HUBIRINI MANENO LAINI YADANGANYAYO
Wengi wetu tayari tunafahamu kwamba moja ya kazi zilizo kuu
kabisa za Ibili ni kudanganya. Yeye anaitwa baba wa uongo, kazi yake kubwa ni
kuudanganya ulimwengu wote.
( UFUNUO 12:9 ), “…………audanganyaye ulimwengu wote, akatupwa hata nchi na
malaika zake wakatupwa pamoja naye”. Tangu wakati ule kazi yao kubwa ni
kuudanganya ulimwengu yamkini kama
ikiwezekana walimwengu wote wawe mbali
na kweli. Kweli ni neno la Mungu. Kweli ni neno lote la Mungu. Kazi ya Shetani
ni kuhakikisha wanadamu wote wanakuwa mbali na kweli. Atafanya juu chini
kulipotosha neno la Mungu. Ikiwa neno la Mungu kwa mfano linazungumza juu ya
Wokovu na Utakatifu hapa duniani.. Shetani atataka watu wafahamu kwamba
haiwezekani kuokoka duniani. Atawadanganya kwamba wokovu siyo hapa duniani ni mpaka mbinguni ili wakifa wakute hakuna
nafasi yoyote ya kuokoka na kujikuta
wakiwa Jehanum. Shetani anajua kuwa mtu amewekewa kufa mara moja na baada ya
kufa ni hukumu ( WAEBRANIA 9:27 ). Hakuna nafasi yoyote ya kusikia Injili baada
ya kufa na ndiyo maana neno linasema “heri wafu wafao katika Bwana maana
matendo yao yawatangulia”. Atawadanganya walimwengu ili wajue kwamba Utakatifu
siyo hapa duniani ni baada ya kufa na watakatifu ni wachache tu, na
wanateuliwa kwa vikao maalumu na
mchakato fulani wa kutafuta watakatifu.. Baada ya mtu kufa ndipo mchakato
unaanza na kuitwa mwenye heri na hatimaye
vikao hivyo vitaendelea na mtu
mmoja atatangaza kuwa mtu huyo ni mtakatifu wakati alishakufa. Watu wataamini
hivyo wakati Biblia haisemi hivyo. Biblia inasema kwamba kila mtu anayetaka
kuingia mbinguni na kukaa na Mungu milele anatakiwa kuwa mtakatifu.
( 1 PETRO 1:15-16 )
“Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi
iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa
watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu”.Hili ni agizo kwa kila mmoja wetu kwamba
tunatakiwa kuwa watakatifu tukiwa hapahapa duniani. ( TITO 2:12 ), “Nayo
yatufundisha kukataaa ubaya na tama za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na
haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa”.Utauwa maana yake utakatifu.
Neno la Mungu linatuagiza kuishi aisha ya uauwa hapahapa duniani katika ulimwengu
huu wa sasa. ( ZABURI 16:3 ),”Watakatifu waliopo duniani ndio waliobora, hao
ndio ninaopendezwa nao”.
Nyakati za kanisa
la kwanza haikuwa hivi kama leo katika madhehebu fulanifulani. Watakatifu
walikuwa ni watu waliookoka kwa kutubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha
kabisa na kutafuta utakaso. Tunaona watakatifu wengi wakiwa na majina ya
kizungu na hao ndio watakatifu wa leo katika madhehebu hayo ingawa wengine
walikuwa waovu wakubwa kabla ya kufa kwao. Mungu anataka kumuona kila aliyeokoka
akiwa mtakatifu. Tunaona nyaraka za Paulo Mtume ziliandikwa kwa watakatifu
waliokuwepo duniani nyakati za kanisa la kwanza:
(WAFILIPI 1:1 ),”Paulo na Timotheo, watumwa wa Kristo Yesu,
kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu, waliopo Filipi, pamoja na maaskofu na
mashemasi’. ( WAKOLOSAI 1:1-2 ),” Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya
Mungu, na Timotheo ndugu yake, kwa ndugu watakatifu, waaminifu katika Kristo,
walioko Kolosai. Neema na iwe kwenu, na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu”.
Hiyo ndiyo kweli kwamba pasipo kuishi maisha matakatifu hapa
duniani mtu hawezi kuingia mbinguni. (
WAEBRANIA 12:14 ), “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote na huo
utakatifu ambao hapana mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao”.
Shetani sasa
anataka kuwafanya watu wadanganyike
kuona utakatifu ni wa watu wachache
sana, tena watu fulanifulani. Anawafanya kuona kwamba kuokoka na kuishi
maisha matakatifu hapa duniani haiwezekani. Watu wanaoitwa eti ni
watakatifu ni waovu wakubwa. Wameishi
maisha hapa duniani wakiwa mbali na Wokovu. Kazi ya Shetani sasa ni kuudanganya
ulimwengu wote, si wawili watatu ambao watadanganywa bali ni watu wengi kila
mahali duniani. Kutakuwa na umati mkubwa wa watu kila mahal duniani ,
watachukuliwa na uongo huo.
Shetani anafanya kazi hii namna gani? Anafanya kazi hii kwa
kutuia pepo wa uongo.
Mungu alivyo kama mtu
ameamua mwenyewe kutokutaka kweli, anaachia roho ya upotevu kwake , anamwingiza
vizuri kabisa na kumwachia kudanganyika
. Tunaona mfano hapa:
Wakati wa Ahabu mfalme wa Israeli alikuwa hataki kuwaongoza
Waisraeli katika kweli , alikuwa amechagua kukaa katika uongo na akatamani
Waisraeli wote wawe waabudu miungu. Na kwa sababu alichagua kudanganyika ,
akapenda uongo kuliko kuipenda kweli . Mungu alimwachilia roho ya upotevu. Roho
hiyo ya upotevu ilizidi kumfunika ili hatimaye aangamizwe. Mungu mwenyewe ndiye
aliyewaruhusu roho hawa wa uongo kutenda kazi.
( 1 WAFALME 22:20-22 )
“Bwana akasema, ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili akwee
Ramoth-Gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi. Akatoka pepo,
akasimama mbele za BWANA, akasema,Mimi nitamdanganya. BWANA akamwambia, Jinsi
gani? Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo kinywani mwa manabiii wake
wote. Akasema, Utamdanganya na kudiliki pia; ondoka ukafanye hivyo”.
Maandiko yananena
waziwazi ya kwamba siku za mwisho zitakuwa siku za hatari, roho zidanganyazo
zitakuwa zinatenda kazi kwa namna isiyo ya kawaida. Watu watakuwa wakiupenda
uongo kuliko kuipenda kweli. Watu wengi watapenda na kufurahia kukaa katika
mafundisho ya mashetani. Siku za mwisho wadanganyaji watazidi kudanganya na
wale wanaodanganywa kuzidi kudanganywa. Na neno la Mungu halikutuficha.
( 1 TIMOTHEO 4:1 ), “Basi roho anena waziwazi ya kwamba
nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho
zidanganyazo,na mafundishoya mashetani”. ( 2 TIMOTHEO 3:1,), “Lakini ufahamu
neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako na nyakati za hatari”. Mstari 13 “
Lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea kuzidi kuwa waovu, wakidanganya
na kudanganyika”.
Nyakati za mwisho ni nyakati za hatari sana. Sehemu nyingine
katika Biblia inasema kuwa, Shetani
ameshuka mwenye ghadhabu nyingi sana akijua
muda wake uliobaki ni mchache sana. Kwa sababu hiyo, amemwaga roho
zidanganyazo kwa namna isiyo ya kawaida akiwa na lengo la kuudanganya ulimwengu
wote waiache imani . Watoke katika kweli halisi.
Kutokana na roho hizi ambazo zitawafanya watu kudanganywa na
kudanganyika , kama ilivyokuwa kwa Ahabu Pepo wa uongo aliingia katika vinywa
vya manabii wake wote. Watu wanaoitwa watumishi wa Mungu, wahubiri, ndani ya
vinywa vyao kutakuwa na pepo wa uongo. Watakuwa wanadanganya watu kwa wingi
wao. Lakini si hilo tu, kutakuwa na umati mkubwa wa watu ambao wanataka
kudanganywa. Watawaambia wahubiri “hubirini maneno laini yadanganyayo”.
Hawataki kusikia kweli wanataka kudanganywa. Watu wa namna hi watawatia moyo
wahubiri, yatakuwepo makanisa yanayojaa na kufulika kila kona kila mahali. Na itaonekana kana kwamba kuna uamsho kumbe ni roho
zidanganyazo zinafanya kazi. Ni pepo wa uongo wanafanya kazi.
Jambo la kusikitisha ni kwamba watu wengi wanataka
kudanganywa na hawapendi kweli, wanafurahia kukaa kwa mhubiri anayehubiri
maneno laini yanayodanganya na kumtia mtu faraja kwamba anaenda mbinguni wakati mhubiri ni
chafu nay eye anayehubiriwa wote ni wachafu. Nyakati tulizonazo zinaitwa
nyakati za hatari kwa sababu maasi yameongezeka kwa namna ya kutisha. Watu
wengi, wachungaji, wainjilisti, walimu na wengine ambao mwanzo walikuwa
wakifundisha kweli yote bila kuchuja neno lolote, wengi wao wamebadilika siku
hizi. Upendo wao wa kwanza umeshaibiwa na Adui. Zamani walikuwa wakikemea
dhambi ya kusuka nywele, kuvaa mapambo n.k kama yanenavyo maandiko leo kiko
wapi? ( 1 TIMOTHEO 2:9-10; 1 PETRO 3:3-5 ). Yesu alisema siku za mwisho wengi
upendo wao utapoa kwa sababu ya kuongezeka maasi ( MATHAYO 24:12
).
Maasi yatakuwa yameongezeka kama nyakati za nabii Isaya.
Nabiin Isaya hakuwa na mchezo na dhambi kama tunavyoona kwa watumishi wengine
nyakati hizi. Isaya alikuwa anahubiri kweli na watu hawakutaka kumsikia kwa
kuwa walipenda kudanganywa. Historia ya nyakati zile za nabii Isaya inaeleza
kuwa kweli aliyokuwa akiihubiri
iliwaudhi sana watu. Watu wa nyakati zile hawakutaka kuyasikia mafundisho yake
kiasi kwamba aliitwa na kuambiwa ‘utaendelea kufundisha maneno haya mazito ya
kukwaza na kuwafanya watu kila wakati kuambiwa
wachafu na waovu?”. Unaweza kuona kwa mfano mahubiri yake yalivyokuwa (
ISAYA 1:3-18 ). Nabii Isaya aliwaitwa watu wale kuwa ni watu wa Sodoma tena ni
watu wa Gommora. Aliwaita watu wachafu kwa namna ileile ya watu wa Sodoma na
Gomora.. Kutokana na mahubiri yake ya usafi
( utakatifu ) watu wengi walikwazika. Hatimaye Isaya aliitwa na wakuu,
wakamwambia mahubiri yake yanakwaza watu, wakati wote dhambi dhambi dhambi dhambi. Acha kuhubiri dhambi, acha
kuhubiri maneno hayo, hubiri tu maneno laini yadanganyayo. Lakini nabii wa
Mungu Isaya hakutaka kuchuja viwango vya utakatifu na waka,wambia kama hutaki tutakukata pingili moja ya kidole
kimoja kimoja mpaka tumalize vidole vyote. Lakini Isaya alisema siko tayari
kuchuja viwango. Historia hiyo inaeleza kuwa walimkata pingili mojamoja ya kila
kidole kwa msumeno, damu ikichuluzika huku akiulizwa “ Isaya hutaki kuchuja
viwango? Hutaki kuhubiri maneno laini?”. Isaya alisema kila neno ambalo Bwana
ananipa ndilo nitakalolihubiri. Walipomaliza kukata vidole vya mikono
waliendelea na vidole vya miguu mpaka alipokata roho na kufa.
Nyakati za nabii Isaya walikuwepo watu waasi ambao walitaka
wahubiriwe maneno laini yadanganyayo
( ISAYA
30:9-10 )
“Kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo,
watoto wasiotaka kusikia sheria ya BWANA; Wawaambiao waonaji, Msione, na manabii,
Msitoe unabii wa mambo ya haki, tuambieni maneno laini, hubirini maneno
yadanganyayo”.
Hawakumtaka Isaya lakini waliwataka wahubiri watakaokuwa
tayari kuwahubiri laini yadanganyayo. Hao ndio waliowapenda, hao ndio
waliowatukuza, waliowasifu kwamba wana
upako, hao ndio waliowasifia kwamba ndio watumishi wa Mungu. Mhubiri Isaya
hakuwa kati yao, alipingana nao. Na sisi wahubiri wa leo tusiwe miongoni mwa
walimu wengi wanaochuja neno na
kufundisha maneno laini yadanganyayo. Tusifundishe mafundisho ya kuwapendezesha
watu bali tufundishe kweli ya neno la Mungu kama ilivyo bila kujali lolote
litakalotokea kwa viwango hivyo.
Wakati wa Paulo mtume walikuwepo watu waliohubiri maneno
laini yadanganyayo na Paulo mtume alipambana wao. Paulo alisema watu wanaohubiri maneno laini
yadanganyayo hawamtumikiii Kristo bali
wanatumikia matumbo yao wenyewe.
(
WARUMI 16:17-18 )
“Ndugu zangu, nawasihi, wale wafanyao fitina na mambo ya
kukwaza kinyume cha mafundisho mliyojifunza, mkajiepushe nao. Kwa sababu walio
hivyo hawamtumikii Bwana wetu Kristo, bali matumbo yao yenyewe; na kwa maneno
laini nay a kujipendekeza waidanganya
mioyo ya watu wanyofu.”
Walikuwepo wahubiri nyakatiza Paulo waliopingana na Paulo
katika kufundisha neno la Mungu. Wahubiri hao waliwaambia watu kuwa wanaweza
kufanya dhambi na wakaingia mbinguni. Kwamba wanaweza kuazini lakini wakaingia
mbinguni. Paulo mtume yeye alizidi kusisitiza katika mafundisho akisema
“msidanganyike”
( WAEFESO 5:3,5-6 ; 1 WAKORINTHO 6:9-10 )
Watu wapendao
uongo na kuufanya hawawezi kuingia mbinguni
(
UFUNUO 22:14-15 )
“Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mji wa
uzima na kuingia mjini kwa milango yake. Huko nje wako mbwa, na wachawi, na
wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na
kuufanya” Watu wanaoufanya uongo ni wale wanaoigiza maigizo. Mtu anaigiza
uchungaji akiwa yeye siyo mchungaji, anawadanganya watu wanaotazama. Namna
yoyote ya kuigiza yaisha ya watu wengine kwa mfano watakatifu wa zamani.
Tunaweza kuona filamu zinazoitwa za Musa, Paulo,, n.k jambo la kushangaza ni
kwamba nyakati zao haikuwepo teknolojia ya video tulionayo leo. Hazikuwepo
video camera wakati ule. Neno la Mungu latosha kwa kujifunza na kuamini si
mpaka kuona. Yesu alisema wa heri wale watakaosadiki pasipo kuona.. Imani huja
kwa kusikia na siyo kwa kuona. Watu wote wanaoangalia filamu zote na maigizo
wote wanaupenda uongo. Hata kama wewe ni mchungaji au mtu unayesema umeokoka
hauna nafasi katika nji ule wa mbinguni kama unapenda uongo wa ect za maigizo
na filamu. Wanaocheza bahati na sibu katika simu n.k wote wanaupenda uongo.
Wanatuma sms kwa Tsh 150 n.k kwa kudanganywa eti watashinda Gari la mamilioni
lakini mtu mmoja katika nchi nzima ndiye anakuwa mshindi na watu wote wanaliwa
. Wachungaji wana wanaoshusha viwango vya neno la Mungu na kuwaambia watu
kusuka nywele siyo shida kiroho, kupaka wanja, kujichubua, kuvaa wigi, kuvaa
laster, suruali kwa wanawake, mapambo n.k wote hawa wanaufanya uongo. Mbona
Pentekeoste ya miaka ya nyuma ilikuwa ikikemea mambo hayo tena msisitizo na
hatua kali zikichukuliwa kwa watu waliofanya hivyo. Wote wanaovaa mavazi hayo
kinyume na neno la Mungu kwa kuwasikiliza walimu wao wa madhehebu yao au
mengine wote wanapenda uongo. Watu wa namna hii hawana nafasi katika uzima wa
milele ( UFUNUO 22;14-15 )
Mtu anaweza kuhama
kanisa kwa kukimbia viwango vya neno la
Mungu na kutafuta kanisa lingine ambalo linaruhusu hicho anachotaka kufanya. Ni
kweli makanisa yako mengi lakini kweli ya neno la Mungu ni moja tu. Madhehebu
ni mengi lakini kanisa la Yesu ni moja tu nalo ni lile linaloongozwa na kweli
yote. Njia ya kutufikisha mbinguni ni moja tu, Yesu Kristo Mwana wa Mungu.
Tunaingia mbinguni kwa kutii maagizo yote ya Mungu katika Neno lake ( ZABURI
119:6 ).
Wapo walimu wengi ( wahubiri ) watakaofundisha maneno laini yadanganyayo na kusema Mungu haangalii mambo ya mwili , anaangalia
mambo ya roho tu. Watu watafurahia kuwepo kwa wahubiri hao kwa kwa sababu
wanawatia moyo kuendelea kuvaa vyovyote na chochote katika mwili. Je, ni kweli
kwamba utakatifu ni rohoni tu na siyo katika mwili na roho? Ukweli wa jambo
hili unapatikana katika maandiko yenyewe. Biblia inasema utakatifu ni mwili na
roho ( 1 WAKORINTHO 7:34; 2WAKORINTHO 7:1; 1WATHESALONIKE 5:23; MATHAYO
23:25-26 ).. Wanawatia moyo watu na kuwaambia “msimsikilize Kakobe Mungu
haangalii mambo ya mwili anaangalia mambo ya roho”. Huo ni uongo wa mchana kweupe. Je uasherati
na uzinzi ni mambo ya roho. Unafikiri roho ndizo zinafanya uasherati? Kama
Mungu haangalii mambo ya mwili wahubiri kuwa uasherati siyo shida. Je mtu anapo
muua mwenzie kinachokufa ni roho? Kama ni mwili basi hata mauaji siyo shida. Je
watu wanapopigana zinapigana roho? Kama ni miili mbona wahubiri hao wanahubiri
kuwa kupigana ni dhambi?
Hapa Full Gospel yupo Isaya, hakuna maneno laini. Tunaishi
kwa kweli yote kama mtu hataki kuishi sawasawa na Neno lote la Mungu tusimuone
jumapili ijayo. Sipo tayari kuhubiri uongo na kuwafariji watu eti wanaweza
kwenda mbinguni na kuchubua ngozi, na mawigi yao,na heleni, mikufu, bangili, na
uchafu wote wa kila namna.. Hivyo ni vifaa vya makahaba. Hakuna watu wanaocheza
rapu, wanaonengua viungo makanisani, wanaocheza karata, wanaocheza drafti,
wanaocheza bahati na sibu, n.k watakaoingia mbinguni. Bahati na sibu zote ni
kamali. Chochote kilicho kinyonge hakitaingia katika mji ule.
Ikiwa umeamua kuokolewa utakuwa tofauti kabisa na ulimwengu.
Watu wengine wanasema, “Kakobe inamaana wewe tu na kanisa lako la Full Gospel
ndiyo watakatifu tu?”. Ni kweli watakatifu hawako Full Gospel peke yake tu
lakini hata wakiwa popote tutawatambua kwa matunda yao. Kweli ni moja tu
aliyoihubiri Paulo mtume.
( WAGALATIA 1:6-9 )
“Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliye waita
katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine. Wala si nyingine;
lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo. Lakini
ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa
hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe. Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema
tena mtu awayeyote akiwahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa hiyo mliyopokea,
na alaaniwe”.
Yeyote ambaye haihubiri injili ya Paulo mtume tayari
amekwisha kulaaniwa sawasawa na andiko hilo hapo juu. Paulo mtume anahubiri
injili ya namna gani?
“Wanawake wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri sikwa kusuka
nywele wala kwa dhahabu na lulu kama wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu ( 1 TIMOTHEO 2:9-10 )
Mume
amefungwa na mkewe mpaka kifo kiwatenganishe. Ikiwa wameachana wakae hakuna
kuoa wala kuolewa au wapatane tena na
kuishi pamoja ( wasameheane).
( 1 WAKORINTHO 7:10-11,; WARUMI 7:2-3 )
Kwa hiyo
imempasa mwanamke ( imempasa yaani ni
lazima ) awe na dalili ya kumilikiwa kichwani kwa ajili ya malaika ( 1
WAKORINTHO 11:10 ).
Mwanamke anapaswa kufunika kichwa chake kwa kilemba (
kitambaa ) wakati wote awapo kanisani na wakati wote wa kuomba au katika ibada
ya aina yoyote. Tumezoea kuona wanaume wakivua kofia lakini tunashindwa kujua
kuwa sheria hiyohiyo ndiyo inamtaka mwanamke kufunika kichwa. Malaika wanataka
order ( utaratibu ) ili mamlaka ya Kristo ambaye ni Kichwa cha Kanisa iweze
kutenda kazi.
Yeyote ambaye hahubiri injili hii amelaaniwa na watu ambao
wanamfuata wamedanganyika, wameuamini uongo. Siku ile ya mwisho kila mtu bila
kujali yuko Assemblies of God, Church of God,
Full Gospel, Cathoric, Anglican n.k, atahukumiwa kwa injili ya Paulo
mtume na siyo kwa injili anayohubiriwa na Pandrii wake, siyo kwa injili
inayohubiriwa na Askofu wake anayehubiri uongo.
(
WARUMI 2:16 )
“Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu wote
sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu” Watu wote watahukumi kwa injili
hiyohiyo ya Paulo mtume inayokataza mapambo, inayowaagiza wanawake kufunika
vichwa wawapo kanisani na wakati wote wa ibada. Unapokimbia injli hiyo ya Paulo
na kusema na sisi kwetu kuna inahubiriwa injili. Hiyo ni injili ya namna
nyingine. Kweli nin injli iliyohubiriwa na Paulo mtume. Tunapaswa kuwa mbali na
walimu wengi wa uongo wanaotuzunguka, watu wanaolipindisha Neno la Mungu kwa
kusudi ili wawe na washirika wengi na kupata sadaka nyingi. Mungu wao ni tumbo
kama Paulo alivyosema (
WARUMI 16:17-18 )
Watu ambao hawataki kweli lakini wanataka kuendelea kuona uwepo wa Mungu kwao ili wajifariji
kwamba Mungu anakubaliana na mawigi na
kujikoboa ngozi. Mungu atawaachilia pepo wafanye miujiza ili wazidi kupotea
hatimaye waweze kuangamizwa. Unafikiri mapepo hayawezi kufanya miujiza ?
Kumbuka wakati wa Musa na Haruni, waganga na wachawi wa Haruni waliweza kufanya
miujiza..
Siku hizi za mwisho roho ya Asi ( mpinga Kristo ) inafanya
kazi na tunaona uasi wa kila namna hata makanisani. Watu hawataki kukaa katika
Neno la Mungu. Ni kizazi cha Laudikia. Neno Laudikia katika lugha ya asili
maana yake ni “freedom of the right” kwa Kiswahili “Uhuru wa washirika
kutakakufanya wanachotakakufanya na wasiambiwe na wasikemewe kwa lolote” Kanisa
Laudikia liko hivyo. Makanisa mengi siku hizi za mwisho yamekuwa vuguvugu na
yanaelekea kuwa baridi kabisa ( UFUNUO 3:15-16 ). Ukweli ni kwamba na washirika
wa akanisa hayo wamepoa kutokana na
mafundisho laini yadanganyayo wanayohubiriwa kinyume na Kweli ya Paulo mtume.
Msingi wa mmafundisho ya mitume umeachwa na ndiyo maana kazi zilizofanywa na
mitume na matokeo yake hatuzioni maishani mwetu. Mitume waliweza kuupindua
ulimwengu bila vyombo vya usafirsi kama vile ndege, magari, pikipiki, baiskeli
n.k. ( MATENDO 17:6 )
Paulo mtume
alitabiri juu ya nyakati hizi tulizonazo. Alisema kuwa watu wengi hawatapenda
kweli, watapenda kudanganywa hivyo watajitafutia walimu makundimakundi kwa
sababu wana masikio ya utafiti. ( 2TIMOTHEO 4:3-4 )
Mpendwa msomaji, baada ya kusikia yote haya kutoka kwa nabii
aliyetumwa kukuletea ujumbe huu, usifanye moyo wako kuwa mgumu. Hii ni nafasi ya kipekee ya kuokoka. Je, unajuaje kama utaamka kitandani baada ya
kulala usiku wa leo? Wakati uliokubalika
wa wokovu ni sasa (2 WAKORINTHO 6:2).
Labda utaniuliza, ili uokoke, ufanyeje?
Jibu ni rahisi, kwa imani ukitubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha,
na kumwambia Yesu Kristo akusamehe, utasamehewa sasa hivi, na msamaha wa
dhambi, huambatana na wokovu (LUKA 1:77).
Je, uko tayari kuokoka sasa hivi?
Najua uko tayari. Basi fuatisha sala hii kwa dhati toka moyoni, “Mungu
baba asante kwa kuniletea ujumbe huu.Natubu dhambi zangu zote, kwa kumaanisha
kuziacha. Yesu Kristo nakuomba unisamehe dhambi zangu na kunipa uwezo wa
kushinda dhambi na kuniokoa kutoka katika mateso ya moto wa milele. Asante, kwa
kuniokoa katika Jina la Yesu. Amen”. Tayari sasa umeokoka, na kwa hakika unakwenda
mbinguni sasa, hata ukifa leo. Ili uzidi
kuukulia wokovu, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri
wokovu. MUNGU AKUBARIKI !!!
No comments:
Post a Comment