Ina maana gani kwamba mshahara wa dhambi ni mauti?

Warumi 6:23 inasema, "Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu." Katika msingi wake, dhambi ni uasi dhidi ya Mungu. Dhambi zetu hututenganisha na Mungu, Muumba na mwenye uzima. Yesu alisema, "Mimi ndimi njia na kweli na uzima" (Yohana 14: 6). Mungu anajulikana kama "MIMI NDIMI" mkuu. Uzima uu katika Mungu. Kwa hivyo, tunapofanya dhambi na kujitenganisha na Mungu, tunatengana na uzima wa kweli. Kwa hivyo, bila shaka, tunakumbana na mauti. Hoja tatu za ufafanuzi zinahitajika: Kwanza, dhambi hasa haisababishi kifo cha kimwili mara moja. Warumi 6 haituambii kwamba tunapofanya dhambi tutakufa kimwili. Badala yake, inarejelea kifo cha kiroho. Pili, wakati tunapookoka katika Kristo, tunaokolewa kutokana na hatima ya kifo cha kiroho na kuletwa katika hatima ya uzima wa kiroho. Paulo aliwaambia Warumi, "Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu" (Warumi 6:23). Tatu, hata dhambi za waumini bila shaka zitasababisha aina ya "kifo" cha kiroho. Ingawa tumeokolewa kutokana na adhabu ya mwisho ya dhambi (kutengwa kwa milele na Mungu), hatuokolewa kutokana na matokeo ya asili ya uhusiano uliovunjika na Baba . Tunapofanya dhambi, tunapata dalili za kifo cha kiroho. Tunaweza kujihisi kuwa na hatia, kuwa wapungufu, kuchanganyikiwa, au kutokuwa na uhusiano na Mungu. Sisi hufanya kama waadilifu badala ya kuwa wenye haki. Dhambi zetu, hata kama waumini, huumiza moyo wa Mungu na uhuzunisha Roho Wake (Waefeso 4:30). Ingawa dhambi zetu haziachi uhusiano wetu na Yeye, huweka kizuizi kati yetu. Fikiria mtoto na mzazi. Wakati mtoto anapoasi, uhusiano na mzazi wake unafadhaika. Mzazi bado anampenda mtoto na bado ana nia bora kwa mtoto moyoni. Mtoto kamwe aachi kuwa bila mzazi. Hata hivyo, mtoto anaweza kupata matokeo fulani: kutoaminiwa, nidhamu, hisia ya hatia, na kadhalika. Bila shaka hatimaye uhusiano hurejeshwa ila kawaida pigo huja kwanza. Hivyo ni pamoja nasi na Mungu. Tunapoasi dhidi ya utawala wa Mungu katika maisha yetu, tunaasi dhidi ya Uzima, na hivyo tunakumbana na mauti (kuvunjika kunaosababisha maumivu). Tunapomrudia Mungu, tunarudishwa tena kwenye ushirika wa kiroho na Mungu, hisia za lengo, haki, uhuru, nk. Baba mwenye furaha katika mfano wa Mwana mpotevu alisema vizuri zaidi: "Huyu mtoto wangu alikuwa amekufa na yu hai tena "(Luka 15:24).

HAZINA ILIYOSITIRIKA NA MFANYABIASHARA

 

HAZINA ILIYOSITIRIKA NA MFANYABIASHARA

 (MATHAYO 13:44-46)

 

Katika mistari hii Yesu anatufundisha juu ya Ufalme wa mbinguni kwa kutumia mifano miwili.  Hazina iliyositirika, na mfanyabiashara mwenye kutafuta lulu nzuri.  Kuna mengi ya kujifunza katika mifano hii tunapoichambua mmoja baada ya mwingine.

 

(1)              HAZINA ILIYOSITIRIKA  (MST. 44)

 

Katika mfano huu, HAZINA ni Taifa la Israeli (ZABURI 135:4; MALAKI 3:17).  MTU anayeitafuta hazina hii ni Yesu Kristo mwenyewe (LUKA 19:10; MATHAYO 15:24; MATHAYO 10:6).  Hazina hii imesitirika au imefichika katika SHAMBA.   Shamba hili ni Ulimwengu (MATHAYO 13:38).  Yesu alipokuja kwa Waisraeli, hawakumpokea, WALIJIFICHA (YOHANA 1:11; MATHAYO 23:37-39; WARUMI 10:16, 19-21).  Baada ya Yesu kuiona hazina iliyositirika katika shamba, yaani kuwaona Waisraeli wamejificha kwa kukataa kumpokea, alilinunua shamba lote, yaani ulimwengu wote.  Kwa damu yake iliyomwagika msalabani, aliununua ulimwengu wote na siyo taifa la Israeli tu (YOHANA 11:49—52; MATHAYO 21:43; 1 WAKORINTHO 6:19-20;  MATENDO 20:28; 2 PETRO 2:1; WARUMI 11:11-12).  Hazina hii ingawa Yesu ameiona, bado imefichika mpaka wakati Yesu atakapokuja mara ya pili duniani na wakati huo hazina ya Mungu, Waisraeli wote, watakaokuwa hai wakati huo; wataokoka (WARUMI 11:25-32).

 

MAMBO YA ZIADA YA KUJIFUNZA KATIKA MFANO HUU

 

    Mambo mengi ya Ufalme wa Mungu ambayo ni hazina, yamesitirika, ni mafumbo.  Yako chini sana ya ardhi.  Hayako juujuu tu.  Inabidi kuchimba sana chini kwa maombi, kusoma na kujifunza Neno, kujitenga na ulimwengu n.k.; na kuyatafuta kwa bidii ili kuyapata                          (LUKA 6:48;       DANIELI 2:22; 1 WAKORINTHO 2:10).

    Tukitaka kuwa Watumishi wa Mungu wakubwa kwa kumletea hazina kubwa Yesu Kristo katika uvuvi wetu wa watu, ni lazima tufahamu kwamba samaki wengi wakubwa baharini hawapatikani ufukoni tu, wanapatikana kilindini, chini sana ya bahari.  Ni lazima tuwe tayari kwenda kilindini kwa maombi na kujitoa kwetu katika muda, fedha, na kuhubiri kwa wakati unaofaa na usiofaa, tukizidi kupanda neno ndani ya watu (LUKA 5:4-7).  Tupande Neno ndani ya watu asubuhi na jioni kila siku, hatimaye mavuno mengi ni dhahiri (MHUBIRI 11:6).

    Injili imesitirika au imefichwa kwa watu ambao hawajaokoka.  Inabidi mtu afunuliwe ili alielewe Neno la Mungu (2 WAKORINTHO 4:3-4;             MATHAYO 11:25-27).  Ni juu yetu kuchimba chini sana kwa maombi ili watu waijue kweli.

    2.                 MFANYABIASHARA MWENYE KUTAFUTA LULU NZURI (MST. 45-46)

 

LULU, ni aina fulani ya madini ya thamani kubwa ambayo hupatikana katika wanyama fulani wa baharini wenye gamba au kombe wa aina ya chaza (oyster).  Lulu hizi hupatikana kutoka kwa wanyama hawa wanapopatwa na aina fulani ya maradhi yanayosadikika kuchukua miaka saba.  Kama lulu hizo hazipatikani katika kipindi hicho wanyama hao hufa, na lulu zikapotea.  Thamani ya lulu moja, ni karibu US $ 400,000, ambazo ni karibu TShs. 200,000,000.  Kuingia mbinguni ni kama kupata lulu nzuri yenye thamani kubwa kuliko hata maisha yetu hapa duniani (MATENDO 20:24).  Imani halisi ya wokovu, ni ya thamani kama lulu (2 PETRO 1:1).  Ahadi ya Yesu aliyosema amekwenda kutuandalia makao, ili pale alipo sisi nasi tupate kuwapo (YOHANA 14:1-3); ni ya thamani sana kwetu kama lulu                     ( 2 PETRO 1:4).  Watu wanaangamizwa kwa kukosa na kuyakataa maarifa (HOSEA 4:6).  Maarifa ya Neno la Mungu ni ya thamani kama lulu (MITHALI 20:15).  Maarifa haya ndiyo ambayo hatimaye yatatufanya tuuone mji wa mbinguni Yerusalemu mpya uliojengwa kwa lulu (UFUNUO 21:21).  Tunapaswa kuwa kama mfanya biashara mwenye kutafuta lulu hii – imani hii na maarifa haya na tukiipata, tuuze vyote tulivyo navyo na kuinunua.  Mfanyabiashara ana sifa saba zifuatazo:

 

    Hutangatanga kutafuta mali.  Tuwe tayari kutangatanga na kuwa tayari kuliacha kanisa lisilofundisha kweli.  Hilo silo lulu.  Mfanyabiashara haendelei na biashara isiyompa faida kwa sababu ya kuizoea tu!

    Huwa tayari kufuata mali hata kama iko mbali.  Tusiridhike tu kusali kwenye makanisa ya karibu.  Tuweke mtaji mkubwa, tuwe tayari kutoa nauli kubwa kufuata Kanisa linalotupa maarifa kama Malkia wa Kusini (MATHAYO 12:42);

    Huwa tayari kutoa muda wote, nguvu zake zote na hata kupata mateso na dhiki ili apate mali.  Tufanye vivyo hivyo ili tuupate ufalme wa mbinguni.

    Hujikana nafsi yake, hujinyima hata usingizi na anasa za ulimwengu ili apate mali na asifilisike.  Sisi nasi tujikane nafsi zetu ili tuupate ufalme wa mbinguni (LUKA 9:23-25);

    Huwa tayari kuwaacha ndugu, mke, wazazi, marafiki na kwenda mbali kusiko na ndugu na kukaa huko miaka mingi kutafuta mali.  Vivyo hivyo tunapaswa kuwa tayari kuacha vyote ili kuupata ufalme wa mbinguni (LUKA 14:25-26, 33);

    Huwa na watu wanaomjia kumshawishi ili amalize fedha zake kama malaya n.k; na pia huwa macho kujilinda na wezi wanaopanga kumwibia mali zake.  Sisi nasi tukeshe na kuomba ili kujilinda na wezi na malaya wanaotaka kuiba lulu zetu.  Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji (lulu) yako;

    Haridhiki au hatosheki na fedha hata kama anazo kiasi gani.  Tunapaswa kujiona hatuna kitu wakati wote (WAGALATIA 6:3) na kujiona kwamba hatujafika wala hatujawa wakamilifu (WAFILIPI 3:12-15).  Tudumu kuwa tayari kujifunza Neno la Mungu wakati wote.  Tusitosheke na viwango vya Utakatifu na utendaji kazi tulivyo navyo mpaka tufikie kimo na cheo cha utimilifu wa Kristo (WAEFESO 4:15).

 

Yesu aliwauliza, Mmeyafahamu hayo yote?  Wakamwambia, Naam (MATHAYO 13:51).

 

Ikiwa umeyafahamu, PIGA VITA VIZURI VYA IMANI, ILINDE IMANI YA WOKOVU KAMA LULU.  TUONANE PARADISO KWENYE

 

Usikose faida zilizomo katika somo”PUNJE YA HARADALI NA CHACHU” katika link hiihttps://davidcarol719.wordpress.com/punje-ya-haradali-na-chachu/

 

…………………………………………………………………………………………………………………………………..

 

Ni sifa ipi ya kutuwezesha kuingia mbinguni?  Ni utakatifu (WAEBRANIA 12:14).  Ndani yake hakitaingia kamwe chochote kilicho kinyonge (UFUNUO WA YOHANA 21:27).  Kinyonge ni kipi?  Ni yule anayetenda dhambi.  Huyu ni mtu asiyefaa, ni mnyonge!  Je, wewe ni mtakatifu?  Jibu ni la!  Maisha yako yamejaa dhambi, pamoja na kusema una dini; hivyo wewe pia ni mnyonge, hufai kuingia mbinguni. Ukitubu leo dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na kuifuata njia ya Yesu Kristo, ndipo utakapopata rehema ya kuingia mbinguni (MITHALI 28:13;  YOHANA 14:6).  Je, uko tayari kutubu sasa ili upate rehema hii?  Najua uko tayari.  Basi fuatisha sala hii ya toba kwa dhati kutoka moyoni;  “Mungu Baba asante kwa ujumbe huu.  Hakika mimi ni mnyonge, mwenye dhambi.  Sistahili kuingia mbinguni. Natubu dhambi zangu zote kwa kumaanisha kuziacha.  Kuanzia leo nataka niifuate njia ya Yesu Kristo.  Bwana Yesu niwezeshe.  Asante kwa kunisikia katika Jina la Yesu.  Amen”.  Mpendwa msomaji umekubaliwa kuingia mbinguni.  Ili uzidi kudumu katika utakatifu mpaka siku ya kuiaga dunia hii, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu.  MUNGU AKUBARIKI !!!   FULL GOSPEL

 

No comments: