Ina maana gani kwamba mshahara wa dhambi ni mauti?

Warumi 6:23 inasema, "Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu." Katika msingi wake, dhambi ni uasi dhidi ya Mungu. Dhambi zetu hututenganisha na Mungu, Muumba na mwenye uzima. Yesu alisema, "Mimi ndimi njia na kweli na uzima" (Yohana 14: 6). Mungu anajulikana kama "MIMI NDIMI" mkuu. Uzima uu katika Mungu. Kwa hivyo, tunapofanya dhambi na kujitenganisha na Mungu, tunatengana na uzima wa kweli. Kwa hivyo, bila shaka, tunakumbana na mauti. Hoja tatu za ufafanuzi zinahitajika: Kwanza, dhambi hasa haisababishi kifo cha kimwili mara moja. Warumi 6 haituambii kwamba tunapofanya dhambi tutakufa kimwili. Badala yake, inarejelea kifo cha kiroho. Pili, wakati tunapookoka katika Kristo, tunaokolewa kutokana na hatima ya kifo cha kiroho na kuletwa katika hatima ya uzima wa kiroho. Paulo aliwaambia Warumi, "Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu" (Warumi 6:23). Tatu, hata dhambi za waumini bila shaka zitasababisha aina ya "kifo" cha kiroho. Ingawa tumeokolewa kutokana na adhabu ya mwisho ya dhambi (kutengwa kwa milele na Mungu), hatuokolewa kutokana na matokeo ya asili ya uhusiano uliovunjika na Baba . Tunapofanya dhambi, tunapata dalili za kifo cha kiroho. Tunaweza kujihisi kuwa na hatia, kuwa wapungufu, kuchanganyikiwa, au kutokuwa na uhusiano na Mungu. Sisi hufanya kama waadilifu badala ya kuwa wenye haki. Dhambi zetu, hata kama waumini, huumiza moyo wa Mungu na uhuzunisha Roho Wake (Waefeso 4:30). Ingawa dhambi zetu haziachi uhusiano wetu na Yeye, huweka kizuizi kati yetu. Fikiria mtoto na mzazi. Wakati mtoto anapoasi, uhusiano na mzazi wake unafadhaika. Mzazi bado anampenda mtoto na bado ana nia bora kwa mtoto moyoni. Mtoto kamwe aachi kuwa bila mzazi. Hata hivyo, mtoto anaweza kupata matokeo fulani: kutoaminiwa, nidhamu, hisia ya hatia, na kadhalika. Bila shaka hatimaye uhusiano hurejeshwa ila kawaida pigo huja kwanza. Hivyo ni pamoja nasi na Mungu. Tunapoasi dhidi ya utawala wa Mungu katika maisha yetu, tunaasi dhidi ya Uzima, na hivyo tunakumbana na mauti (kuvunjika kunaosababisha maumivu). Tunapomrudia Mungu, tunarudishwa tena kwenye ushirika wa kiroho na Mungu, hisia za lengo, haki, uhuru, nk. Baba mwenye furaha katika mfano wa Mwana mpotevu alisema vizuri zaidi: "Huyu mtoto wangu alikuwa amekufa na yu hai tena "(Luka 15:24).

JINSI YA KUFAHAMU MIUJIZA YA SHETANI

 JINSI YA KUFAHAMU MIUJIZA YA SHETANI

Nyakati tulizonazo leo,zinzitwa NYAKATI ZA HATARI..Biblia inasema kwamba siku hizi za mwisho,wengine watajitenga na imani,wakisikiliza ROHO ZIDANGANYAZO na MAFUNDISHO YA MASHETANI (2TIMOTHEO 3:1,1TIMOTHEO 4:1).Roho zidanganyazo zitafanya kila namna,kutudanganya,ili kile cha Mungu tukiite cha shetani,na kile kilicho cha shetani,tukiite cha Mungu.Leo,tunazungukwa na watu wanaosema,jihadhari usiende kule.Ingawa kuna miujiza mingi huko,miujiza hiyo,inatokana na ROHO CHAFU au MASHETANI.Mtu yule,anatoa pepo kwa kutumia DAWA au HIRIZI.Kutokana na mambo yake ya ushirikina,mtu akienda kumsikiliza mara moja tu,yeye naye ananyweshwa roho chafu na kudanganyika.Maneno haya,yanaweza yakawa ya kweli au yasiwe ya ukweli.Pasipokuwa na mafundisho,hatuwezi kupambanua kilicho cha Mungu na kilicho cha Shetani.Pasipo kuoambanua,tunaweza tukamwita mtu wa Mungu kuwa ni PEPO na kwamba anatoa pepo kwa BEELZEBULI,mkuu wa pepo,kwasababu tu HAFUATANI NASI (YOHANA 8:48-49; MATHAYO 12:22-24;LUKA 9:49-50).Mambo haya,hayapaswi kuwa hivi.Kwa sababu hii basi ni makusudi ya Mungu ujifunze somo hili.Tunaligawa somo hili katika vipengele vitatu;-

 

UWEZEKANO WA SHETANI KUFANYA MIUJIZA.

JINSI YA KUIFAHAMU MIUJIZA YA MUNGU.

HUKUMU YA WATUMISHI WA SHETANI

1.UWEZEKANO WA SHETANI KUFANYA MIUJIZA.

 

Shetani, ana uwezo wa kufanya ishara na miujiza kadhaa,kwa kipimo kidogo cha uwezo ulio na mpaka.Roho chafu,roho za mashetani,zina uwezo wa kufanya ishara (UFUNUO 16:13-14).Wakati wa dhiki kubwa,roho za mashetani,zitafanya ishara kubwa,hata kufanya moto kutoka mbinguni uje juu ya nchi mbele ya wanadamu (UFUNUO 13:11-13).Wakati wa wana wa Israeli, walipokuwa hawajatoka Misri,waganga na wachawi wa Farao,walifanya miujiza kwa uwezo wa Shetani:-

 

(a).  Wachawi hao,walipozibwaga fimbo zao chini,ziligeuka kuwa nyoka kwa mfano wa muujiza alioufanya Mungu kwa kuwatumia Musa na Haruni (KUTOKA 7:8-12).

 

(b)  Wachawi hawa,walifanya muujiza wa kubadili maji kuwa damu,kwa mfano wa muujiza alioufanya Mungu kwa kuwatumia Musa na Haruni (KUTOKA 7:19-22)

 

Hata hivyo,pamoja na wachawi na waganga  hawa kufanya miujiza hii,walikuwa na mpaka katika uwezo wao.Wachawi hawa,walishindwa kufanya mavumbi ya nchi kuwa chawa kwa mfano wa Musa na Haruni,na vulevile walishindwa kuzuia majipu yaliyosababishwa na muujiza wa Mungu kupitia kwa Musa,kuwapata na wao pia.Wakakiri kwamba uwezo wa Mungu uko juu mno kuliko uwezo wao (KUTOKA 8:16-19;9:8-11).Shetani hana uwezo wote,hawezi kutenda mambo yote.Mungu wetu ana uwezo mkuu mno.Fimbo ya Haruni,ilizimeza fimbo za wachawi,kudhihirisha uwezo wa Mungu ulivyo mkubwa mno kuliko majeshi yote ya Shetani (KUTOKA 7:11-12).Ni muhimu kufahamu kwamba miujiza ya Shetani,inalengo la KUWAPOTEZA,kama yamkini hata walio wateule.Ni nguvu ya upotevu,ya kuwafanya wale wote wasioipenda kweli ya Neno la Mungu KUPOTEA (MATHAYO 24:24;2WATHESALONIKE 2:7-12).Ili basi tusipotezwe na roho hizi za mashetani,ni muhimu kuifahamu Kweli,ili tuweze kupambanua miujiza ya mashetani na miujiza ya Mungu.Hili sasa linatuleta katika kipengele cha pili cha somo letu.

 

2. . JINSI YA KUIFAHAMU MIUJIZA YA MUNGU.

 

Ili kuifahamu na kuipambanua miujiza ya mashetani.itakuwa vema kujifunza alama zitakazotuwezesha kuifahamu miujiza ya Mungu.Tukiweza kufahamu namna ya kupambanua miujiza ya Mungu,itakuwa ni rahisi kufahamu kinyume chake,na kuifahamu miujiza ya mashetani.ZIKO ALAMA KUMI (10) za kutuwezesha kuifahamu miujiza ya Mungu.Alama zote hizi,lazima zionekane katika huduma yoyote inayotumiwa na Mungu kufanya miujiza.Tukiziona alama zote hizi kumi katika huduma yoyote ya miujiza,tujue huduma hiyo niya Mungu,na hatupaswi kusema mtu huyo wa Mungu anatumia roho chafu au anatoa pepo kwa Beelzebuli,mkuu wa pepo.Alama hizi kumi ni hizi zifuatazo:-

 

1.      .Mtu anayetumiwa kufanya miujiza ya Mungu, lazima mwenyewe awe ameamini na kuokolewa; akikiri mwenyewe wokovu ulio katika Kristo Yesu, na kuushuhudia ishara au miujiza ya Mungu, hufuatana nao WAAMINIO tu, au waliookolewa (MARKO 16:17).Mtu yeyote ambaye hajaokoka, hawezi kufanya miujiza inayotokana na Mungu.Miujiza anayoifanya mtu yeyote ambaye hajaokoka, ni miujiza ya shetani.

 

2.     .Huma yoyote ya miujiza ya Mungu, lazima iambatane na Biblia au Neno la Mungu, kwa kuwa Neno la  Mungu ndiyo dawa ya ugonjwa na tena ndilo linalofanya miujiza(ZABURI 107:20; MITHALI  4:20-22; YOHANA  6:63). Mtu anayetumiwa kufanya miujiza ya Mungu, ataiamini Biblia na kuifanya kuwa msingi wa utendaji wake wote. Huduma yoyote ya miujiza isiyoambatana Biblia, inatokana na Shetani.

 

3.      Huduma yoyote ya miujiza inayotokana na Mungu, LAZIMA iambatane na KUHUBIRI NA KUFUNDISHA Neno la Mungu. Mtu yeyote anayedai kwamba yeye hakupewa kuhubiri Neno, ila amepewa karama ya kutenda miujiza tu, huyo anatumiwa na Shetani (LUKA  4:18; 5:17; 9; 8:1-2; MATHAYO  10:7-8). Huduma yoyote ya miujiza ya Mungu, lazima iambatane kuhubiri kwamba watu watubu dhambi zao na kuziacha, na kuokolewa. Kinyume cha hapo, ni huduma ya Shetani (MARKO  4:6;12-13).

 

4.      Miujiza yoyote ya Mungu, LAZIMA ifanyike kwa jina la YESU (LUKA 10:17; MATENDO 4:30; MARKO 16:17; MATENDO 3:6;  4:10;  3;13,  16, 16:18).

 

5.      Miujiza yoyote ya Mungu, hutumika kuwaleta watu kwa Bwana Yesu na kuwafanya wawe wanafunzi wa Yesu, na kuwafundisha kudumu katika kanisa linalohubiri wokovu (MATENDO 5:12, 14; 2:41-43;  6:7-8; 8:5-8, 12). Miujiza isiyo na lengo hili ni miujiza ya Shetani.

 

6.      Mtu yeyote anayetumiwa kufanya miujiza ya Mungu, lazima afanye huduma yake kwa kushirikiana na makanisa yanayohubiri wokovu, ili apate kutoa ripoti ya huduma yake inavyokwenda na kuwajibika (MATENDO 14:27; 21:17-19; 1WAKORINTHO 14:29).

 

7.      Miujiza ya Mungu, hutusogeza katika kumtumikia Yesu Kristo na kushika maagizo yake, na kutufanya kuwa watakatifu kama yeye alivyo mtakatifu. Miujiza yoyote inayoambatana na maagizo yoyote yaliyo kinyume na Neno la Mungu, kama kutumia sanamu za watakatifu, kufukiza uvumba, kutumia rozari au maji ya Baraka, kuzuru makaburi, kuwaomba wafu tuwaombee n.k; haitokani na Mungu (KUMBUKUMBU 13:1-4).Mafundisho ya mtu anayetumiwa kufanya miujiza ya Mungu, hutufundisha kuwa watakatifu, na kuwa mbali na mapenzi ya Mataifa. Wote waliotumiwa sana na Mungu kufanya miujiza kama Paulo, Petro, Yakobo na Yohana, walifundisha hivyo (WARUMI 12:1-2; 1YOHANA 2:15-17; 1 PETRO 1:14-16; 2:12; 4:2-3; YAKOBO 4:4; 1 WAKORINTHO 4:3-4).

 

8.     Miujiza ya Mungu hutolewa bure, hainunuliwi (MATHAYO 10:8; 2 WAFALME 5:14-16; DANIELI 5:16-17; 1 WAFALME 13:6-8; MATENDO 8:18-20). Namna yoyote ya kuomba hela ili kununua muujiza ni kinyume na mpango wa Mungu .Hata kama tutaona wakiuza vitambaa,leso na sabuni zilizoombewa ili zitusaidie, hatuna budi kujua mapanzi ya Mungu kwa watumishi wake ni kutoa huduma ya maombezi bure. Huduma yoyote inayochangisha mchango au kiingilio kwa ajili ya semina ya Neno la Mungu hiyo siyo huduma ya kimungu, ni huduma ya Shetani. Mungu anataka injili iwafikie watu wote.Mfano 1 wa huduma ya shetani ni huduma ya babu wa Loliondo. Bila kutoa sh: 500  usingeweza  kupata msaada.Pia miujiza ya Mungu inatokana na Neno la Mungu kama tulivyoona hapo juu. Miujiza ya Mungu inakuwa na lengo la kuwaleta watu kwa Yesu.Watu wanaokuja kutafuta msaada kwa Yesu sharti waongozwe kutubu dhambi zao

 

kwanza ili kuwapatanisha na Mungu kwa ajili ya kufungua mlangio wa Miujiza yao.

 

9.       Miujiza ya Mungu humtukuza mwana wa , Yesu kristo (YOHANA 11:4), wale wanaotumiwa na Mungu kufanya miujiza ya Mungu hubaki wanadamu na wao kukiri hivyo, na kumpa Mungu utukufu(MATENDO 14:8-18). Tunapomuona  mtu akichukua utukufu kana kwa mba yeye ndiye anayetenda miujiza ndipo tunatambua kuwa huyo si mtumishi wa Mungu.

 

10.      Maisha ya mtu anyetumiwa na Mungu kufanya miujiza yanapaswa kuwa sawasawa na Neno la Mungu. Watu wanaotumiwa na Shetani kufanya miujiza, huambatana na dhambi NNE zinazoonekana upesi-uzinzi au uasherati (1 WAKORINTHO 6:15-17), maneno ya kihuni (YAKOBO 3:10-12), maisha yaliyo sawa na mataifa katika kuvaa na kutenda (WARUMI 12:2;  1 PETRO 2:12; YAKOBO 4:4), maisha yasiyo na uaminifu katika masuala ya fedha na kusema uongo (NEHEMIA 7:2)

 

3.  HUKUMU YA WATUMISHI WA SHETANI

 

Watumishi wanaotumiwa kufanya miujiza ya mashetani, mahali pao ni katika ziwa la moto (UFUNUO 19:20; KUMBUKUMBU 13:1-5; MATHAYO 7:22-23. Baada ya kuwa tumefahamu; ni wajibu wetu kujihadhari nao na kuwa mbali na mafundisho yao (MATHAYO 7:15-17;  WARUMI 16:17).Mungu akuongoze kufanya maamuzi mazuri katika kuchagua mahali pa kuabudia (dhehebu au kanisa), maana kufanya makosav katika kuchagua mahali pa kulishwa  NENO LA MUNGU kunaweza kukugharimu milele. Tafuta mahali ambapo utaelezwa kweli yote bila kufarijiwa kunyume na maandiko.

No comments: