Dhiki KUU
Tunajifunza somo hili kwa kuligawa katika vipengele saba.
( i ). Dhiki tofauti
na zote
( ii ). Muda wa
dhiki kuu
( iii ). Majina yanayotumika
kuzungumzia dhiki kuu
( iv ) Watakaohusika
kuileta dhiki kuu
( v ). Makusudi ya
dhiki kuu
( vi ) Hali itakavyokuwa
wakati wa dhiki kuu
( vii ). Jinsi ya kuikwepa dhiki kuu
( I ). DHIKI TOFAUTI NA ZOTE
Wanadamu hapa duniani, wanapitishwa katika dhiki za namna
namna. Wanapitishwa katika mateso ya namna namna. Wengine wanapitishwa katika hali
nzito ya njaa nchi nzima hali inakuwa mbaya. Nchi ambazo zimewahi kushuhudia njaa
kali kama Ethiopia na Somalia, watu watakondeana na kubaki mbavu kabisa. Njaa
itakuwa kali kiasi kwamba hata ukipita mjusi watatamani kuurukia waweze kuula
lakini hata nguvu za kuurukia mjusi zinaweza kukosekena . Watu wengine
watafukiwa na vifusi sehemu zile za India kutokana na matetemeko. Wengine
wataweza kupelekwa mbali kwa kurushwa na vimbunga. Dhiki ulizozipata kwa
kuanguka katika maporomoko, kwa kupanda milima mirefu kwa shida, hizo siyo dhiki
ukilinganisha na dhiki kuu itakayouijilia ulimwengiu. Dhiki wanazozipata
wanadamu kwa kutupwa magerezani na kuteswa na kuumizwa sana, wengine wakiwekwa
katika viti ambavyo watateswa sana na polisi ili waweze kueleza yale waliyoyafanya.
Watakazwa sehemu zao za siri, watachomwachomwa kwa vitu vyenye ncha kali,
watapigwa mijeredi kwa kuwekewa pilipili kwanza sehemu za siri. Hizo siyo dhiki
kabisa ukilinganisha na ukilinganisha na dhiki itakayokuja baada ya kanisa
kunyakuliwa. Watu waliookolewa nao
wanaweza kupita katika dhiki za namna namna hapa duniani kama vile kutengwa na
wazazi, kupigwa na wazazi, kupigwa na mume
au mke kwasababu ya wokovu. Wengine watafungwa, watapigwa mawe hata kuuliwa,
hizo ni dhiki kidogo tu. Yesu Kristo alisema “duniani mnayo dhiki lakini jipeni
moyo, mimin nimeushinda ulimwengu”.Sikuja kuleta amani bali upanga watakuwepo
watu watakaofarakana pamoja nanyi, amani itavurugika”. Dhiki unazozipata
kwa sababu umeokolewa hizo ni dhiki
kidogo sana. Dhiki hizo zinaitwa dhiki
nyepesi katika biblia. ( 2 WAKORINTHO
4:17 ). Watu wote waliookoka walipita katika dhiki za namna namna kwasababu ya
wokovu ili waukane wokovu wao. Wamkane Yesu Kristo aliyewaokoa. Wengine
walikatwa vichwa na wengine kusulibiwa
kwa namna nyingi. Hayo mateso na mengine mengi waliyoyapata ni dhiki nyepesi
ukilinganisha na dhiki kubwa itakayouijilia ulimwengu. Dhiki itakayouijilia
ulimwengu inaitwa dhiki kubwa kwasababu ya mateso makubwa yatakayokuwepo (
MATHAYO 24:21 ). Wahubiri wengine wanaiita dhiki kuu lakini kitu kinachotajwa
hapo ni dhiki kubwa lakini ni kitu kilekile. (DANIELI 12:1). Utaweza kuona watu
watakaookolewa katika dhiki hii kubwa kuwa ni
Waisraeli tu kutokana na agano ambalo Mungu Alilifanya na baba zao
(Ibrahimu, Isaka na Yakobo).
( II ). MUDA WA DHIKI KUU
Dhiki kuu inatajwa kwamba itakuwa kwa muda wa juma moja la
Danieli. Itakuwa kwa muda wa juma moja la Danieli, juma la savbini. ( DANIELI
9:24-27 ) “Neno juma moja ( DANIELI 9:27)”. Juma Moja linalozungumziwa hapa
ndiyo kipindi cha dhiki kubwa. Katika unabii juma moja linazungumziwa
kumaanisha miaka saba. (MWANZO 29:27) “Timiza siku zako saba, inamaanisha
timiza miaka yako saba”. Juma moja la Danieli linalozungumziwa ni miaka saba ya
dhiki kuu.
Miaka saba ya dhiki kuu itakuwa imegawanywa katika
sehemu kuu mbili na kila sehemu itakuwa
na kipindi cha miaka mitatu na nusu au muda wa miezi arobaini na mbili (miezi
42) au siku zipatazo 1260. Kutakuwa na
mambo yatakayotokea katika miaka mitatu na nusu ya mwanzo na mambo
yatakayotokea katika kipindi cha miaka mitatu na nusu iliyosalia (UFUNUO
11:2-3), Miezi arobaini na mbili (miezi 42) na siku elfu moja na mia mbili na
sitini nazo zimetajwa zikimaanisha miaka mitatu na nusu. (UFUNUO 13:5). Katika
andiko hili inatajwa tena miezi arobaini na mbili (miezi 42) ambayo ni sawa na
miaka mitatu na nusu ya kwanza katika kipindi cha miaka saba ya dhiki kuu.
Baada ya kufahamu vipindi hivi viwili vya dhiki kuwa ni muhimu kufahamu jinsi
itakavyokuwa katika vipindi hizi viwili tofauti.
Katika kipindi cha kwanza cha miaka mitatu na nusu (miezi
arobaini na mbili) ya mwanzo, mpinga kristo atafanya agano pamoja na wana wa
Israeli. Atafanya agano na Taifa la Israeli na watadanganyika kwa kiasi
kikubwa. Katika kipindi hicho cha miaka titatu na nusu ya mwanzo, kutakuwa na
nafuu kwa wana wa Israeli kutokana na agano hilo la uongo ambalo hatimaye
litavunjwa na mpinga kristo mwishoni mwa kipindi hiki.. Katika kipindi cha pili
cha dhiki kuu cha miakamitatu na nusu, dhiki itaongezeka hususani kwa wana wa
Israeli. Wakati huo agano la mpinga kristo na wana wa Israeli litakuwa
limeshavunjika. Kwa nini dhiki itaongezwa kwa wana wa Israeli na kwa makusudi
gain? Tutaona sababu hapo mbele kidogo.
( III ). MAJINA YANAYOTUMIKA KUIZUNGUMZIA DHIKI KUBWA.
Yapo majina
mbalimbali yanayotumika kuizungumzia dhiki kuu na tunapokutana nayo
tunaweza kuyachanganya na kufikiri yanazungumzia kitu mambo mengine kumbe
yanazungumzia mambo haya. Majina hayo ni :-
( A ). Ghadhabu itakayokuja.
( 1 WAKORINTHO 1:10 )
Tunaweza tukaokolewa na ghadhabu itakayokuja yaani dhiki
kubwa. Kanisa, watu waliookolewa hatutakuwepo wakati huo wa ghadhabu ya Mungu
kwa wenye dhambi walioukataa wokovu wa Yesu.
( B ). Saa ya hukumu.
( UFUNUO 14:7 ).
Wakati wa dhiki kuu
utakuwa ni wakati wa hukumu kama
tutakavyoweza kuona hapo mbele kidogo
( C ). Adhabu na ghadhabu.
( ISAYA 24:21; ISAYA
26: 21)
Hapa inazungumziwa dhiki kuu na siyo kitu kingine
( D ). Saa ya kujaribiwa.
( UFUNUO 3:10 )
Saa ya kujaribiwa itakayoujilia ulimwengu wote ni kipindi
cha dhiki kuu
( E ). Tabu yake Yakobo.
( YEREMIA 30:7 ).
Andiko hili linazungumzia tabu watakayo wapata hususani wana
wa Israeli. Israeli mwanzo iliitwa Yakobo. Tabu yake Yakobo au Tabu yake
Israeli. Tutaweza kuona jinsi wana wa Israeli watakavyookolewa kipekee katika
dhiki kuu.
( F ). Uangamivu.
( YOELI 1:15 ).
Utakuwa ni wakati wa kuangamizwa kwa wanadamu.
( G ). Siku ya giza na weusi , siku ya mawingu na giza kuu.
( YOELI 2;1-12).
Watu watakaokuwepo duniani kwenye dhiki kubwa watageuka
nyuso zao, nyuso zitakuwa nyeupe sana kwa hofu. Jasho jembamba lililojaa chumvichumvi litakuwa limewafunika
na watakuwa kama wamepakazwa chumvi kutokana na hofu na matetemo watakay0kuwa
wameyapata.
( IV ). WATU WATAKAOHUSIKA KUILETA DHIKI HIYO KUU
Dhiki hii itakuwa kubwa sana kutokana na watatu watakaohusika
kwa wanadamu Itakuwa ni ole kwa yule atakayekuwa ameachwa na kukabiliwa na
hatari itakayokuwa inaujilia ulimwengu. Watatu hao ni akina nani? Watatu hao ni
Mungu, Shetani na Mpinga Kristol.
( i ). Mungu.
Mungu atahusika kikamilifu kuileta ghadhabu na mapigo kwa
watu.
( ISAYA 26:21 )
“Mungu atakuwa
anawaadhibu wanadamu walioukataa wokovu”
(UFUNUO14;7 ) Ni hukumu ya Mungu.
(UFUNUO15:7 )
Ghadhabu ya Mungu.
Jaribu kuwaza hapa ni Mungu anashusha ghadhabu yake.
( ii ) Shetani.
Ghadhabu kubwa ya Shetani itashushwa kwa wanadamu. Sasa hivi
tunaona jinsi Shetani anavyosababisha magonjwa
ya kila namna , akisababisha ajari, akiwafanya watu wawe vilema, washindwe kutembea , akiwafanya
watu wapooze, kuleta majipu juu ya watu kama kwa Ayubu. Hayo anayafanya sasa
lakini ghadhabu yake bado haijaja. Shetani atawashukia watu watakaobaki duniani
kwa ghadhabu nyingi akijua kwamba wakati
wake uliobaki kabla ya kutupwa katika
ziwa la moto milele na milele utakuwa unaendelea kuwa finyu au mchache. Kwa
hiyo, Shetani atashuka akiwa na ghadhabu nyingi kwa wanadamu wenye dhambi ambao
waliukataa wokovu na kuachwa wakati wa unyakuo wa kanisa ( UFUNUO 12:12 ). Si hao tu wawili, yupo wa tatu.
( iii ). Mpinga
Kristo
Leo tunawapinga Kristo wengi duniani, watu wanaosema Yesu
siyo Mwokozi ni wapinga Kristo, wanaosema hakuna kuokoka duniani ni wapinga
Kristo, wanaosema Yesu siyo mwana wa Mungu, wanaosema hakuja katika mwili, (
Mungu ) ni wapinga Kristo. Watu wote waoyapinga maandiko matakatifu ya Mungu
katika biblia takatifu woye ni wapinga Kristo hata kama wanajiita kuwa ni
wakristo. Wapinga Kristo wa namna hii wapo wengi sana duniani bado wanaendelea
kufanya kazi zao lakini yupo mmoja Mpinga Kristo anayekuja ( 1 YOHANA 2:18 ). Angalia
neno “Mpinga Kristo yuaja” huyo anayetajwa ni mmoja ajaye.
Pia kuna wapinga kristo wengi ambaowamekwisha kuwapo. Yupo
mmoja anayeitwa Mpinga Kristo kwa namna ya tofauti na Wapinga Kristo wengi wa
sasa. Yupo mpinga Kristo ajaye, anajulikana kwa majina tofauti katika biblia
zetu.
( i ). Mpingamizi
( ii ) Asi
( iii ) Chukizo la uharibifu
( iv ) Mnyama
Kwa nini anaitwa mnyama?
Anaitwa mnyama
kwasababu atakuwa ni mkatiri sana kama wa wanyama wakali walivyo. Kama jinsi Simba asivyokuwa na
huruma, anavyoweza kumchana Paa. Kama Mbwa mwitu asivyovyokuwa na huruma, kama
Chui, Dubu wasivyokuwa na huruma ndivyo atakavyokuwa. Ukatili wa kinyama
atakaokuwa nao unamfanya kuitwa Mpinga Kristo kuitwa Mnyama.
( 2 WATHESALONIKE 2:1-8 ).
Kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo hakuji mpaka afunuliwe kwanza mpinga Kristo (
ufunuliwe ukengeufu ). Hapa ndipo watu wanapochanganya mambo. Ndiyo maana
tunapaswa kujifunza kweli ili tupate kuifundisha kwa wengine.
Kuna kuja kwa Yesu
mara ya mara mbili tofauti. Kuja kwa Yesu duniani kwa mara ya kwanza kulitimia
alipozaliwa duniani kama mwanadamu lakini kuja kwa Yesu mara ya pili kutatokea
baada ya miaka saba ya dhiki kubwa. Yesu atakuja duniani kutawala kwa miaka elfu
moja na ndiyo maana atashuka kwa utiosho mwingi nautukufu mwingi tofauti na
alipokuja mara ya kwanza ambapo wanadamu
waliweza kumpiga, kumburuta na kumtemea mate. Alipokuja mara ya kwanza alikuja
katika udhaifu kwa kuzaliwa katika hori ya ng’ombe na kuishi maisha ya
kimaskini. Atakuja kama Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana na hapo ndipo
kila jicho litamwona na kila ulimi kukiri kuwa Yesu ni Bwana. Yesu atakuja na
watakatifu ( kanisa ) aliowatwaa miaka saba iliyopita na watatua katika mlima
mzeituni alipoondokea wakati anakwende mbinguni akiwa katikati ya wanafunzi
wake . Yesu atakuja akiwa amempanda Farasi mweupe. Ikimbukwe kuwa miaka saba hiyo mbinguni
kulikuwa na harusi ya mwana kondoo ( Yesu ) na watu watapokea taji mbalimbali
kutokana na kazi waliyofanya wakiwa hapa duniani. Wakati wa unyakuo wa kanisa
siyo wakati wa kuja kwa Yesu mara ya pili duniani maana Yesu hatatua juu ya uso
wa dunia. Baada ya parapanda kulia watakatifu watatwaliwa kama kwa sumaku na
kumlaki Yesu mawinguni. Yesu atakuwa mawinguni pamoja na mwaliko wa malaika
wake. Siku hiyo hakuna aijuaye lakini kuja kwake mara ya pili duniani itakuwa
baada ya kipindi cha dhiki kubwa yaani miaka saba. Andiko linalochanganya watu
ni ( 2 WATHESALONIKE 2:1-8 ) ambalo lina maana kuwa, kuja kwa Yesu kutawala
dunia miaka elfu moja ni mpaka afunuliwe kwanza mpinga Kristo ambaye kutawala
kwake ni miaka saba. Lakini huyo mpinga Kristo bado hajafunuliwa kanisa ndilo
limezuia kufunuliwa kwake. Kanisa likinyakuliwa ndipo natakapofunuliwa. (
MATHAYO 24:25 ; UFUNUO 13:1-6)
Mnyama anayetajwa hapa ni Mpinga Kristo atakayekuwa na ukali
wa kinyama Anatajwa kutoka katika bahari. Je, ni bahari gain? Bahari inayotajwa
hapo katika unabii inamaana ya kusanyiko kubwa la watu. Mahali lilipo kusanyiko
kubwa la watu linaitwa bahari ( ISAYA 57:20 ) Wabaya wengi kwa pamoja wote
wanaitwa bahari. Sehemu nyingine
inayosema “bahari ikawatoa wafu wake” ina maana ya dunia kuwatoa wafu wake.
Mnyama au mpinga Kristo anatajwa kutoka katika bahari, maana yake atatoka
katikati ya watu walioopo duniani. Huyo mnyama atakuwa ni mtu kabisa na
kwasababu tuko ukingoni mwa haya mambo kutokea inamaana huyo mtu yupo sasa
anangoja kaniosa linyakuliwe ndipo apate kufunuliwa ( UFUNUO 13:1-6 ).Vichwa,
Pembe Vilemba ni alama ya nguvuna utawala. ( UFUNUO 17:3, 9-13 ) Ufalme na
mamlaka ya kipekee ndiyo nyanazungumzia vilemba saba. Mnyama ( mpinga Kristo )
anatajwa kufananishwa na Chui, Dubu na Simba ambao ni wanyama wakali sana.
Ukatiri wa Chui, Dubu na Simba umo ndani ya mpinga Kristo Mpinga Kristo atakuwa
na mamlaka ya Kishetani, mamlaka ya kifalme ambayo itamfanya kushirikiana na wafalme duniani ( maraisi ) watakaokuwepo . Kuna wafalme
ambao hata falme zao zinazidi kuimarika na hao watampa nguvu sana ya kiuchumi , nguvu ya kivita na kumfanya awe
tishio kwa wanadamu na watu wote dunia
yote watalazimika kumsujudia.
Watu wanaofundisha kwamba kanisa
litakuwepo wakati wa dhiki kubwa, hawataki
watu wajiandae vizuri ndilo lengo la Shetani kuyaleta mafundisho hayo.
Kwamba tutapita kwenye dhiki hivyo hatuna haja ya kujiandaa kwa lolote. Hao
walimu wanaofundisha hivyo wanachanganya mafundisho.
Mpinga Kristo atakuwa amepewa uwezo wa kishetani kama tulivyosoma ( UFUNUO 13:1-8 ). Kutokana
na ishara zake na mateso yake atawafanya watu wengi walioachwa kumwabudu
Shetani au siyo kuuawa ( UFUNUO 13:13-17 ).. Kwasababu atakuwa na mamlaka ya
kipekee atawafanya watu wengi wamsujudie . Mtu ambaye hatakubali chapa ya
mnyama ambayo ni namba 666 Hataweza kununua wala kuuza na akikubali atalazimika
kumsujudia huyo Mnyama aliyepewa mamlaka na Shetani. Mwenye akili na afahamu.
Yesu alisema, “mimi nimekuja kwa jina la Baba yangu hamkunipokea lakini atakuja
mwingine kwa jina lake mtampokea” ( YOHANA 5:43 ).Watu wengi wanaomkataa Yesu
leo watalazimika kumkubali mpinga Kristo kutokana na mamlaka atakayokuwa nayo
na unabii kuhusiana na hilo lazima utatimia. Wanadamu wengi watampokea na
kumsujudia wakifikiri kuwa yeye ndiyo msaada na mkombozi wao kumbe watakuwa
wanazidi kuharibikiwa.
( V ). MAKUSUDI YA
DHIKI KUBWA
( I ). Kuliandaa
Taifa la Israeli kumpokea Yesu Kristo kama masihi wao.
Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu alijifunga katika agano au
ahadi na ahadi za Mungu haziwezi kutanguka. Mungu alijifunga katika agano
kwamba Israeli wote wataokolewa.. Alipokuja kwa ajili yao ( Israeli )
hawakuweza kumpokea kabisa ( YOHANA 1:11 ). Yesu alikuja kwa ajili ya wana wa Israeli lakini
hawakumpokea ndipo akawageukia mataifa. Mungu alishajifunga katika agano na
baba zao kuwa atawaokoa wote. Makusudi ya dhiki kuu ni kuwatesa waisraeli na
kwa mateso hayoi watamkiri Yesu Kristo kuwa ni Bwana na mwokozi wao Dhiki hiyo kubwa itawatesa sana
waisraeli lakini wote watakaokuwa wamefuata masherti kama
alivyosema Bwana wetu Yesu. Wote watakaokimbilia milimani kwa kukimbia kukwepe
kumsujudia Mnyama ( Mpinga Kristo ) na kukwepe namba yake 666, hao wote ndio
watakaookolewa Yesu atakapokuja mara ya pili duniani kwa ajili ya utawala wa
miaka elfu moja pamoja na watakatifu. Hawa ndo watakatifu wanaotoka katika
dhiki kubwa. Biblia inaposema siku zitafupishwa kwa ajili ya watakatifu ni hao
wanaotoka katika dhiki na si vinginevyo ( MATHAYO 24:21-22 ). Hawa wanaotajwq
ni watakatifu wanaotoka katika dhiki kubwa na siyo sisi tuliookolewa leo. Baada
ya wana wa Israeli kuokolewa (watakatifu
waliotoka katika dhiki ) wataungana na watakatifu ( kanisa ) ambao watakuja na
Yesu ili kutawala pamoja nae. Watakatifu watakaotoka kwenye dhiki wataungana na
wale ambao Yesu aliwatwaa duniani wakati wa unyakuo wa kanisa miaka saba
iliyopita dhiki kubwa ikiendelea duniani na wote kwa pamoja watatawala na Yesu
duniani kwa miaka elfu moja.. AGANO LA MUNGU NA WANA WA ISRAELI ( KUMBUKUMBU LA TORATI 4:30-31 ). Wakishakupatwa
na mambo hayo yote wakati wa dhiki kubwa, hatimaye Taifa la Israeli litamrudia
Bwana. Mungu alijitambulisha kwao kuwa yeye ni Mungu wa Ibrahimu, Isaka na
Yakobo. Mungu hatasahau agano aliloagana na baba zao Ibrahimu, Isaka na Yakobo
( YEREMIA 30:7). Yakobo ni Israeli. AGANO LA MUNGU NA WANA WA ISRAELI (
EZEKIELI 20:37; YEREMIA 30:7; TORATI 4:30-31) UFAFANUZI WA AGANO LA MUNGU NA
WAISRAELI ( WARUMI
11:25-27 ). Paulo mtume aliyepewa wingii
wa mafunuo kwake tunajifunza mambo ya siku za mwisho ( WARUMI 11:25-27 )
Utimilifu wa mataifa uwasili inazungumzia kunyakuliwa kwa kanisa. Majira
tuliyonayo sasa yanaitwa majira ya mataifa. Kwasababu ni wakati wa majira ya
mataifa ndiyo maana sasa wana wa Israeli ni wagumu sana kuukubali wokovu.
Kuhubiri injili Israeli ni ngumu sana kuliko sehemu nyingine yoyote duniani (
WARUMI 11:25-27, 27-32 ). Hivyo Israeli wote wataokoka.
Katika miaka mitatu na nusu ya kwanza, wana wa Israeli
watakuwa na unafuu kutokana na agano la uongop ambalo watakuwa wamelifanya na
mpinga Kristo Lakini miaka mitatu na nusu iliyosalia , chukizo la uharibifu
litasisimama kikamilifujuu ya Israeli ( DANIELI 9:27; MATHAYO 24:15-21 ). Baada
ya miaka mitatu na nusu ya kwanza, mpinga Kristo atavunja agano lake paoja na
wana wa Israeli. na kuwatesa kipekee ili wao nao wakubari kumsujudia Mpinga
Kristo kama mataifa mengine wanavyofanya. Maandiko hayo yanawazungumzia
wayahudi na siyo sisi watanzania ( mataifa ). Biblia katika ( MATHAYO 24: 16 )
inasema kuwa waliop[o uyahudi wanapaswa kukimbilia milimani ili kukwepa
kumsujudia Mnyama. Hapa Yesu anazungumzia watu wa Uyahudi ( Israeli ). Hao
watakaoikwepa namba 666 ndio watakatifu wanaotoka katika dhiki kubwa. Yesu anasema ole ni kwa
Wanyonyeshao, wenye mamba maana hao
watashindwa kumkimbia Mpinga Kristo na kukamatwa na majeshi yake. Pia
anawaambia Waisraeli waombe siku hiyo isitokee siku ya sabato maana waisraeli
ni washika sabato. Katika sabato huwa kuna mwendo wa sabato ( MATENDO 1:12 ).
Wakati wa sabato, mtu anatakiwa kutembea mwendo wa sabato chini kidogo ya maili
moja.. YUmbali kutoka mlima zeituni hadi Yerusalemu ni mwendo wa sabato.
Waisraeli wanatakiwa kuomba siku hiyo isitokee siku ya sabato wasije wakashika
sheria ya sabato ya kutembea mwendio chini kidogo ya maili moja na kushindwa
kumkimbia mpinga Kristo ( MATHAYO 24;21-22 ).
Siku za dhiki kubwa zimefupishwa kwa ajili ya wateule ambao
Mungu amekusudia kuwaokoa kutokana na agano ambalo tuekwisha kuliona. Walimu
wengine wanachanganya kwasababu ya neno wateule wanafikiri kuwa neno hilo
linazungumzia sisi tuliookolewa leo. Neno mteule linapotumika katika biblia, linatumika katika namna nne tofauti:-
( I ). Yesu Kristo
( ISAYA 42:1 )
( ii ). Malaika wateule
( 1 TIMOTHEO 5:21 )
( iii ) Sisi tuliookoka
( TITO 1:1; 1 PETRO 1:1-2; WARUMI 8:33; LUKA 18:7 )
( iv ) Wateule vilevile ni Taifa la Israeli ( ISAYA 65:8-9; ISAYA 45:4 )..
Tunatakiwa kupambanua vizuri ili tusichanganye mambo na kujikuta tunafundisha watu uongo bila
kujua ( YAKOBO 3:1 ).
( II ). Kuleta
hukumu ya adhabu kwa watu wote ambao hawakuukubali wokovu ( waliokuwa wakisema
hakuna kuokoka duniani na kumkataa Mwokozi Yesu anayeokoa)
( ISAYA 26:20-21; 2 WATHESALONIKE 2: 7-12 )
Kwasababu hawakutaka kuipenda ile kweli wapate kuokolewa,
ghadhabu ya Mungu itashuka kwao.
( 2 WATHESALONIKE 2:10-12 )
Nguvu ya upotevu ni nguvu ya mpinga Kristo na ishara zake.
Watu wote walioukataa wokovu , Mungu mwenyewe atawaletea nguvu ya upotevu ili
wauamini uongo wa mpinga Kristo wasije
wakaokolewa. Mataifa mengine yote isipokuwa Israeli pekee, watampokea mpinga
Kristo, watamwabudu, watamsujudia na wataipokea chapa yake ya 666. Watu ambao
siyo waisraeli hawatakuwa na nafasi ya
kutubu na kuokolewa. Majira ya mataifa yatakuwa
yamekwisha kupiita wakati wa unyakuo wa kanisa.. Wakati tulionao ndio
wakati ambao ni majira ya mataifa, tunaweza kuokoka sasa kwa kuwa parapanda ya
Bwana kwa ajili ya unyakuo wa watakatifu ( kanisa ) bado haijalia. Yesu Kristo
alikuja kwa waliowake (Waisraeli ) lakini waliowake wakamkataa ( hawakumpokea )
YOHANA 1:11. Ndipo alipoamua kuwageukia mataifa ( MATHAYO 28:19-20; MATENDO 1:8
).. Wakati tulionao ni wakati wa neema kwa mataifa ( hatukustahili ) lakini
kanisa likinyakuliwa utakuwa ni utimilifu au mwisho wa neema ya wokovu kwa
mataifa. Huo unaitwa utimilifu wa mataifa
( WARUMI 11:25-32 ).. Katika andiko hilo kuna siri kubwa sana na ni siri
ambayo shetani hataki watu waijue ili wazidi kudanganyika eti na mataifa
wataokoka katika dhiki kubwa kumbe siyo kweli. Mataifa yote isipokuwa Israeli
tumepewa nafasi moja tu ( one chance )
na hakutakuwa na wokovu kwa mataifa.
( VI ). HALI
ITAKAVYOKUWA WAKATI WA DHIKI KUBWA
Itakuwa ni kilio na kusaga meno. Kutakuwa na mateso na dhiki
ambayo yatafanya watu wauawe na damu yao kumwagwa kama mavumbi na nyama yao
kama mavi. Hatakuwepo mtu wa kumlilia mwenzake wala wa kuzika mwenzake, wote
watakuwa katika hali nzito ya mateso na dhiki kuu ambayo haina mfano wake. ( SEFANIA 1:15, 17-18 ). Dhiki italetwa
kwasababu watu wamemtenda Bwana dhambi, huu ni uthibitisho kwamba sisi
tuliookolewa leo hatutakuwepo wakati wa dhiki kubwa.. Watu watateswa mateso makuuu na wengi watakufa na miili yao
haitazikwa maana kila mtu atakuwa katika dhiki hiyo na hakutakuwepo na mtu wa
kumlilia mwenzake maana kila mmoja atakuwa anajililia mwenyewe. Miili ya watu
watakaouawa itakuwa samadi juu ya uso wan chi (YEREMIA 25:33). Watu leo
wanatenda dhambi na utadhani Mungu hayoko lakini hasira yake Mungu imewekwa akiba
, iefichwa kwa ajili ya wakati ule wa dhiki kubwa ( SEFANIA 2:1-3 ) Akiba ya hasira ya Mungu itafunuliwa
wakati wa dhiki kubwa. Leo mtu anaweza kusema hakuna kuokoka, hakuna Mungu,
Yesu siyo Mungu, Yesu hakuja katika mwili n.k, lakini siku ile utalia sana na
kusaga meno kutokana na mateso yatakayokuwepo ambayo hayana mfano wake tangu
kuumbwa kwa ulimwengu na hayatakuwako tena.
MAPIGO YATAKAYOMWAGWA JUU YA WANADAMU WAKATI WA DHIKI KUBWA
Mapigo saba ( vitasa saba vya ghadhabu ) yatamwagwa juu ya
wanadamu wakati wa dhiki kubwa. Hali itakuwa nzito kwa mateso makuu
yatakayokuwepo wakati huo. ( UFUNUO
15:1; UFUNUO 16;1-6 )
1. Jipu baya bovu (
UFUNUO 16:1-2 )
Watu duniani watakuwa na majipu mabaya, yanayotoa usaha na
harufu mbaya sana. Wataumizwa sana kwa majipu hayo kuliko wakati wa Ayubu.
2. Maji yote yatageuzwa kuwa damu (.UFUNUO 16;3-6 ).
Chemchemi zote zitatoa damu. Bahari, Maziwa na Mito vyote
vitageuzwa kuwa damu. Wanadamu watanyweshwa damu kwasababu ya damu ya watakatifu
iliyomwagwa .Watu waliwaua manabii na mitume hivyo watanyweshwa damu kwa sababu
hiyo. Damu itakuwa nzito kiasi kwamba mtu akiinywa ataweweseka mara moja na
kuanguka chini na kuzimia. Itakuwa ni
hali nzito sana kunywa damu wakati ule. Viumbe vyote viishivyo baharini,
kwenye maziwa na mito vitakufa kutokana na maji yote kuwa damu. Kutakuwa na
harufu ya kutisha kutokana na viumbe vyote kufa.
3.. Jua litashushwa karibu sana na uso wa dunia ( UFUNUO
16:8 )
Jua lina joto kiasi cha sentigredi 1,000,000 unaweza kuona jinsi mates ohayo ya kuunguzwa na joto
hilo yatakavyokuwa makubwa sana. Ndiyo maana watu wengi watakufa wakati wa
dhiki kubwa. Watu watamtukana Mungu kwa maunguzo hayo ya jua.
4. Matatameko , umeme
na radi vitaachiliwa na Mungu juu ya uso
wa dunia. ( UFUNUO 16:18 ).
Matetemeko hayo yanatajwa kuwa hayajawahi kutokea tangu
dunia kuwako. Matetemeko yanayoripotiwa katika vyombo vya habari ambayo
yanasababisha maafa makubwa katika mataifa mbalimbali ni matetemeko madogo sana
ukilinganisha na matetemeko yatakayoletwa na Mungu mwenyewe wakati wa dhiki
kubwa. Umeme na radi vitakuwa ni sehemu ya mateso kwa wanadamu walioukataa
wokovu na kuachwa duniani wakati wa unyakuo wa kanisa.
5. Mvua ya mawe makubwa
( UFUNUO 16:21 )
,Mawe yanatajwa kuwa na uzito wa taranta. Taranta moja ni
sawa na kg 53 za uzito. Watu watamtukana sana Mungu kutokana na mates ohayo yam
awe.
6. Nzige wenye sumu kali
( UFUNUO 9:2-6 )
Nzige wenye sumu kali kama ya kuumwa na nnge watakuwepo
wengi duniani kwa muda wote wa dhiki kubwa ili kuwatesa wanadamu walioukataa
wokovu wa Yesu. Wakati wote watu watakuwa wakiumwa na Nzige hao.
7. Kutakuwa na giza
kuu juu ya uso wa dunia
( UFUNUO 16:10 )
( VII ). JINSI YA KUIKWEPA DHIKI HII KUBWA .
Kila anayetaka kuikwepa dhiki hii kubwa hana budi kujificha ndani na kufunga milango
yote kama vile wakati wa Safina ya Nuhu. ( ISAYA 26:20 )
Kwa kufanya yafuatayo:-
( i ) . Kuhakikisha tunatubu dhambi zetu zote kwa kumaanisha
kuziacha na kuokolewa kwa kumwamini mwana wa Mungu Yesu Kristo. ( MITHALI 28:13
) “ Afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeye aziungamaye na kuziacha
atapata rehema”. ( YOHANA 3:36 ) “
Amwaminiye mwana wa Mungu hahukumiwi”.
( ii ) Kukaa ndani ya
Yesu Kristo na kulifuata neno lake na maagizo yake yote ( ZABURI 119:9; ZABURI
119:6 )
( iii ) Kukaa mahali ambapo kuna mafundisho ya kweli ya neno
la Mungu. Tuwe tayari kufata kila
tunaloelezwa ambalo ni la kibiblia. Tukiambiwa kumwacha mke wa pili au mume wa
pili tuwe tayari. Dhiki utakayoipata kwa kumwacha huyo mume au mke wa mtu
mwingine ni ndogo sana ukilinganisha na dhiki kubwa inayokuja. Tukiambiwa
tuache kuvaa mavazi ya kidunia ( kikahaba ) tusiwe wabishi. Watu wanapoelezwa
kuhusiana na mapambo kwamba hayatakiwi kuvaliwa na mtu aliyeokoka wao
wanawasikiliza walimu wao wa uongo ambao siku zote wanachanganya mafundisho kwa
kutojua kweli ipasavyo. Mapambo yamekatazwa ( 1 TIMOTHEO 2:9-10; 1 PETRO 3:3-5;
MWANZO 35:1-5; KUTOKA 33:4-6; EZEKIELI 23:26-30,40, 42; ISAYA 3:16-24; HOSEA
2:13; YEREMIA 4:30, 2 WAFALME 9:30-37, UFUNUO 2:20).
Wanawake wasivae mavazi yawapasayo wanaume wala wanaume
kuvaa mavazi yanayowapasa wanawake, kufanya hivyo ni machukizo kwa Bwana (
KUMBUKUMBU LA TORATI 22:5 ). Suruali ni vazi la wanaume kibiblia. Sehemu zote
zinazotaja suruali katika biblia inatajwa ikiwa imevaliwa na wanaume. Walimu wa
uongo wanawafariji wanawake wapenda dunia ( 1 YOHANA 2:15-17, YAKOBO 4;4 )
waendelee kuvaa suruali eti hazina shida. Hao ni watumishi wa Shetani ambao
wapo kwa mfano wa watumishi wa haki ( 2 WAKORINTHO 11:14 )
Ukiambiwa kubatizwa katika maji tele usibishe ndivyo
inavyotupasa ( YOHANA 3:23; WAKOLOSAI 2:12 ). Lazima uzamishwe katika maji kama
kuzikwa kwa Yesu ili tushiriki mauti yake.
( iv ). Kukesha wakati wote na kuyatunza mavazi meupe ya utakatifu. Doa dogo tu husababisha uchafu
( WIMBO ULIOBORA 2:15 ). Lazima tujihadhari na Mbweha wadogo. Dhambi
tunazoziona ndogo zinaweza kutuingiza katika dhiki kubwa. Adamu na Hava
walifanya dhambi ambayo tungeweza leo kuiita dhambi ndogo. Walikula matunda
katika mti waliokatazwa na Mungu lakini adhabu waliyopewa ni kubwa mno kwa kosa
hilo tu. Wachungaji na walimu wengi wa uongo , wanaotumiwa na shetani wanaweza
kukwambia siyo shida kufanya hili au lile kwa namna ileile ya nyoka
alivyowadanganya Adm na Hawa ( MWANZO
3:1-19 ). Mpendwa msomaji, baada ya kusikia yote haya kutoka kwa nabii
aliyetumwa kukuletea ujumbe huu, usifanye moyo wako kuwa mgumu. Hii ni nafasi ya kipekee ya kuokoka. Je, unajuaje kama utaamka kitandani baada ya
kulala usiku wa leo? Wakati uliokubalika
wa wokovu ni sasa (2 WAKORINTHO 6:2).
Labda utaniuliza, ili uokoke, ufanyeje?
Jibu ni rahisi, kwa imani ukitubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha,
na kumwambia Yesu Kristo akusamehe, utasamehewa sasa hivi, na msamaha wa
dhambi, huambatana na wokovu (LUKA 1:77).
Je, uko tayari kuokoka sasa hivi?
Najua uko tayari. Basi fuatisha sala hii kwa dhati toka moyoni, “Mungu
baba asante kwa kuniletea ujumbe huu.Natubu dhambi zangu zote, kwa kumaanisha
kuziacha. Yesu Kristo nakuomba unisamehe dhambi zangu na kunipa uwezo wa
kushinda dhambi na kuniokoa kutoka katika mateso ya moto wa milele. Asante, kwa
kuniokoa katika Jina la Yesu.
Amen”. Tayari sasa umeokoka, na
kwa hakika unakwenda mbinguni sasa, hata ukifa leo. Ili uzidi kuukulia wokovu, hakikisha
unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu. MUNGU AKUBARIKI !!! (FULL GOSPEL)
No comments:
Post a Comment