Ina maana gani kwamba mshahara wa dhambi ni mauti?

Warumi 6:23 inasema, "Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu." Katika msingi wake, dhambi ni uasi dhidi ya Mungu. Dhambi zetu hututenganisha na Mungu, Muumba na mwenye uzima. Yesu alisema, "Mimi ndimi njia na kweli na uzima" (Yohana 14: 6). Mungu anajulikana kama "MIMI NDIMI" mkuu. Uzima uu katika Mungu. Kwa hivyo, tunapofanya dhambi na kujitenganisha na Mungu, tunatengana na uzima wa kweli. Kwa hivyo, bila shaka, tunakumbana na mauti. Hoja tatu za ufafanuzi zinahitajika: Kwanza, dhambi hasa haisababishi kifo cha kimwili mara moja. Warumi 6 haituambii kwamba tunapofanya dhambi tutakufa kimwili. Badala yake, inarejelea kifo cha kiroho. Pili, wakati tunapookoka katika Kristo, tunaokolewa kutokana na hatima ya kifo cha kiroho na kuletwa katika hatima ya uzima wa kiroho. Paulo aliwaambia Warumi, "Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu" (Warumi 6:23). Tatu, hata dhambi za waumini bila shaka zitasababisha aina ya "kifo" cha kiroho. Ingawa tumeokolewa kutokana na adhabu ya mwisho ya dhambi (kutengwa kwa milele na Mungu), hatuokolewa kutokana na matokeo ya asili ya uhusiano uliovunjika na Baba . Tunapofanya dhambi, tunapata dalili za kifo cha kiroho. Tunaweza kujihisi kuwa na hatia, kuwa wapungufu, kuchanganyikiwa, au kutokuwa na uhusiano na Mungu. Sisi hufanya kama waadilifu badala ya kuwa wenye haki. Dhambi zetu, hata kama waumini, huumiza moyo wa Mungu na uhuzunisha Roho Wake (Waefeso 4:30). Ingawa dhambi zetu haziachi uhusiano wetu na Yeye, huweka kizuizi kati yetu. Fikiria mtoto na mzazi. Wakati mtoto anapoasi, uhusiano na mzazi wake unafadhaika. Mzazi bado anampenda mtoto na bado ana nia bora kwa mtoto moyoni. Mtoto kamwe aachi kuwa bila mzazi. Hata hivyo, mtoto anaweza kupata matokeo fulani: kutoaminiwa, nidhamu, hisia ya hatia, na kadhalika. Bila shaka hatimaye uhusiano hurejeshwa ila kawaida pigo huja kwanza. Hivyo ni pamoja nasi na Mungu. Tunapoasi dhidi ya utawala wa Mungu katika maisha yetu, tunaasi dhidi ya Uzima, na hivyo tunakumbana na mauti (kuvunjika kunaosababisha maumivu). Tunapomrudia Mungu, tunarudishwa tena kwenye ushirika wa kiroho na Mungu, hisia za lengo, haki, uhuru, nk. Baba mwenye furaha katika mfano wa Mwana mpotevu alisema vizuri zaidi: "Huyu mtoto wangu alikuwa amekufa na yu hai tena "(Luka 15:24).

JEHANUM YA MOTO

 

 JEHANUM YA MOTO

 

Yesu Kristo anatufundisha waziwazi kuhusu Jehanum ya moto, akituonya kumwogopa Mungu mwenye uwezo wa kututupa Jehanum. Anaendelea kutuonya kwamba, ni heri kukubali lolote lile litupate kuliko kwenda kwenye mateso makali ya Jehanum (LUKA 12:5, MATHAYO 5:22, 29-30). Maandiko pia yanaendelea kusisitiza kwa msisitizo mkubwa kwamba, ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai na kutupwa katika Jehanum ya moto (WAEBRANIA 10:26-27, 31). Jehanum hii ya moto inaitwa pia kuzimu (ZABURI 9:17) na tena inaitwa Tofeni (ISAYA 30:33). Hatupaswi kulipuuza jambo hili na kulifanya juu juu tu. Kwa sababu hii, leo, tutajifunza kwa undani kuhusu Jehanum ya moto, na tutaligawa somo letu katika vipengele vinne:-

 

(1)    HUKUMU BAADA TU YA KUFA

 

(2)    JEHANUM YA MOTO IKO WAP?

 

(3)    HALI HALISI YA JEHANUM NA WALE WALIOKO HUKO

 

(4)    JINSI YA KUIKWEPA JEHANUM YA MOTO

 

( 1 ). HUKUMU BAADA YA KUFA

 

Biblia inaeleza waziwazi kwamba mtu anapokufa, sekunde ileile ya kufa kwake anakabiliwa na hukumu (WAEBRANIA 9:27). Watu wanaofundisha kinyume na kweli ya neno, hufundisha kwamba mtu anapokufa analala tu na hakuna lolote la hukumu ya mara moja. Wanatumia maandiko yanayozungumzia kulala kwa kuyatafsiri isivyo (MATHAYO 27:52; 1 WAKORINTHO 15:20; YOHANA 11:11-14 n.k ) na pia wanasema wafu hawajui lolote kwa kutumia maandiko kama MHUBIRI 9:5. Ilivyo ni kwamba kinachobaki kaburini ni mwili tu. Nafsi na roho ya mtu  huondoka kwa kuvalishwa mwili mwingine ( 1WAKORINTHO 15:40 ). Mwili unaobaki kaburini ndiyo ambao umelala haujui lolote na hauna kumbukumbu, lakini pasipo mwili huo mtu atamwona Mungu ikiwa ameishi katika mapenzi yake (AYUBU 19:26). Mwili hubaki kaburini, lakini roho ya mtu huondoka (MHUBIRI 12:7). Ikiwa mtu ameishi katika mapenzi ya Mungu mara tu ya kufa huchukuliwa mbinguni na malaika kwa kutumia magari maalum ya mbinguni (LUKA 23:43; 16:22;  2WAFALME 2:11-12; ZABURI 68:17; WAEBRANIA 1:7, 14). Ikiwa ameishi katika dhambi hukumu yake huwa kutupwa katika Jehanum ya moto mara tu baada ya kufa (MITHALI 9:13-18; ISAYA 5:11-15; MITHALI 17:24-27).

 

( 2 ). JEHANUM YA MMOTO IKO WAPI?

 

Mtu anapokufa tu, huwa kwenye njia panda. Kila mmoja hupenda kwenda mbinguni, hata hivo ikiwa jina lake haliko katika kitabu cha uzima cha mbinguni, hulazimika kwenda Jehanum ya moto. Mtu anayetakiwa kwenda motoni huchachamaa na kukataa kwenda kwenye njia mbaya inayotisha ya motoni na hulazimika kukamatwa na kutupwa Jehanum (UFUNUO 19:20; 20:10). Mbinguni ni juu (mbingu ya tatu) lakini kuzimu au Jehanum ya moto ni chini (pande za chini za nchi) 2WAKORINTHO 12:1-4; ITHALI 15:24; ZABURI 63:9;  EZEKIELI 31:14.

 

( 3 ). HALI HALISI YA JEHANUM NA WALE WALIOKO HUKO

 

Jehanum ya moto ni kuzimu au shimo kubwa na refu sana lililojaa moto. Moto huu huwashwa mfululizo kwa pumzi ya Bwana (ISAYA 14:15; 30:33). Moto ni mkali kuliko moto wowote tunaoufahamu duniani, uwe gesi, umeme, makaa yam awe au lolote jingine (WAEBRANIA 10:27). Moto huu ni mweusi unaosababisha giza na kufanya mtu awaone wenzake wachache tu wa karibu naye (MATHAYO 11-12; 22:13; 25:30 YUDA 1:6). Moto huu una uwezo wa kula na kutafuna, kwa hiyo huwatafuna au kuwala wale walioko motoni (KUMBUKUMBU LA TORATI 32:22; WAEBRANIA 10:36-27). Hata hivyo, kama jinsi ambavyo chumvi inavyozuia nyama kuharibika, moto humtafuna mtu lakini hamaliziki (MARKO 9:43-49). Ni moto wa milele (MATAYO 25:41). Mafundisho potofu ysnswafariji watu na kusema eti mtu ataunguzwa na moto na kutoweshwa au kupotea na kuangamia  kabisa na ndiyo mwisho wake. Wanatumia maandiko kama MATHAYO 10:28 ( kuangamizwa ) na YOHANA 3:16 ( kupotea ). Kuangamia hakumaanishi kualizika kabisa (ESTA 4:16). Kondoo akipotea haimaanishi hayupo kabisa ila ametengwa na mchungaji (angalia ISAYA 57:1-3). Vilevile neno “kuharibu” linapotumika kuhusiana na adhabu ya milele halina maana ya kufanya kitu kisiwepo, bali ni la kuzdhibu vikali ( 1WAKORINTHO 3:16-17 ). Waalimu hawa wa uongo hufundisha pia kwamba ati watu watatoweshwa kama moshi baada kwa kuunguzwa kwa kutumia ZABURI 37:20. Kutoweshwa hapa ni kutenganishwa mbali na Mungu. Moto wa milele, huambatana na madini yanayoitwa kiberiti (lugha ya kitaalam, “sulphur”). Madini haya yakiwaka huwa kama mpira na hutoa harufu kama ya mayai yaliyooza. Harufu ya namna hii inafunika kuzimu yote. Siyo hayo tu, katika moto huu wamo funza maalum ambao huwatafuna watu na kufanya matundu mengi katika miili yao wakiingia na kutoka. Hii hufanya sura zao kuwa mbaya mno kama madude tu! (ISAYA 14:11; MARKO 9:43-49; ISAYA 66:24). Jehanum ya moto, huitwa pia mauti ya pili (UFUNUO 21:8). Uchungu wa mauti unaompata mtu anapokufa, huwa juu ya mtu motoni, milele na milele (UFUNUO 20:10). Watu walioko motoni hujawa wakati wote na vilio na tena husaga meno yao kama mtu anayeona baridi kali MATHAYO 8:12). Kuzimu, urikalo ni pigo lif urikalo ambalo huwachukua wenye dhambi asubuhi, mchana na usiku (ISAYA 28:15, 18-19). Walioko motoni wanajifahamu, na kuwakumbuka wenzao waliowaacha duniani na tena hutoa ndimi zao nje wakitamani maji kidogo kupoza ulimi (LUKA 16:19-24). Juu ya yote hayo, katika vilio vyao, humwomba Mungu awahurumie na kuwasamehe lakini Yeye amekwishasema, “Nami jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma” (EZEKIELI9:10;8:18).

 

USEMI NA FIKRA ZA WALE WALIOKO MOTONI

 

Watu walioko motoni hutamani mtu mmoja kati yao aje awashuhudie ndugu zao ili wayoache dhambi na kukwepa mateso yao (LUKA 16:27-31). Wale walioko huko wajiopata mafundisho haya kabla, husema, “Jinsi nilivyochukia maonyo, na  na moyo wangu ukadharau kukemewa; wala sikuisikia sauti ya waalimu wangu, wala sikuwategea sikio langu walionifundisha (MITHALI 5:11-13)” Wakimwona yeyote anayejiunga nao, humwambia, “Jew ewe umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe ummekuwa kama sisi!”  ( ISAYA 14:9-10).

 

WALIO MBINGUNI HUPEWA NAFASI YA KUWACHUNGULIA

 

Walioko mbinguni watatoka kidogo kuwaangalia (ISAYA 66:24) ila hawatakuwa na  machozi yoyote juu yao.

 

TOFAUTI KATI YA JEHANUM YA MOTO NA ZIWA LA MOTO

 

Jehanum ya moto ni tofauti na ziwa la moto linalotajwa katika UFUNUO 20:14-15; 21:8 kwa jinsi ileile mbingu ya sasa ilivyo tofauti na mbingu mpya inayotajwa katika UFUNUO 21:1. Ziwa la moto kwa sasa halina mkazi ndani yake. Watakaokuwa wa kwanza kuingia humo watakuwa mnyama (Mpinga Kristo) na nabii wa uongo (UFUNUO 19:20). Kisha atafuata ibilisi ambaye atatupwa humo baada ya vita ya Gogu na Magogu (UFUNUO 20:7-10). Baada ya hapo kutafuata hukumu ya jiti cha enzi, kikubwa cheupe. Hukumu hii itatolewa baada ya ufufuo wa pili au ufufuo wa hukumu ambao utawafufua walioko Jehanum ya moto.Baada ya hawa kuelezwa kwa nini wamehukumiwa adhabu ya matesoya milele, ndipo watakapotupwa katika ziwa la moto. Mateso yaliyoko ziwa la moto ni zaidi sana kuliko mateso ya Jehanum ya moto. Ni kama Jehanum walikuwa mahabusu na sasa wanapelekwa gerezani. Kama mbingu mpya itakavyokuwa nzuri zaidi kuliko mbingu ya sasa, vivyo ziwa la moto litakuwa na mateso yaliyokithiri kuliko Jehanum ya moto.

 

( 4 ). JINSI YA KUIKWEPA JEHANUM YA MOTO

 

1 .Kuungama dhambi na kuziacha (MITHALI 28:13).

 

2. Kulishika Neno la Mungu kwa kufanya maagizo yote ya Mungu na kuwakata wafariji    wenye kutaabisha wanaosema kufanya hili na lile siyo lazima  ( YOHANA 8:51; ZABURI 119:6; AYUBU 16:1-2 ).

 

3. Kutohesabu sheria kuwa kutu kigeni. Kukubali kuongozwa na sheria ya Kristo. Hakuna mwanafunzi asiyeishi kwa sheria  ( HOSEA 8:12; WAGALATIA 6:2; ISAYA 8:16 ).

 

4. Kuwa mtakatifu na kutoifuatisha namna ya dunia hii katika mavazi, usemi, matendo n.k. ( WAEBRANIA 12:14;  WARUMI 12:2; YAKOBO 4:4; 1YOHANA 2:15-17 )

 

JE! WEWE NAWE UMEKUWA DHAIFU KAMA SISI!

 

ISAYA 14:9-10

 

No comments: