JE, KUCHEZA AU KUSHABIKIA MPIRA NI DHAMBI? JE, KUCHEZA AU KUSHABIKIA MPIRA NI DHAMBI?
MECHI
Je, wewe ni mchezaji
wa mpira au ni mshabiki tu? Kama jibu ni ndiyo somo hili ni muhimu sana kwako.
Hata kama wewe siyo mchezaji au mshabiki wa mpira, somo hili ni muhimu kwako
kwani limejaa maarifa mengi ya kukujenga kiroho.
Wako watu
wengne ambao kwa kutokuelewa wanataka kila neno ambalo ni dhambi walione
limeandikwa hivyo hivyo kama linavyotamkwa katika biblia zetu kwa mfano sigara
au hii habari ya mipira ya ligi.biblia imeandikwa ili ipate kueleweka kwa
vizazi vyote tangu kipindi cha uumbaji au kipindi chote hiki cha miaka elfu
elfu ilyopita.mfano redio, tv, magari ndege tulizonazo leo hayakuwepo nyakati
zao za nyuma.lakin neno moja tu linatolewa kuwa MAARIFA YATAONGEZEKA [DAN
12:4]. Linatoa picha kutakuwa na mambo gani yatakayotokea leo ,lazima tuelewe
biblia haijaandika neno moja, kuna maneno kadha wa kadha ambayo hayajaandikwa
kwa sababu hayakuwepo katika vizazi vingine vilivyotangulia, na hivyo watu wa
vizazi hivyo wasingeweza kuyaelewa kwa namna tunavyoweza kuyaelewa leo. ndiyo
mana MUNGU katika kuleta neno lake, alilileta ili lipate kuwa ni neno
linaloweza kuvifaa vizazi vyote kwa wakat wowote.
kwa
sababu hiyo tunaweza tukawa tunataka kufahamu ni nini mapenzi ya MUNGU katika
jambo fulani na tukilitafuta kama lilivyo katika biblia, tutapata shinda
kuliona,mengi hatutaweza kuyaona kwa sababu hayakuwepo kama yalivyo nyakati
nyingine za biblia. mfano jambo la mchezo wa mpira wa miguu au soka ambao
unaendesha mamilion ya watu leo.sasa mtu atajiuliza tukiwa tumeokolewa tunaweza
tukawa mashabiki wa mipira au kucheza mipira hiyo.Na mtu anaweza kujiona salama
kwa kusema hakuna mahali tulipokatazwa ktk biblia.
Hik
tunachokiita mchezo wa mpira si kitu cha zamani kama wengine wanavyofikiria.ebu
tuangalie historia fupi ya mchezo huu ndipo nitakueleza kwa nini mpira ni
dhambi. Huko zamani kile walichokuwa wanakiita mpira hakikuwa hvyo kwa sheria
tulizo nazo kwa namna ya sasa.kitu hichi kinachoitwa mpira kilianza mwaka 1863
mwezi 10,walikuwepo watu kadhaa waliotoka katika shule kadhaa uingereza na club
chache zilizokuwapo hapo,wakawa wamewakilisha vikundi11 na ndio wakakusanyika
mwezi 10,1863 na kuanza kutunga sheria za kupatana za mchezo
Hawa
ndio waliosababisha kiundwe chama cha mpira ambacho kinaitwa FA (FOOTBALL
ASSOCIATION) cha England mwaka huu 1863 ambao ni mwaka wa karibun sana (miaka
149 iliyopita).lakini mwaka 1869 ndipo katika sheria hizo walizounda wakazidi
kuziboresha kuwa katika mpira huo hautakiwi kushika mpira kwa mkono na kuubeba,
itakuwa faulo.ndio wakatenganisha mchezo huu wa ragbi na football mwaka 1871
ndipo mashindano ya kwanza ya mpira yalipoanzishwa ya kombe la FA CUP.mwak 1888
ndipo mashindano ya kwanza ya ligi ya mpira yalipoanzishwa30-12-1872 ndipo mech
ya kwanza ya mpira ya kimataifa ilipochezwa kati ya england na scotland. Chama
cha mpira cha dunia(FIFA) kilianzishwa mwak 1904,waanzilish zilikuw nchi saba
ufaransa,ubelgiji,dernmark,netheland,spain,sweeden na swizland. mwaka 1930
ndipo kwa mara kwanza kombe la dunia lilipoanzishwa.
Kwa hiyo mpira huu ni kitu cha majuzi sana kuliko wengi
tunavyofahamu.kama ingeandikwa habari za mipira ya ligi, soccer miaka hiyo ya
nyuma watu wasingeelewa kwa namna ambavyo sisi tunavyoelewa.
Sasa
tunajuaje je wakristo au watu tuliookoka, je tunaweza kushiriki mipira kama hii
na club kam hizi.ili kuweza kujua vitu kama hivi, tunatakiwa tuangalie
kanuni.MUNGU ameweka kanuni ambazo zinatuongoza kupata ufahamu mapenzi ya MUNGU
kwa kila jambo.
Pale
ambapo jambo halijatajwa moja kwa moja, kanuni hizi zinaweza zikatuongoza.sasa
tutakwenda kuangalia kanuni kadha wa kadha ambazo zitakuwa zinahusisha mambo
mengi sana ambayo yanaweza kujitokeza katika nyakati mbalimbali katika vizazi
tofauti. Sasa tunajuaje je wakristo au watu tuliookoka, je tunaweza kushiriki
mipira kama hii na club kama hizi. ili kuweza kujua vitu kama hivi, tunatakiwa
tuangalie kanuni. MUNGU ameweka kanuni ambazo zinatuongoza kupata ufahamu
mapenzi ya MUNGU kwa kila jambo. pale ambapo jambo halijatajwa moja kwa moja,
kanuni hizi zinaweza zikatuongoza. sasa tutakwenda kuangalia kanuni kadha wa
kadha ambazo zitakuwa zinahusisha mambo mengi sana ambayo yanaweza kujitokeza
katika nyakati mbalimbali katika vizazi tofauti.
Yako maandiko kadha wa kadha ambayo yanaweza kutuongoza
katika kujua mapenzi ya MUNGU katika mipira hii.
1) (WAKOLOSAI
3:17) “KILA MFANYALO KWA NENO AU KWA TENDO, FANYENI LOTE KWA JINA LA BWANA YESU
NA KUMSHUKURU MUNGU BABA“Ni muhimu kuelewa ndani yetu tuliokoka kuna mafuta au
tuna dhamiri ambayo inatufundisha kujua mema na mabaya (1PET2:26-27).Hata kama
jambo hatujajifunza kwa undani juu ya jambo fulani,ndani yetu kutakuwepo roho
mtakatifu akitufundisha kuwa hapa siyo na hapa ndiyo.
Sasa kila tunalolifanya kwa neno au kwa tendo, anasema
tulifanye hayo yote kwa kufungua kwa maombi.sasa kutokan na mafuta ndani yetu
JE TUNAWEZA KUFUNGUA MECHI YA MPIRA KWA KUSHUKURU BABA KWA MAOMBI? Utaona ndani
yetu inakataa.
2.) (YOHANA
5:19) “MWANA HAWEZI KUTENDA NENO MWENYEWE ISIPOKUWA AMEMUONA BABA ANALITENDA”.
(YOH 14:6-9) Hivyo hatuna budi kujiuliza kutokana na maisha ya YESU, JE
INAWEZEKANA YESU AKAWA ANACHEZA MPIRA? YESU KASHIKA MPIRA, MARA BEKi FULANI
KAMKATA MTAMA AU TIMU YA YESU IMEPIGWA MAGOLI 6-0? kama dhamiri inakataa kuwa
YESU hawezi kufanya hvyo na sisi hatuwezi kufanya hvyo.Tunatenda neno ambalo
YESU anaweza kulitenda.
3) Mashabiki
wengi wa jambo hilo,vinara wa jambo hilo ,JE NI MATAIFA?Kama wanaongoza ni
mataifa,basi nyuma ya jambo hilo kuna mashetani (UFUNUO 18:2-3,23). Mataifa
yote yanapokuwa wanachukuliwa hivyo katika jambo hilo, ndio vinara, mashabiki,
kwa namna hiyo hiyo uchawi unavyotajwa lazima tujue kuna roho za
mashetani.ukiona vinara au viongozi ndio waasherati au walevi,wavuta bangi.
Hawa wanaotajwa washauri wa mambo ya kifundi katika timu
hizo ndio wachawi wa timu.
4) Sitatiwa
chini ya uwezo wa kitu chochote (1WAKORINTHO 6:12).Shetan anaitwa mfalme wa
uwezo wa anga (EFESO 2:1-2). Chochote kile ambacho nyuma yake kuna mashetani
kinamuweka mtu au watu chini ya uwezo fulani na hawezi kujikwamua pale, atakuwa
anakitumikia kile kitu na hawezi kujinasua.unaweza kuona mtu anaweza kuwa na
uchungu wa kuona timu yake imefungwa hata kushindwa kula lakini hana uchungu
kufunga ili kuona watu wanaokoka, mtu anaweza kukaa masaa mengi kuangalia na
kusiliza hizo mechi zake lakini mtu huyu huyu ni shida kuchukua masaa mengi
kusoma biblia, hata kwenye ibada akiona mchungaji anahubiri muda mrefu, anatamani
akatishe au anasinzia ibadani.saa nyingine anaweza kugairi kuja kwenye ibada
kama ikiwa ratiba hiyo imeingiliana na mechi yake.kwa ujumla mtu halifurahii
neno kama anavyoushabikia mpira.ndio mana ni rahisi kujiua kwa ajil ya mpira
kuliko kwa ajili ya YESU.MTU ATAKITAMANi KUACHA INAKUWA SHIDA, UJUE AMETIWA
CHINI YA UWEZO WA MPIRA NA SHETANi.
Miongoni mwa mambo ambayo shetani amefanikiwa kuchukua watu
wengi ni katika mipira, hata walokole nao wanatetea kwa nguvu zote. Ndio
unasikia kanisa fulani ina timu ya mpira inaitwa haleluya football club.ndio
maana makanisa ya leo yameishiwa ngvu za MUNGU si kama kanisa la
kwanza,watumishi wa leo wanalazimisha kuangusha watu chini na kukumbatia wake
za watu kwa kigezo ndo wanaachilia upako.shame upon them.ni kwa sababu
lnachanganya mambo ya kdunia na kuyaingiza kanisani.
Sasa
nimependa kuanza hivyo ili tupate kujua kuwa sisi tuliookolewa hatuna chetu /
hatuna sehemu katika kushiriki michezo ya dunia hii. kushindana kwetu ni juu ya
kuishindania imani tuliyokabidhiwa mara moja tu. watakatifu wa kanisa la kwanza
walilijua vema jambo hili na kutokana na jinsi walivyokuwa wakamilifu
hawakushiriki katika michezo na walichukiwa na jamii iliyowazunguka kwasababu
walionekana “washamba” haya ni maelezo kuhusu watakatifu wa kanisa la kwanza”
The Christians were charged with being unsocial and came to be hated and
counted as enemies of societies, they were simple and modest in dress, strictly
moral in their conduct and would not go to the games and feast “maneno haya
yanapatikana katika biblia iitwayo THOMPSON CHAIN REFERENCE BIBLE(NIV)” ambayo
mwisho kwenye kurasa za mwisho inatoa dondoo(notes) ya baadhi ya matukio ya
kanisa la kwanza na kabla yake. sasa ikwa sisi tutanana nao wanaoshabikia
mipira na michezo mingineyo tofauti yetu na wao ni ipi? tujifunze kwa ndugu
zetu walio tutangulia, tuige imani yao maana ikiwa tufanana na watu wa
ulimwengu na sisi tukaanza kuenenda kama ulimwengu unavyoenenda tukaishi kana
kwamba sisi ni wenyeji hapa duniani basi tunaitwa wazinzi kwa kuwa tutakuwa na
mabwana wawili mungu wa dunia hii, shetani (2WAKORINTHO 4:3-4) na MUNGU muumba
wa mbingu na nchi; (YAKOBO 4:4) Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa
dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya
kuwa adui wa Mungu” BAADHI YA MASOMO YAPO CHINI BOFYA SOMO UINGIE UJIFUNZE; FULL GOSPEL
No comments:
Post a Comment