Ina maana gani kwamba mshahara wa dhambi ni mauti?

Warumi 6:23 inasema, "Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu." Katika msingi wake, dhambi ni uasi dhidi ya Mungu. Dhambi zetu hututenganisha na Mungu, Muumba na mwenye uzima. Yesu alisema, "Mimi ndimi njia na kweli na uzima" (Yohana 14: 6). Mungu anajulikana kama "MIMI NDIMI" mkuu. Uzima uu katika Mungu. Kwa hivyo, tunapofanya dhambi na kujitenganisha na Mungu, tunatengana na uzima wa kweli. Kwa hivyo, bila shaka, tunakumbana na mauti. Hoja tatu za ufafanuzi zinahitajika: Kwanza, dhambi hasa haisababishi kifo cha kimwili mara moja. Warumi 6 haituambii kwamba tunapofanya dhambi tutakufa kimwili. Badala yake, inarejelea kifo cha kiroho. Pili, wakati tunapookoka katika Kristo, tunaokolewa kutokana na hatima ya kifo cha kiroho na kuletwa katika hatima ya uzima wa kiroho. Paulo aliwaambia Warumi, "Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu" (Warumi 6:23). Tatu, hata dhambi za waumini bila shaka zitasababisha aina ya "kifo" cha kiroho. Ingawa tumeokolewa kutokana na adhabu ya mwisho ya dhambi (kutengwa kwa milele na Mungu), hatuokolewa kutokana na matokeo ya asili ya uhusiano uliovunjika na Baba . Tunapofanya dhambi, tunapata dalili za kifo cha kiroho. Tunaweza kujihisi kuwa na hatia, kuwa wapungufu, kuchanganyikiwa, au kutokuwa na uhusiano na Mungu. Sisi hufanya kama waadilifu badala ya kuwa wenye haki. Dhambi zetu, hata kama waumini, huumiza moyo wa Mungu na uhuzunisha Roho Wake (Waefeso 4:30). Ingawa dhambi zetu haziachi uhusiano wetu na Yeye, huweka kizuizi kati yetu. Fikiria mtoto na mzazi. Wakati mtoto anapoasi, uhusiano na mzazi wake unafadhaika. Mzazi bado anampenda mtoto na bado ana nia bora kwa mtoto moyoni. Mtoto kamwe aachi kuwa bila mzazi. Hata hivyo, mtoto anaweza kupata matokeo fulani: kutoaminiwa, nidhamu, hisia ya hatia, na kadhalika. Bila shaka hatimaye uhusiano hurejeshwa ila kawaida pigo huja kwanza. Hivyo ni pamoja nasi na Mungu. Tunapoasi dhidi ya utawala wa Mungu katika maisha yetu, tunaasi dhidi ya Uzima, na hivyo tunakumbana na mauti (kuvunjika kunaosababisha maumivu). Tunapomrudia Mungu, tunarudishwa tena kwenye ushirika wa kiroho na Mungu, hisia za lengo, haki, uhuru, nk. Baba mwenye furaha katika mfano wa Mwana mpotevu alisema vizuri zaidi: "Huyu mtoto wangu alikuwa amekufa na yu hai tena "(Luka 15:24).

MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU

 

 MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU

 

   Kama vile kunavyokuwako na mwisho wa dakika, saa, siku, wiki, mwezi, mwaka, karne, milenia au “millennium”, ndivyo kutakavyokuwako pia na “mwisho wa dunia” na “siku za mwisho”. Chenye mwanzo, hakikosi kuwa na mwisho. Biblia inaeleza juu ya siku za mwisho (1 TIMOTHEO 4:1), mwisho wa dunia (MATHAYO 24:3), n.k. Sasa basi, maandiko matakatifu yanatuonyesha kwamba tunapaswa kujiangalia, ili siku ya mwisho isitujie ghafla; kama mtego unasavyo ( LUKA 21:34-35 ). Ndiyo maana leo,  tunajifunza somo,”MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU”. Tutajifunza somo hili, kwa  kulitafakari katika vipengele vine:-

 

( 1 ).  MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU

 

( 2 ).  KUNYAKULIWA KWA WATAKATIFU

 

( 3 ).  DHIKI KUBWA AMBAYO HAIJAWAHI KUTOKEA TANGU              KUUMBWA KWA ULIMWENGU

 

( 4 ).  JINSI YA KUFANYA ILI KUNYAKULIWA

 

( 1 ).  MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU

 

Katika Kalenda ya Mungu, inayothibitishwa na Historia ya  Biblia, tunapomaliza mwaka huu wa 2000, inakuwa  imetimia miaka 6000 tangu Adamu, mtu wa kwanza alipoumbwa na kuishi duniani. Kuanzia wakati wa kuumbwa Adamu mpaka wakati wa kuzaliwa Ibrahimu, ni miaka 2000. Kuanzia wakati wa kuzaliwa Ibrahimu mpaka wakati wa kuzaliwa Yesu Kristo, ni miaka 2000. Wana historia wakubwa wa karne ya kwanza hadi ya nne kama mwanahistoria mkubwa JEROME aliyeishi katika miaka ya mwisho ya karne ya 4, kunako mwaka wa 392. B.K; alihifadhi historia kubwa ya vizazi vya wanadamu. Sasa basi, katika unabii, miaka 1000, ni sawa na siku moja ( 2PETRO 3:8 ). Hivyo inapotimia miaka 6000 ,maana yake, zinakuwa zimetimia siku sita, na tunapoanza sasa milenia au millennium nyingine au miaka 1000 mingine, maana yake ni kwamba, tunaanza siku ya saba. Katika kalenda ya Mungu, miaka hii 2000 baada ya Yesu Kristo inayotimiza siku sita tangu Adamu inaitwa siku za mwisho.

 

Miaka ipatayo 34 baada ya kuzaliwa Kristo, ndipo ilipotimia siku ya pentekoste, ambayo wanafunzi wa Yesu walipokea nguvu ya Roho Mtakatifu(LUKA 3:23, MATENDO 1:1-14; 2:1-4). Ujazo huu wa Roho Mtakatifu, uliwafanya watu wengi kufikiri ni kulewa mvinyo mpya, na Petro aliposimama kufafanua, alisema kwamba jambo hilo limetokea katika siku za mwisho sawasawa na unabii wa Nabii Yoeli(MATENDO 2:5-18). Kumbe basi milenia mbili baada ya Kristo inatimiza siku ya sita inayofayofanya siku za mwisho. Ni kama siku ya ijumaa, mwisho wa wiki. Na siku ya saba, ni kama jumamosi katika wiki. Zamani hizo za unabii wa Nabii Yoeli, siku ya saba, yaani jumamosi katika wiki ilikuwa sabato.

 

( 2 ). KUNYAKULIWA KWA WATAKATIFU

 

Milenia ya saba tayari inatangazwa kuanza mwanzo wa mwaka huu tarehe 1 january 2000. Maana yake ni kwamba tayari tumeanza siku ya saba. Ni mapema alfajiri siku ya saba katika unabii.Siku hii ya saba kama tulivyokwisha kujifunza, Yesu atakuja mawinguni, na kwa namna ya sumaku kuvuta chuma, atawavuta au kuwanyakua watakatifu walioko duniani ( 1WATHESALONIKE 4:13-17 ; ZABURI 16:3; 1WAKORINTHO 15:50-54 ). Kama ni usiku watakuwako wawili kitandani mmoja aliyeishi mbali na dhambi atwaliwa, mmoja aliyelipuuza neno la Mungu aachwa. Kama -ni mchana, wawili watakuweko kondeni (shambani ), mmoja atwaliwa, mwingine   aachwa,(MATHAYO 24:40-41) .Kunyakuliwa kwa kanisa hasa kutakuwa siku ipi, tarehe ipi, mwezi upi, au mwaka upi? Biblia haitaji tarehe halisi, tunachojua tu ni siku ya saba na dalili zake zote tayari. Yesu anakuja ghafla kama mwivi wa namna iliyozoeleka, asivyotoa taarifa ya kuja kuiba. Hata hivyo wengi wasiojua kwamba tayari siku ya saba imeanza, watajikuta hawajitayarisha ( MATHAYO 24:3-14, 36-41 ).

 

( 3 ).  DHIKI KUBWA AMBAYO HAIJAWAHI KUTOKEA TANGU KUUMBWA  KWA ULIMWENGU                       

 

Baada tu ya kunyakuliwa watakatiifu, hapa duniani kwa wale wenye dhambi ambao hawakutaka kutubu dhambi zao, na kuziacha ili waokolewe kutoka katika dhiki hiyo, watakuwa katika dhiki hiyo, watakuwa katika dhiki kubwa ambayo haijawahi kutokea tangu kuumbwa kwa ulimwengu ( MATHAYO 24:21 ). Dhiki hii itakuwa ya miaka saba na itakuwa ya kutisha. Watu watatamani kufa, lakini mauti itawakimbia (UFUNUO 9:1-10 ; 6:15-17; 16:1-21). Kama ilivyokuwa siku za Nuhu na wakati wa Sodoma na Gomora, Mungu hawaadhibu waliowake. Wenye haki hutengwa pembeni kabla ya wasiohaki kuteswa kwa ghadhabu ya Mungu. Kwa sababu hiyo, watu waliojitenga na dhambi, wataokoka kutoka katika dhiki kubwa. Nuhu na jamii yake wenye haki waliondolewa na kuwekwa safinani kabla ya ghalika kuja. Luthu na jamaa yake wenye haki walitengwa na wenye dhambi kabla ya Sodoma na Gomora kuteketezwa ( MWANZO 18:20-33; 19:1-24; MATHAYO 24:37-39; LUKA 17:26, 28-30 ).

 

( 4 ). JINSI YA KUFANYA ILI KUNYAKULIWA.

 

Mungu wetu ni Mungu wa upendo, hapendi hata mmoja ateseke. Moto wa milele na mateso yote ya jinsi hii hakuwekewa mwanadamu, bali Ibilisi na malaika zake ( MATHAYO 25:41 ). Hata sasa Mungu anasubiri kwa upendo wake ili tutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kuziacha na kuokolewa ( MITHALI 28:13; WARUMI 2:4-5; 2PETRO 3:9 ).Kusamehewa dhambi zetu huambatana na kuokolewa kutoka katika dhiki kubwa na hivyo kunyakuliwa na Bwana Yesu (LUKA 1:77 ). Yote haya hufanyika kwa imani tu katika Yesu Kristo aliyejaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote bila kutenda dhambi, kwa uwezo wa Roho Mtakatifu si kwa uwezo wetu  wala kwa nguvu zetu ( ZEKARIA 4:6; WAFILIPI 4:13; WAEBRANIA 4:14-16 ). Baada ya hapo kama watoto wachanga wa kiroho tuzidi kujifunza neno ambalo ni maziwa yasiyoghoshiwa ( yasiyochanganywa na maji ) ili tuukulie wokovu. Bila kuhudhuria ibada hizi kadri tunapopata nafasi, ni rahisi tena kujikuta tumeanguka dhambini tena. Utakatifu hudumu kwa neno ( ZABURI 119:11; YOHANA 15:3 )..

 

                ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

 

         Ni sifa ipi ya kutuwezesha kuingia mbinguni?  Ni utakatifu (WAEBRANIA 12:14).  Ndani yake hakitaingia kamwe chochote kilicho kinyonge (UFUNUO WA YOHANA 21:27).  Kinyonge ni kipi?  Ni yule anayetenda dhambi.  Huyu ni mtu asiyefaa, ni mnyonge!  Je, wewe ni mtakatifu?  Jibu ni la!  Maisha yako yamejaa dhambi, pamoja na kusema una dini; hivyo wewe pia ni mnyonge, hufai kuingia mbinguni. Ukitubu leo dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na kuifuata njia ya Yesu Kristo, ndipo utakapopata rehema ya kuingia mbinguni (MITHALI 28:13;  YOHANA 14:6).  Je, uko tayari kutubu sasa ili upate rehema hii?  Najua uko tayari.  Basi fuatisha sala hii ya toba kwa dhati kutoka moyoni;  “Mungu Baba asante kwa ujumbe huu.  Hakika mimi ni mnyonge, mwenye dhambi.  Sistahili kuingia mbinguni. Natubu dhambi zangu zote kwa kumaanisha kuziacha.  Kuanzia leo nataka niifuate njia ya Yesu Kristo.  Bwana Yesu niwezeshe.  Asante kwa kunisikia katika Jina la Yesu.  Amen”.  Mpendwa msomaji umekubaliwa kuingia mbinguni.  Ili uzidi kudumu katika utakatifu mpaka siku ya kuiaga dunia hii, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu.  MUNGU AKUBARIKI !!!

 

No comments: