DHAMBI YA MAWAZO
MABAYA (MATHAYO 15:19-20)
Mawazo mabaya ni dhambi ya mauti kama dhambi nyinginezo
ambazo zitamfanya mtu akose uzima wa milele. Katika somo letu la leo
tutaangalia kwa mapana, urefu na kina juu ya dhambi hii ambayo wengi wetu
wanafahamu juu yake kwa juu juu tu. Tutaligawa somo letu katika vipengele
viwili:-
(1) DHAMBI YA MAWAZO MABAYA NI NINI?
(2) JINSI YA KUISHINDA DHAMBI HII.
(1) DHAMBI YA MAWAZO MABAYA NI NINI?
Ukifanya lolote kati ya mambo 25 yafuatayo, ujue unafanya
dhambi ya mawazo mabaya:-
1. Kutunga maovu – ZABURI 64:5-6;
2. Kumwonea wivu mtu kwa sababu ya mafanikio yake ya kimwili
au kiroho – MWANZO 37:9-11;
3. Kumchukia mtu na kuacha kusema naye kwa amani – MWANZO
37:4;
4. Kukusudia mabaya – MWANZO 50:20; NEHEMIA 6:2; EZEKIELI
38:10-12;
5. Kuwa na wazo la kukwepa wajibu – KUMBUKUMBU LA TORATI
15:9;
6. Kufanya maamuzi bila taarifa za uhakika – WAAMUZI 15:1-2;
7. Kupanga kuua, kuiba au kufanya uzinzi au uasherati –
WAAMUZI 20:5; 2 SAMWELI 13:6-11;
8. Kusema jambo la kukisia kana kwamba una uhakika nalo – 1
SAMWELI 1:12-13;
9. Kuwaza mawazo ya tamaa mbaya – 2 NYAKATI 32:1;
10. Mawazo ya majivuno – kujiona wewe ni zaidi ya wengine na
kwamba unastahili heshima zaidi kuliko wengine – ESTA 6:6;
11. Kuwaza kwamba hakuna Mungu – ZABURI 10:14;
12. Kujiinua juu ya elimu ya Mungu – 2 WAKORINTHO 10:5;
13. Kutumainia mali na kufikiri kufa ni kwa maskini – ZABURI
49:6-12;
14. Kuwaza kufanya au kusema jambo la kukufanya uonekane
mtundu au tofauti na wengine – MITHALI 24:8-9;
15. Kuwasema vibaya viongozi mawazoni – MHUBIRI 10:20;
16. Kuwa na wasiwasi juu ya maisha ya baadaye – LUKA 12:29;
17. Kumlaumu mtu au kumshitaki kutokana na taarifa usizokuwa
na uhakika nazo, au za uongo – MATHAYO 9:2-4; MATHAYO 12:22-27;
18. Kumvizia mtu kwa kutafuta kosa lake – LUKA 6:6-11;
19. Kuwa na mawazo ya kutaka ukubwa – LUKA 9:46-48;
20. Kutaka Karama za Roho Mtakatifu ili watu wakuone wewe ni
zaidi au kwa kuona utanufaika – MATENDO 8:18-19;
21. Kujiona wewe umesoma, au una mali na kutaka ufanyiwe
jambo kutokana na kisomo au utajiri wako – 1 WAKORINTHO 3:18-20;
22. Kujihesabia haki kutokana na matendo yako – LUKA
18:9-12;
23. Kuwa na mawazo ya ubaguzi au upendeleo – YAKOBO 2:1-4;
24. Kuona shaka moyoni na kuwa na fadhaiko linalotokana na
kukosa imani – LUKA 24:36-38;
25. Kuwa na mawazo ya kumtamani mwanamke au mwanamume kwa
uasherati au uzinzi – MATHAYO 5:28.
(2) JINSI YA KUISHINDA DHAMBI HII
1. Kuwa na hakika kwamba umezaliwa mara ya pili. Huwezi
kuishinda dhambi yoyote au kuushinda ulimwengu na mambo yake bila kuzaliwa mara
ya pili (YOHANA 3:3; 1 YOHANA 5:4, 18);
2. Kumwomba Mungu akutakase baada ya kuwa umezaliwa mara ya
pili ( 1 WATHESALONIKE 5:23-24);
3. Kuendelea kujitakasa kila siku kwa kudumu katika kuomba
na kuongozwa na Neno la Mungu ( 1 YOHANA 3:3; YOHANA 15:3; YOHANA 17:17).
barikiwa. Kwasababu hii share ujumbe huu kwa kubonyeza neno“
share” lililopo chini ya “note” hii, kwa kufanya hivyo ujumbe huu utafika kwa
watu wengi. Hakika, Baraka za Mungu zitakuwa nawe
No comments:
Post a Comment