HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI
Leo, tunamaliza kutafakari SURA YA 14 ya Kitabu cha YOHANA
katika Biblia zetu. Tunachukua muda wa
Siku ya leo ya Kuichambua Biblia, kujifunza YOHANA 14:13-31. Katika mistari hii, pamoja na mambo mengine,
tutajifunza kuhusu, “HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI“. Tutayagawa mafundisho yote tunayoyapta katika
mistari hii, katika vipengele tisa:
(1) KUOMBA KWA JINA
LA YESU (MST. 13-14);
(2) HAKIKA YA
KUJIBIWA MAOMBI (MST. 13-14);
(3) ALAMA YA KUMPENDA
YESU (MST. 15, 21, 23-24);
(4) MSAIDIZI MWINGINE
(MST. 16-27, 25-26);
(5) SITAWAACHA NINYI
YATIMA (MST. 18-20);
(6) FAIDA ZA
KUZISHIKA AMRI ZA YESU (MST. 21-23);
(7) MSIWE NA WOGA
(MST. 27-29);
(8) MKUU WA ULIMWENGU
HANA KITU KWA YESU (MST. 30);
(9) JINSI YA
KUUJULISHA ULIMWENGU YA KUWA TUNAMPENDA BABA
(MST.34).
(1)
KUOMBA KWA JINA LA YESU (MST. 13-14)
Yesu Kristo aliye Bwana na Mwalimu wetu, hapa anatufundisha
jinsi ya kuomba, ili maombi yetu yawe na uwezo wa kipkee wa kuleta majibu
kutoka kwa Mungu. Anatuelekeza kumwomba
Mungu baba, kwa JINA LA YESU, na anarudia maelekezo haya tena na tena (YOHANA
16:23-24). Shetani, adui yetu, hataki
kuona maombi yetu yakiwa na uwezo, hivyo mbinu yake kubwa, ni kutufanya tuombe
kinyume na maelekezo ya Yesu. Atatufanya
tuwaombe watakatifu Petro, Yohana, Yakoba, n.k.
watuombee. Yote haya, ni kinyume
na maelekezo haya ya Yesu. Maelekezo ya
Yesu kwetu ni “Nanyi Mkiomba“, kutufundisha wajibu weetu wa kuomba
wenyewe. Wanaotajwa kutuombea katika
Biblia, ni WAWILI TU, Roho Mtakatifu na Yesu mwenyewe; na hawa hufanya hivyo
kwetu, bila kuwaomba watuombee (WARUMI 8:26; 1 YOHANA 2:1). Bikira Mariamu, anjitaja yeye mwenyewe
kwkamba ni MJAKAZI WA BWANA, au mtumwa wa kike wa Mungu, na kamwe hajitaji kuwa
Mama wa Mungu (LUKA 1;38). Yesu kama
Mungu hana mama (WAEBRANIA 7:3). Bikira
Mariamu, ni mama yake Yesu katika ubinadamu wake tu. Bikira Mariamu, pamoja wanafunzi wengine wa
Yesu, wote walimwomba Baba kwa Jina la Yesu (MATENDO 1:13-15). Ktumia sanamu za watakatifu fulani katika
maombi yetu, vivyo hivyo ni kinyume na maelekezo haya. Mungu ni roho, inatupasa kumwabudu KATIKA
ROHO NA KWELI, na kuikimbia ibada ya sanamu, maana sanamu hizi ni dhambi (ISAYA
31:7; ZABURI 135:15-18; 1 WAKORINTHO 10:14).
(2)
HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI (MST. 13-14)
Yesu Kristo hapa anatuelezea juu ya hakika ya kujibiwa
maombi. Anasema, tukiomba kama
alivyotuelekeza kwa Jina la Yesu, hilo tunaloliomba, atalifanya. Hata hivyo, hatuna budi kuviondoa vikwazo
vingine vya kujibiwa maombi, vinavyotajwa katika maandiko, ili hakika ya
kujibiwa maombi itende kazi kwetu.
Hatuna budi kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu au Neno lake (1 YOHANA
5:14-15; MATHAYO 20:20-23). Hatuna budi
pasipo kutaka kuvitumia kwa tamaa zetu (YAKOBO 4:3). Hatuna budi kuomba pia kuwa mbali na dhambi
au uasi wa sheria za Mungu (MITHALI 28:9; 15:29; YAKOBO 4:2), na pia hatuna
budi kuomba kwa imani, pasipo shaka yoyote (YAKOBO 1:6-7). Tukiondoa vikwazo hivi, hatuna budi kuwa na
hakika ya kujibiwa maombi kwa wakati wa Mungu uliokubalika.
(3) ALAMA YA KUMPENDA
YESU (MST. 15, 21, 23-24)
Wako watu wengi ambao wanassema wanampenda Yesu, hata hivyo,
wengi kati yao wanapenda kwa neno tu, siyo kwa tendo na kweli (1 YOHANA
3:18). Yesu anatufundisha alama
itakayoonyesha kwa tendo na kweli kwamba tunampenda Yesu. Alama hii, ni kuzishika amri zake zote,
kulishika neno lake na kulitendea kazi kama lilivyo, bila kulijadili. Yeyote anayesema anampenda Yesu huku
hayashiki maneno yake, huyu ni mwongo.
(4)
MSAIDIZI MWINGINE (MST. 16-17, 25-26)
Yesu Kristo alipokuwa duniani, alikuwa Msaidizi wa kipekee
kwa wanafunzi wake. Hata sasa
anatusaidia sisi (2 WAKORINTHO 6:2; WAEBRANIA 2:18; 13:6). Kabla ya kuondoka, anatutambulisha kwa
Msaidizi mwingine. Msaidi huyu, siyo
Mtume Mohamed, kama wengine wanavyodai.
Msiaidizi huyu, ni ROHO WA KWELI, siyo mtu. Ulimwengu hauwezi kumpokea, wala kumwona kwa
macho, wala kumtambua; naye atakuwa NDANI ya wanafunzi wa Yesu, naye anakaa nao
MILELE (MST. 16-17). Sifa hizi zote,
haziko kwa mtume yeyote mwanadamu.
Wengine wote hawakuwa ndani ya watu na pia hawakukaa milele! Msaidizi huyu wingine ni ROHO MTAKATIFU (MST.
25-26). Huyu hutusaidia udhaifu wetu wa
kuomba (WARUMI 8:26), na kutufundisha na kutukumbusha yote, na kutuongoza
atutie kwenye kweli yote. Msaidizi huyu,
ni wa muhimu mno kwetu ikiwa tunataka kuwa mashahidi wa Yesu (MATENDO
1:8). Pasipo Msaidizi huyu, hatuwezi
kuwaleta watu kwa Yesu kwa mfanikio makubwa (YOHANA 16:7-8).
(5)
SITAWAACHA NINYI YATIMA (MST. 18-20)
Yesu hakutuacha yatima.
Siyo tu ametuachia Msaidizi mwingine, lakini tukiwa wawili watatu
tumekusanyika kwa jina lake, yupo kati yetu katika roho (MATHAYO 18:20). Kwa sasa tunamwona katika roho, hata hivyo
atakuja kwetu wakati wa kunyakuliwa kwa kansia na tutamwona katika utukufu wake
akiwa ndani ya Baba.
(6)
FAIDA ZA KUZISHIKA AMRI ZA YESU (MST. 21-23)
Tukizishika amri za yesu, Baba na Mwana wote hutupenda. Yesu akitupenda hivi, anajidhihirisha kwetu;
kutuonyesha upendo wake katika kututendea mengi, katika roho na mwili. Tukizishika amri za Yesu, Baba na Mwana,
hufanya makao kwetu. Wakifanya makao
kwetu, hatutapungukiwa kitu, wala hatuna haja tena ya kuogopa lolote.
(7)
MSIWE NA WOGA (MST. 27-29)
Woga, ni kinyume na imani (MARKO 4:40). Woga hautokani na Mungu, bali Shetani (2
TIMOTHEO 1:7). Tukiruhusu woga au hofu
kututawala, tunampa Ibilisi nafasi ya kutupa adhabu (WAEFESO 4:27; 1 YOHANA
4:18). Ikiwa baba, Mwana, wamefanya
makao kwetu, na roho Mtakatifu pia yuko ndani yetu, na ni Msaidizi wetu, kwa
nini tuogope kama kwamba tuko wenyewe?
Yesu kwa kutupa maelezo haya, anazidi kusema “Amani yangu nawapa“, Amani
nawaachieni“. Amani yake Yesu aliyotupa,
itafuta kila namna ya hofu ndani yetu.
Kama tuna hofu, tupokee amani hii ndani mwetu, kwa imani.
(8)
MKUU WA ULIMWENGU HUU HANA KITU KWA YESU (MST. 30)
Mkuu wa Ulimwengu huu yaani watu wa ulimwengu huu wenye
dhambi, ni Ibilisi au Shetani (1 YOHANA 5:19; WAEFESO 2:1-2; WAKOLOSAI
1:13). Yesu hapa, anatuhakikishia kwamba
Shetani hana kitu chochote kwake.
Tunapoomba na kuliitia Jina la Yesu, hatuna haja ya kuogopa, Shetani
hana kitu kwa Bwana wetu Yesu! Majini
yote hayana kitu kwake. Hatuna haja ya
kuogopa vitisho vya mapepo tukiwa na Yesu!
(9) JINSI YA KUUJULISHA ULIMWENGU YA
KUWA TUNAMPENDA BABA (MST.
31)
Hapa, Yesu anatuonyesha jinsi ya kuujulisha ulimwengu ya
kuwa tunampenda Baba. “Kama Baba alivyomwamuru, ndivyo afanyavyo“, ni
kielelezo cha Yesu kwetu. Je, kama baba
anavyotuamuru katika neno lake, ndivyo tufanyavyo? Kama sivyo, hatumpendi Baba! FULL GOSPEL
No comments:
Post a Comment