Ina maana gani kwamba mshahara wa dhambi ni mauti?

Warumi 6:23 inasema, "Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu." Katika msingi wake, dhambi ni uasi dhidi ya Mungu. Dhambi zetu hututenganisha na Mungu, Muumba na mwenye uzima. Yesu alisema, "Mimi ndimi njia na kweli na uzima" (Yohana 14: 6). Mungu anajulikana kama "MIMI NDIMI" mkuu. Uzima uu katika Mungu. Kwa hivyo, tunapofanya dhambi na kujitenganisha na Mungu, tunatengana na uzima wa kweli. Kwa hivyo, bila shaka, tunakumbana na mauti. Hoja tatu za ufafanuzi zinahitajika: Kwanza, dhambi hasa haisababishi kifo cha kimwili mara moja. Warumi 6 haituambii kwamba tunapofanya dhambi tutakufa kimwili. Badala yake, inarejelea kifo cha kiroho. Pili, wakati tunapookoka katika Kristo, tunaokolewa kutokana na hatima ya kifo cha kiroho na kuletwa katika hatima ya uzima wa kiroho. Paulo aliwaambia Warumi, "Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu" (Warumi 6:23). Tatu, hata dhambi za waumini bila shaka zitasababisha aina ya "kifo" cha kiroho. Ingawa tumeokolewa kutokana na adhabu ya mwisho ya dhambi (kutengwa kwa milele na Mungu), hatuokolewa kutokana na matokeo ya asili ya uhusiano uliovunjika na Baba . Tunapofanya dhambi, tunapata dalili za kifo cha kiroho. Tunaweza kujihisi kuwa na hatia, kuwa wapungufu, kuchanganyikiwa, au kutokuwa na uhusiano na Mungu. Sisi hufanya kama waadilifu badala ya kuwa wenye haki. Dhambi zetu, hata kama waumini, huumiza moyo wa Mungu na uhuzunisha Roho Wake (Waefeso 4:30). Ingawa dhambi zetu haziachi uhusiano wetu na Yeye, huweka kizuizi kati yetu. Fikiria mtoto na mzazi. Wakati mtoto anapoasi, uhusiano na mzazi wake unafadhaika. Mzazi bado anampenda mtoto na bado ana nia bora kwa mtoto moyoni. Mtoto kamwe aachi kuwa bila mzazi. Hata hivyo, mtoto anaweza kupata matokeo fulani: kutoaminiwa, nidhamu, hisia ya hatia, na kadhalika. Bila shaka hatimaye uhusiano hurejeshwa ila kawaida pigo huja kwanza. Hivyo ni pamoja nasi na Mungu. Tunapoasi dhidi ya utawala wa Mungu katika maisha yetu, tunaasi dhidi ya Uzima, na hivyo tunakumbana na mauti (kuvunjika kunaosababisha maumivu). Tunapomrudia Mungu, tunarudishwa tena kwenye ushirika wa kiroho na Mungu, hisia za lengo, haki, uhuru, nk. Baba mwenye furaha katika mfano wa Mwana mpotevu alisema vizuri zaidi: "Huyu mtoto wangu alikuwa amekufa na yu hai tena "(Luka 15:24).

DHAMBI YA MAWAZO MABAYA (MATHAYO 15:19-20)

 

 DHAMBI YA MAWAZO MABAYA (MATHAYO 15:19-20)

 

Mawazo mabaya ni dhambi ya mauti kama dhambi nyinginezo ambazo zitamfanya mtu akose uzima wa milele. Katika somo letu la leo tutaangalia kwa mapana, urefu na kina juu ya dhambi hii ambayo wengi wetu wanafahamu juu yake kwa juu juu tu. Tutaligawa somo letu katika vipengele viwili:-

(1) DHAMBI YA MAWAZO MABAYA NI NINI?

(2) JINSI YA KUISHINDA DHAMBI HII.

 

(1) DHAMBI YA MAWAZO MABAYA NI NINI?

Ukifanya lolote kati ya mambo 25 yafuatayo, ujue unafanya dhambi ya mawazo mabaya:-

1. Kutunga maovu – ZABURI 64:5-6;

2. Kumwonea wivu mtu kwa sababu ya mafanikio yake ya kimwili au kiroho – MWANZO 37:9-11;

3. Kumchukia mtu na kuacha kusema naye kwa amani – MWANZO 37:4;

4. Kukusudia mabaya – MWANZO 50:20; NEHEMIA 6:2; EZEKIELI 38:10-12;

5. Kuwa na wazo la kukwepa wajibu – KUMBUKUMBU LA TORATI 15:9;

6. Kufanya maamuzi bila taarifa za uhakika – WAAMUZI 15:1-2;

7. Kupanga kuua, kuiba au kufanya uzinzi au uasherati – WAAMUZI 20:5; 2 SAMWELI 13:6-11;

8. Kusema jambo la kukisia kana kwamba una uhakika nalo – 1 SAMWELI 1:12-13;

9. Kuwaza mawazo ya tamaa mbaya – 2 NYAKATI 32:1;

10. Mawazo ya majivuno – kujiona wewe ni zaidi ya wengine na kwamba unastahili heshima zaidi kuliko wengine – ESTA 6:6;

11. Kuwaza kwamba hakuna Mungu – ZABURI 10:14;

12. Kujiinua juu ya elimu ya Mungu – 2 WAKORINTHO 10:5;

13. Kutumainia mali na kufikiri kufa ni kwa maskini – ZABURI 49:6-12;

14. Kuwaza kufanya au kusema jambo la kukufanya uonekane mtundu au tofauti na wengine – MITHALI 24:8-9;

15. Kuwasema vibaya viongozi mawazoni – MHUBIRI 10:20;

16. Kuwa na wasiwasi juu ya maisha ya baadaye – LUKA 12:29;

17. Kumlaumu mtu au kumshitaki kutokana na taarifa usizokuwa na uhakika nazo, au za uongo – MATHAYO 9:2-4; MATHAYO 12:22-27;

18. Kumvizia mtu kwa kutafuta kosa lake – LUKA 6:6-11;

19. Kuwa na mawazo ya kutaka ukubwa – LUKA 9:46-48;

20. Kutaka Karama za Roho Mtakatifu ili watu wakuone wewe ni zaidi au kwa kuona utanufaika – MATENDO 8:18-19;

21. Kujiona wewe umesoma, au una mali na kutaka ufanyiwe jambo kutokana na kisomo au utajiri wako – 1 WAKORINTHO 3:18-20;

22. Kujihesabia haki kutokana na matendo yako – LUKA 18:9-12;

23. Kuwa na mawazo ya ubaguzi au upendeleo – YAKOBO 2:1-4;

24. Kuona shaka moyoni na kuwa na fadhaiko linalotokana na kukosa imani – LUKA 24:36-38;

25. Kuwa na mawazo ya kumtamani mwanamke au mwanamume kwa uasherati au uzinzi – MATHAYO 5:28.

(2) JINSI YA KUISHINDA DHAMBI HII

1. Kuwa na hakika kwamba umezaliwa mara ya pili. Huwezi kuishinda dhambi yoyote au kuushinda ulimwengu na mambo yake bila kuzaliwa mara ya pili (YOHANA 3:3; 1 YOHANA 5:4, 18);

2. Kumwomba Mungu akutakase baada ya kuwa umezaliwa mara ya pili ( 1 WATHESALONIKE 5:23-24);

3. Kuendelea kujitakasa kila siku kwa kudumu katika kuomba na kuongozwa na Neno la Mungu ( 1 YOHANA 3:3; YOHANA 15:3; YOHANA 17:17).

barikiwa. Kwasababu hii share ujumbe huu kwa kubonyeza neno“ share” lililopo chini ya “note” hii, kwa kufanya hivyo ujumbe huu utafika kwa watu wengi. Hakika, Baraka za Mungu zitakuwa nawe

No comments: