikuwa mtume tu kama Musa au Eliya, au Daniel? Hata usomaji
wa juu juu wa Injili unadhihirisha kwamba Yesu alidai kuwa mtu fulani zaidi ya
nabii. Na hakuna mtume mwingine aliyefanya hayo madai kujihusu, kwa kweli,
hakuna mtume mwingine yeyote aliwahi kujiweka katika nafasi ya Mungu.
Baadhi ya watu wanadai hakuwahi waziwazi kusema “Mimi ni
Mungu”. Ni kweli kwamba hakuwahi kunena maneno hayo? “Mimi ni Mungu”. Vilevile,
Yesu hakuwahi waziwazi kusema “Mimi ni binadamu” au “Mimi ni nabii” Na Yesu
alikuwa binadamu bila shaka, na wafuasi wake walimchukulia kama nabii kama Musa
na Eliya. Kwa hiyo hatuwezi kuamua kwamba Yesu kuwa mtakatifu ni kwa sababu
hakusema maneno hayo, kama ambavyo hatuwezi kusema hakuwa nabii.
Kwa kweli, kauli za Yesu kujihusu zinapinga na wazo kwamba
alikuwa tu mtu mkubwa au nabii. Katika zaidi ya mara moja, Yesu alijiita Mwana
wa Mungu. Wakati alipoulizwa kwamba alifikiria imezidishwa kwa Yesu kuwa Mwana
wa Mungu, mwimbaji kiongozi wa U2 Bono, alijibu:
‘Hapana, haijazidishwa kwangu. Angalia mwitikio wa kawaida
kwa simulizi ya Kristo siku zote huwa hivi. Alikuwa nabii mkubwa, dhahiri
alikuwa mtu wa kuvutia, alikuwa na mengi ya kusema miongoni mwa mitume wengine
wengi, kama Eliya, Muhammad, Buddha, or Confucius. Lakini kwa kwa kweli Kristo
hakuruhusu jambo hilo. Hakuruhusu udhanie hivyo kirahisi. Kristo asema, Hapana,
mimi sisemi, mimi ni mwalimu, msiniite mwalimu. Mimi sisemi mimi ni nabii…
Ninasema mimi ni Mungu katika ubinadamu. “Na watu wanasema, hapana, hapana, ni
nabii tu, nabii tunayeweza kumkubali.”[8]
Kabla hatujachunguza madai ya Yesu, ni muhimu kuelewa kwamba
aliyafanya katika mazingira ya imani ya kiyahudi katika Mungu mmoja. Hakuna
myahudi mwaminifu angeamini Mungu zaidi ya mmoja. Na Yesu aliamini Mungu mmoja,
akisali kwa Baba yake “Mungu wa Kweli wa Pekee.”[9]
Lakini katika maombi hayo, Yesu alizungumzia ya kuwa siku
zote na Baba yake. Na wakati Philipo alipomuuliza Yesu kumuonyesha Baba, Yesu
alisema, “Philipo, nimekuwa nawe kwa muda mrefu na bado haunijui? Yeyote
aliyeniona mimi, amemuona Baba.”[10] Kwa hiyo swali ni “Yesu alikuwa anadai
kuwa Mungu wa Waebrania aliyeumba ulimwengu?
Yesu alidai kuwa ni Mungu wa Ibrahimu na Musa?
Yesu aliendelea kujiita katika namna ambazo
ziliwastaajabisha wasikiliza wake. Kama ambayo Piper alivyonukuu, Yesu alitoa
kauli za kujiamini, “Kabla ya Abraham kuweko, MIMI NIPO.[11] “Alimwambia Martha
na wengine waliomzunguka, “MIMI NI ufufuo na uzima;[12] yeyote aniaminiye, japo
amekufa, ataishi”[13] “MIMI NI njia pekee ya uzima”[14] au, “Mimi ni kweli”[15]
Haya na mengine kadhaa ya madai yake yalitanguliwa na maneno matakatifu kwa
ajili ya Mungu, “MIMI NI (ego eimi).[16] Yesu alimaanisha nini kwa hizo kauli,
nini maana na umuhimu wa neno “MIMI NI”?
Kwa mara nyingine, lazima turejee kwenye maudhui. Katika
maandiko ya kiebrania, wakati Musa alipomwomba Mungu kwa jina lake katika
kichaka kiwakacho, Mungu alijibu “MIMI NI”. Alikuwa akijidhihirisha kwa Musa
kwamba yeye ni Mungu moja wa pekee ambaye yuko zaidi ya nyakati na aliyekuwapo
sikuzote. Kwa kiasi kikubwa Yesu alikuwa akitumia maneno haya matakatifu
kujielezea yeye. Swali ni “Kwanini?”
Tangu kipindi cha Musa, hakuna myahudi angejiita mwenyewe au
kitu chochote kwa kutumia “MIMI NI”. Kama yalivyokuwa matokeo, Madai ya Yesu ya
“MIMI NI” yaliwakasirisha viongozi ya kiyahudi. Wakati mmoja kwa mfano, baadhi
ya viongozi walieleza kwa Yesu kwanini walikuwa wanajaribu kumuua. “Kwa sababu,
wewe mtu tu umejifanya mwenyewe kuwa Mungu.”[17]
Matumizi ya Yesu ya jina la Mungu, yaliwakasirisha kwa kiasi
kikubwa viongozi wa dini. Pointi ni kwamba hawa wasomi wa Agano la Kale,
walijua hasa nini alikuwa akisema – alikuwa akidai kuwa Mungu, kwa uwazi
imedhihirika, si kwa kwa maneno yake tu, lakini pia kwa hatua hasi zao kwa
maneno hayo.
C. S. Lewis mwanzo alimfikiria Yesu kuwa hadithi. Lakini
msomi huyu mwerevu, aliyezijua hadithi vizuri, alihitimisha kwamba Yesu alikuwa
mtu kweli. Zaidi ya hapo, wakati Lewis alipokuwa akichunguza uthibitisho wa
Yesu, alihakikishiwa kwamba sio tu kwamba Yesu alikuwapo kweli, lakini pia
hakuwa kama mtu yeyote aliyeishi. Lewis anaandika,
“Kisha kuna kitu cha kushangaza kweli” Lewis anaandika,
“Miongoni mwa hawa wayahudi, hapo ghafla anatokea mtu anayeendelea kuzungumza
kama vile alikuwa Mungu. Anadai kusamehe dhambi. Anasema siku zote aliwakuwapo.
Anasema atakuja kuhukumu ulimwengu
katika siku za mwisho.”
Kwa Lewis, madai ya Yesu yalikuwa makubwa na mazito sana
kufanywa na mwalimu wa kawaida au mwalimu wa dini. (Kwa kuangalia kwa undani
zaidi madai ya Yesu kuwa Mungu, angalia “Je Yesu alidai kuwa Mungu?”
Yesu ni Mungu wetu ?
Wengine wamebisha kwamba Yesu alikuwa tu akidai kuwa sehemu
ya Mungu. Lakini nia ni kwamba sisi sote tu sehemu ya Mungu, na ndani yetu kuna
mbegu ya utakatifu, hiyo si kwa urahisi kuwa ni maana inayowezekana kwa yale
maneno na matendo ya Yesu. Mawazo hayo ni kudhania kimarejeo, na ni
mageni/tofauti na mafundisho yake, tofauti na imani zake, na tofauti na uelewa
wa wafuasi wake wa mafundisho yake.
Yesu alifundisha kwamba yeye ni Mungu katika namna ambazo
wayahudi walimwelewa Mungu na namna ambayo maandiko ya waebrania
yalivyomwelezea Mungu, sio kwa jinsi ambayo harakati za kizazi kipya
kinavyomwelewa Mungu. Si Yesu wala wamsikilizao waliokatishwa kuona nyota, na
wakati wanapomzunguzia, walikuwa hawazungumzii nguvu za anga. Kwa ufupi ni
vibaya kuelezea upya kitu gani Yesu alimaanisha kuhusu Mungu.
Lewis anaeleza,
Sasa tuwe wawazi. Miongoni mwa waaminio utukufu wa Mungu wa
ulimwengu, kama wahindi, yeyote aweza asema alikuwa sehemu ya Mungu, au
aliyekuwa na Mungu, kwa sababu alikuwa myahudi, hakukumaanisha aina ya Mungu,
kwa lugha yao, ilimaanisha Mungu kuwapo nje ya ulimwengu aliouumba na bila
shaka alikuwa tofauti na kitu kingine chochote. Na unapoelewa hilo, utaona nini
huyu mtu alichosema, rahisi kabisa, kitu cha kushangaza ambacho kimekuwa
kikinenwa na midomo ya wanadamu.[19]
Bila shaka kuna hao ambao wanamkubali Yesu kama mwalimu
mkuu, lakini hawataki kumwita Mungu.
Kama mwamini Mungu, tumeona kwamba Thomas Jefferson alikuwa hana tatizo
kukubali mafundisho ya Yesu ya maadili huku akikataa Uungu wake.[20] Lakini
kama tulivyosema na tutavyochunguza zaidi, ikiwa Yesu hakuwa namna alivyodai
kuwa, lazima tutafute sababu zingine ambazo hazikumfanya kuwa mwalimu mkuu wa
maadili. Lewis alidai “Ninajaribu hapa kumzuia yeyote asije akasema kitu cha
kipuuzi ambacho watu wengi wanasema kumhusu Yeye [Yesu]: “Mimi niko tayari
kumkubali Yesu ni Mwalimu Mkuu wa Maadili, lakini sikubali dai lake la kuwa
Mungu. ‘Hicho ni kitu kimojawapo tusichotakiwa kusema.”[21]
Katika kutafuta kwake ukweli, Lewis alijua kwamba hawezi
kuwa na namna zote mbili za ukuu wa Yesu. Aidha Yesu alikuwa yule – Mungu
aliyedai kuwa, katika mwili au madai yake hayakuwa kweli! Na kama hayakuwa
kweli, Yesu asingeweza kuwa Mwalimu Mkuu wa Maadili. Angekuwa aidha anadanganya
kimataifa? Au angekuwa mwendawazimu akidai namna mbalimbali za Uungu.
Yesu hakudanganya
Hata wakosoaji wakuu wa Yesu wamemwita mwongo. Kashifa hiyo
kwa hakika haimfai Yesu mwenye maadili makuu na mafundisho ya hadhi ya juu.
Lakini ikiwa Yesu si yule anayedai kuwa, lazima tuthibitishe uwezekano kwamba
alikuwa akidanganya kila mtu kimataifa!
Mojawapo ya kazi za kisiasa zenye ushawishi mkuu za nyakati
zote ziliandikwa na Niccolo Machiavelli in 1532. Katika msingi wake,
Mwanamfalme Machiavelli anaaamini kwamba mamlaka, mafanikio, umaarufu na
ufanisi, viko juu ya uaminifu, itikadi na uadilifu.
Ingewezekana Yesu Kristo angejenga kanisa lake katika uongo
ili kupata mamlaka, umaarufu au mafanikio? Kwa kweli, wapinzani wa Yesu wa
kiyahudi, walikuwa wakiendelea moja kwa moja kumfanya Yesu aonekane kama mwongo
na tapeli!
Swali tunalotakiwa kushughulika nalo ni: Kitu gani kingeweza
kumsukuma Yesu kuishi maisha yake yote kuwa mwongo? Alifundisha kwamba Mungu
alipingana na kudanganya na unafiki, kwa hiyo asingekuwa akifanya hivyo
kumfurahisha Baba yake. Kwa hakika hakudanganya kwa manufaa ya wafuasi wake,
kwa sababu wote kasoro mmojawao walikuwa tayari kujitoa mhanga kuliko kukana
ukuu wake. (Angalia “Je, Mitume waliamini Yesu ni Mungu? na kwa hiyo tunabakiwa
na maelezo ya msingi ya namna mbili, na kila namna ni ngumu.
Faida kuu
Watu wengi wamedanganya kwa faida binafsi. Kwa kweli,
msukumo wa danganyifu nyingi ni kuwa baadhi waliona faida kwao binafsi. Kitu
gani Yesu angekuwa ametumainia kwa kudanganya kuhusu utambulisho wake? Mamlaka
ndiyo yangekuwa jibu la wazi dhahiri. Ikiwa watu waliamini alikuwa Mungu,
angekuwa na mamlaka makubwa. (Hiyo ndiyo sababu viongozi wengi wa kale, kama
vile akina Kaizari, walijidai kuwa na asili ya uungu.)
Ugumu wa maelezo haya ni kwamba Yesu alikataa majaribu yote
ya kuelekea kwenye mamlaka za ulimwengu, badala yake aliwaadhibu hao ambao
walitumia vibaya mamlaka na walioishi maisha yao wakiyatafuta mamlaka. Pia
aliaamua kwenda kuwafikia watengwa (makahaba na wakoma), wale wasio na mamlaka,
akitengeneza jumuiya ya watu ambao umuhimu wao uliokuwa chini ya sifuri. Katika
namna ambayo ingeelezwa kuwa kama kituko, yote aliyofanya Yesu na aliyosema
yalikwenda upande mwingine mbali na kujitwalia madaraka.
Ingeonekana kwamba iwapo mamlaka yangekuwa ndiyo kichocheo
kikubwa, angeepuka msalaba kwa gharama zozote. Lakini kwa nyakati kadhaa,
aliwaambia wafuasi wake kwamba, msalaba ulikuwa ndiyo safari yake na mpango
wake. Je, kufa kwenye msalaba wa Kirumi kungemleteaje mtu mamlaka?
Kifo, bila shaka, kinaweka mambo yote katika mwelekeo mzuri.
Na wakati wafia dini wamekufa kwa sababu walizoamini, wachache wamekuwa tayari
kufa kwa uongo wa waziwazi. Hakika, matumaini yake binafsi ya Yesu yangekuwa
yameishia msalabani. Lakini hata wakati wa pumzi yake ya mwisho, hakuacha dai
lake la kuwa Mtoto pekee wa Mungu. Msomi wa Agano jipya, J. I. Packer, aweka
wazi kwamba habari hii yatangaza uungu wake Yesu.[22]
Mapokeo
Hivyo, ingekuwa Yesu alipokuwa juu alidanganya kwa faida
binafsi, basi labda dai lake la msingi lingewekwa kuwa msingi wa uongo ili
kuacha urithi. Lakini hali ya kupigwa sana kuwa nyakanyaka na kupigiliwa
misumari msalabani kungemdhoofishia na kukatisha tamaa/hamu ya kutaka kuwa mtu
maarufu kuliko wote duniani.
Hapa kuna ukweli mwingine wa kukumbuka usiosahaulika.
Ingekuwa kwamba Yesu angeghairi/angeacha madai ya kuwa Mtoto wa Mungu,
asingelilaumiwa. Ilikuwa ni dai lake la kuwa Mungu na kukataa kwa kuliacha dai
hilo ndilo lililomfanya asulubiwe.
Kama ingekuwa ni kuimarisha mamlaka yake na sifa ya
kihistoria ndivyo vitu vilivyomsukuma Yesu kudanganya, basi lazime muelezee ni
namna gani mtoto wa fundi seramala kutoka katika kijiji maskini cha Yuda
angeweza kutarajia matukio ambayo yangelipeleka jina lake kuwa maarufu wa
duniani kote. Angejuaje ujumbe wake ungeishi na ungedumu? Wafuasi wa Yesu
walikimbia na Petro alimkana. Siyo utaratibu hasa wa kawaida kuacha mapokeo ya
kidini.
Je, wanahistoria wanaamini Yesu alidanganya? Wasomi
wamechunguza maneno na maisha ya Yesu kuona kama kuna ushahidi wowote wa kasoro
za maadili katika tabia yake. Kwa kweli hata wakosoaji wakali wanashangazwa na
ujasiri wa Yesu na usafi wa maadili.
Kulingana na mwanahistoria Philip Schaff, hakuna ushahidi,
aidha katika historia ya kanisa au historia ya kawaida kwamba Yesu alidanganya
kuhusu chochote. Schaff anadai, “Ni jinsi gani katika namna ya busara makini na
uzoefu ingeweza kumfanya mtu mwenye hila, mbinafsi, asiye mwadilifu abuni na
aendeleze tabia njema inayoheshimika katika historia, kuanzia mwanzo hadi
mwisho ikiwa na sifa kamilifu za ukweli na uhalisia?”[23]
Kuendelea na nia ya kumwita [Yesu] mwongo inaonekana ni kama
kuogelea kuelekea maporomoko ya juu, na ni kinyume na kila kitu Yesu
alichofundisha, alichoishi na alichofia. Kwa wanafunzi wengi, haina maana hata
kidogo [kusema Yesu ni mwongo]. Pia kukana madai ya Yesu, mtu lazima aje na
maelezo ya kutosha. Na ikiwa madai ya Yesu si ya kweli, na kwamba Yesu alikuwa
hadanganyi, basi hatua iliyobaki ni kusema kwamba alikuwa anajidanganya
mwenyewe.
Yesu angeweza kuwa anajidanganya ?
Albert Schweitzer, ambaye alitunukiwa Nishani ya Nobeli
mwaka 1952 kwa juhudi zake za kibinadamu, alikuwa na maoni yake binafsi kuhusu
Yesu. Schweitzer alidai kwamba uendawazimu uliambatana na madai ya Yesu, kudai
kuwa Mungu! Kwa maneno mengine, Yesu hakuwa sahihi kuhusu madai yake lakini
hakudanganya kimataifa. Kulingana na nadharia hii ya kubuni, anadai Yesu
alijidanganya hadi kufikia hatua ya kuamini alikuwa Masiha!
Lewis anafikiria wazo hili kwa makini sana. Anachambua
kwamba ikiwa madai ya Yesu hayakuwa kweli, basi lazima alikuwa mwendawazimu.
Lewis anatoa sababu kwamba kama mtu aliyedai kuwa Mungu asingekuwa mwalimu mkuu
wa maadili, angekuwa aidha mwendawazimu sawa na mtu anayesema yeye ni yai, au
vinginevyo angekuwa ni shetani wa Jehanam.[24]
Wengi wamesoma maisha na maneno ya Yesu na wamemkiri kwamba
ni mtu tu mwenye busara sana. Ingawaje maisha yake mwenyewe yalishutumiwa na
upotofu na ukosoaji binafsi, mwanafalsafa maarufu wa kiFaransa Jean Jacques
Rousseau (1712 – 78) amekiri tabia kuu takatifu ya Yesu na yenye akili timamu
akisema “Wakati Plato alipoelezea kuwa Yesu ni mwenye haki, alielezea tabia
halisi ya Yesu. Ikiwa maisha na kifo cha Socrates ni yale ya huyo mwanafalsafa,
basi maisha na kifo cha Yesu ni yale ya Mungu.”[25]
Bono anahitimisha kwamba ‘mwendawazimu” ndio kitu cha mwisho
ambacho mtu angemdhania Yesu kuwa.
“Hivyo kitu unachobakia nacho ni aidha kusema Kristo alikuwa
ndivyo alivyosema, alikuwa ndiye, au mwendawazimu. Ninamaanisha, tunasema
mwendawazimu katika dhana ya Charles Manson…. Sitanii hapa. Wazo kwamba
maendeleo yote ya ustaarabu kwa zaidi ya nusu ya dunia yangeweza kubadilika ama
kubadilishwa na mwendawazimu! Kwangu mimi huo ni uongo uliozidishwa
kipimo.”[26]
Eti kwamba Yesu alikuwa mwongo au mwendawazimu, kwamba
alikuwa ni Mtoto wa Mungu? Jefferson angekuwa sahihi kumwita” Yesu mwalimu wa
maadili pekee” huku akina uungu wa Yesu? Kitu cha kufurahisha, watu waliomsikia
Yesu wote, wafuasi na maadui zake hawakuwahi kumfikiria Yesu kuwa ni mwalimu tu
maadili. Yesu amepata mambo matatu kwa watu waliokutana nao: chuki, vitisho au
kuabudiwa.
Madai ya Yesu yametulazimisha kuchagua. Kama ambavyo Lewis
alivyonena, hatuwezi kumweka Yesu katika kundi la kuwa tu ni kiongozi mkuu wa
dini or mwalimu wa maadili. Ukosoaji huu wa kizamani unatupa changamoto
kusafisha akili zetu kuhusu Yesu,
“Lazima ufanye uamuzi wako sasa. Aidha huyu mtu alikuwa, au
ni mwana wa Mungu: au vinginevyo ni mwendawazimu au ni kitu kingine. Unaweza
kumnyamazisha Yesu kwa kumfanya mpumbavu, unaweza kumtemea mate, kumuua kama
pepo au unaweza kuanguka miguuni pake Yesu na kumwita Bwana na Mungu. Lakini
tusilete upuuzi wowote wa kumdhalilisha Yesu kuwa ni mwalimu tu mkuu mwanadamu.
Hajaacha hivyo wazi kwetu. Hakukusudia hivyo.”[27]
Katika ukristu pekee, Lewis amechunguza wazo linalotafakari
utambulisho wa Yesu, akihitimisha kwamba Yesu kwa hakika yuko vile vile
alivyodai kuwa. Uchunguzi wake makini wa maisha na maneno ya Yesu ulipelekea
huyu mtu mwerevu akane imani yake ya
zamani ya kutoamini na akaongoka kuwa mKristu wa kweli dhati anayeamini.
Swali kuu katika historia ya mwanadamu ni, “ni nani ni Yesu
Kristo wa kweli?” Bono, Lewis na wengine wengi wasiohesabika wamehitimisha
kwamba Mungu alitembelea sayari katika umbo la mwanadamu. Lakini kama hivyo ni
kweli, basi tungemtarajia kuwa hai leo. Na hivyo ndivyo ilivyo kwa hakika na
jinsi wafuasi wake wanavyoaamini.
Yesu alifufuka toka
katika Wafu?
Mashahidi wa macho kwa Yesu Kristo kwa kweli walizungumza na
walitenda kama walivyoamini, alifufuka toka katika wafu baada ya kusulubiwa
kwake. Ikiwa walikosea basi uKristu umeanzishwa kwa uongo? Lakini kama walikuwa
sahihi, muujiza huo ungethibitisha yote Yesu aliyosema kuhusu Mungu, kuhusu
yeye na kutuhusu sisi.
Lakini ni lazima tuamini ufufuko wa Yesu Kristo kwa imani
pekee, au kuna ushahidi wowote wa kihistoria? Wakosoaji kadhaa walianza
uchunguzi kwenye kumbukumbu za kihistoria kujaribu kuona kama kweli maelezo ya
ufufuko yalikuwa uongo.
Itaendelea
No comments:
Post a Comment