Ina maana gani kwamba mshahara wa dhambi ni mauti?

Warumi 6:23 inasema, "Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu." Katika msingi wake, dhambi ni uasi dhidi ya Mungu. Dhambi zetu hututenganisha na Mungu, Muumba na mwenye uzima. Yesu alisema, "Mimi ndimi njia na kweli na uzima" (Yohana 14: 6). Mungu anajulikana kama "MIMI NDIMI" mkuu. Uzima uu katika Mungu. Kwa hivyo, tunapofanya dhambi na kujitenganisha na Mungu, tunatengana na uzima wa kweli. Kwa hivyo, bila shaka, tunakumbana na mauti. Hoja tatu za ufafanuzi zinahitajika: Kwanza, dhambi hasa haisababishi kifo cha kimwili mara moja. Warumi 6 haituambii kwamba tunapofanya dhambi tutakufa kimwili. Badala yake, inarejelea kifo cha kiroho. Pili, wakati tunapookoka katika Kristo, tunaokolewa kutokana na hatima ya kifo cha kiroho na kuletwa katika hatima ya uzima wa kiroho. Paulo aliwaambia Warumi, "Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu" (Warumi 6:23). Tatu, hata dhambi za waumini bila shaka zitasababisha aina ya "kifo" cha kiroho. Ingawa tumeokolewa kutokana na adhabu ya mwisho ya dhambi (kutengwa kwa milele na Mungu), hatuokolewa kutokana na matokeo ya asili ya uhusiano uliovunjika na Baba . Tunapofanya dhambi, tunapata dalili za kifo cha kiroho. Tunaweza kujihisi kuwa na hatia, kuwa wapungufu, kuchanganyikiwa, au kutokuwa na uhusiano na Mungu. Sisi hufanya kama waadilifu badala ya kuwa wenye haki. Dhambi zetu, hata kama waumini, huumiza moyo wa Mungu na uhuzunisha Roho Wake (Waefeso 4:30). Ingawa dhambi zetu haziachi uhusiano wetu na Yeye, huweka kizuizi kati yetu. Fikiria mtoto na mzazi. Wakati mtoto anapoasi, uhusiano na mzazi wake unafadhaika. Mzazi bado anampenda mtoto na bado ana nia bora kwa mtoto moyoni. Mtoto kamwe aachi kuwa bila mzazi. Hata hivyo, mtoto anaweza kupata matokeo fulani: kutoaminiwa, nidhamu, hisia ya hatia, na kadhalika. Bila shaka hatimaye uhusiano hurejeshwa ila kawaida pigo huja kwanza. Hivyo ni pamoja nasi na Mungu. Tunapoasi dhidi ya utawala wa Mungu katika maisha yetu, tunaasi dhidi ya Uzima, na hivyo tunakumbana na mauti (kuvunjika kunaosababisha maumivu). Tunapomrudia Mungu, tunarudishwa tena kwenye ushirika wa kiroho na Mungu, hisia za lengo, haki, uhuru, nk. Baba mwenye furaha katika mfano wa Mwana mpotevu alisema vizuri zaidi: "Huyu mtoto wangu alikuwa amekufa na yu hai tena "(Luka 15:24).

CHAKULA CHA WATOTO

 

CHAKULA CHA WATOTO

 

            Tunaendelea kujifunza Biblia katika sura ya 15 ya kitabu cha MATHAYO. Ingawa kichwa cha somo letu ni “CHAKULA CHA WATOTO“, hata hivyo tuna mengi zaidi ya kujifunza. Tutaliangalia somo letu la leo katika vipengele vitatu:-

(1) ALAMA ZA MAFARISAYO;

(2) MPANGO WA MUNGU WA WOKOVU;

(3) CHAKULA CHA WATOTO.

 

(1) ALAMA ZA MAFARISAYO

Katika sura ya 15 pekee ya kitabu hiki cha Mathayo, “Mafarisayo” wanatajwa katika MST. 1 & 12. Katika sura zilizotangulia pia tumeona Yesu akitaja sana habari za “Mafarisayo”. Katika MATHAYO 16:11-12, Yesu anatuonya kujilinda na mafundisho ya Mafarisayo. Sasa basi, tutawezaje kuwafahamu Mafarisayo na mafundisho yao? Tutawafahamu kwa alama zifuatazo:-

1. HULITANGUA NENO LA MUNGU NA KUYASHIKA MAFUNDISHO YALIYO MAAGIZO YA WANADAMU (MATHAYO 15:6-9; MARKO 7:13; YOHANA 17:17);

2. HUMHESHIMU MUNGU KWA MIDOMO TU ILA MIOYO YAO IKO MBALI NAYE (MATHAYO 15:8-9; TITO 1:16; YOHANA 4:23-25);

3. KAZI YAO NI KUTAFUTA MAKOSA (MATHAYO 15:2; 12:1-2; LUKA 14:1-3; MITHALI 28:9);

4. HUJIFANYA WANAFUATA MAAGIZO YA MUSA HUKU WAKIMKANA (MARKO 7:10-12; TITO 3:4-8; 1 WAKORINTHO 10:14) – Musa aliandika habari za Yesu (YOHANA 1:45; 5:46). Musa alisema kwamba watu wamsikie Yesu atakapokuja kwao na kwamba mtu yeyote ambaye hatasikia neno la Yesu, Mungu atalitaka kwake (KUMBUKUMBU LA TORATI 18:15, 18-19; linganisha na YOHANA 12:48; MATHAYO 17:1-5);

5. HUTAWADHA KWA NJE TU NA KUACHA MIOYO YAO MICHAFU (MARKO 7:4; MATHAYO 23:25-28).

 

 

 

(2) MPANGO WA MUNGU WA WOKOVU (MATHAYO 15:21-24)

“Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli”, haimaanishi kwamba Yesu hakuja kwa ajili ya wengine wasio Waisraeli. Katika mpango wowote unaopangwa, yeye anayeupanga ana haki kuamua kwamba ataanzia wapi katika kuutekeleza na anaweza kuweka awamu mbalimbali za utekelezaji wa mpango huo. Katika Mpango wa Mungu wa wokovu, awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mpango huo ilikuwa kuleta wokovu (unaojumuisha uponyaji) kwanza kwa Waisraeli (YOHANA 1:11; MATHAYO 10:6). Awamu ya pili ilikuwa kuwapa ulimwengu wote uliosalia wokovu (MATHAYO 21:423; YOHANA 10:16; 11:49-52; WARUMI 1:16; 9:24-30; MATENDO 15:13-18; WAEFESO 3:1-11).

 

 

 

(3) CHAKULA CHA WATOTO (MATHAYO 15:21-28)

Watu wasio Waisraeli yaani Mataifa, walipewa jina “MBWA” na Waisraeli. Yesu Kristo alilitumia jina hili kwa sababu ulikuwa usemi wa kawaida ulioeleweka na kutumiwa na kila mtu Nyakati za Biblia (1 SAMWELI 17:43; 2 SAMWELI 3:8, 9:8). Jina “MBWA” halikuwa tusi ila lilieleza hali halisi iliyokuwapo. Mbwa hawakuwa wakitunzwa kwa kutengenezewa chakula kizuri na wale waliowafuga ila walitupiwa makombo tu. Hawakuruhusiwa kama ilivyo leo kukaa ndani ya nyumba kuwa karibu sana na wanadamu. Mataifa waliitwa “mbwa” kwa jinsi ambavyo hawakuwa na “haki ya ndani” walizokuwa nazo Waisraeli. Mungu alihesabiwa kukaa katika nyumba ya Waisraeli peke yao. Hao tu ndio waliokuwa watoto wake (1 WAFALME 8:13). Baba anawajibika kuwapa kwanza watoto wake chakula. Ingawa anaweza kumpa chakula mtoto wa wengine hata hivyo kizuri kitakuwa cha watoto wake kwanza.

Watu tuliookoka ni watoto wa Mungu (YOHANA 1:12). Kutokana na kuwa watoto, chakula cha uponyaji, kufunguliwa kutokana na nguvu za giza n.k.; vyote hivi ni HAKI YA WATOTO KATIKA FAMILIA YA MUNGU. Kama hapa mbwa alipewa makombo basi sisi watoto tutapewa uzima tena uzima tele. (MATHAYO 7:7-11; MARKO 9:23; ZABURI 103:13; ISAYA 49:14-16).

barikiwa. Kwasababu hii share ujumbe huu kwa kubonyeza neno“ share” lililopo chini ya “note” hii, kwa kufanya hivyo ujumbe huu utafika kwa watu wengi. Hakika, Baraka za Mungu zitakuwa nawe.. ( FULL GOSPEL)

No comments: