Ina maana gani kwamba mshahara wa dhambi ni mauti?

Warumi 6:23 inasema, "Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu." Katika msingi wake, dhambi ni uasi dhidi ya Mungu. Dhambi zetu hututenganisha na Mungu, Muumba na mwenye uzima. Yesu alisema, "Mimi ndimi njia na kweli na uzima" (Yohana 14: 6). Mungu anajulikana kama "MIMI NDIMI" mkuu. Uzima uu katika Mungu. Kwa hivyo, tunapofanya dhambi na kujitenganisha na Mungu, tunatengana na uzima wa kweli. Kwa hivyo, bila shaka, tunakumbana na mauti. Hoja tatu za ufafanuzi zinahitajika: Kwanza, dhambi hasa haisababishi kifo cha kimwili mara moja. Warumi 6 haituambii kwamba tunapofanya dhambi tutakufa kimwili. Badala yake, inarejelea kifo cha kiroho. Pili, wakati tunapookoka katika Kristo, tunaokolewa kutokana na hatima ya kifo cha kiroho na kuletwa katika hatima ya uzima wa kiroho. Paulo aliwaambia Warumi, "Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu" (Warumi 6:23). Tatu, hata dhambi za waumini bila shaka zitasababisha aina ya "kifo" cha kiroho. Ingawa tumeokolewa kutokana na adhabu ya mwisho ya dhambi (kutengwa kwa milele na Mungu), hatuokolewa kutokana na matokeo ya asili ya uhusiano uliovunjika na Baba . Tunapofanya dhambi, tunapata dalili za kifo cha kiroho. Tunaweza kujihisi kuwa na hatia, kuwa wapungufu, kuchanganyikiwa, au kutokuwa na uhusiano na Mungu. Sisi hufanya kama waadilifu badala ya kuwa wenye haki. Dhambi zetu, hata kama waumini, huumiza moyo wa Mungu na uhuzunisha Roho Wake (Waefeso 4:30). Ingawa dhambi zetu haziachi uhusiano wetu na Yeye, huweka kizuizi kati yetu. Fikiria mtoto na mzazi. Wakati mtoto anapoasi, uhusiano na mzazi wake unafadhaika. Mzazi bado anampenda mtoto na bado ana nia bora kwa mtoto moyoni. Mtoto kamwe aachi kuwa bila mzazi. Hata hivyo, mtoto anaweza kupata matokeo fulani: kutoaminiwa, nidhamu, hisia ya hatia, na kadhalika. Bila shaka hatimaye uhusiano hurejeshwa ila kawaida pigo huja kwanza. Hivyo ni pamoja nasi na Mungu. Tunapoasi dhidi ya utawala wa Mungu katika maisha yetu, tunaasi dhidi ya Uzima, na hivyo tunakumbana na mauti (kuvunjika kunaosababisha maumivu). Tunapomrudia Mungu, tunarudishwa tena kwenye ushirika wa kiroho na Mungu, hisia za lengo, haki, uhuru, nk. Baba mwenye furaha katika mfano wa Mwana mpotevu alisema vizuri zaidi: "Huyu mtoto wangu alikuwa amekufa na yu hai tena "(Luka 15:24).

CHUKI NA MAUDHI KWA MKRISTO

 

CHUKI NA MAUDHI KWA MKRISTO

Mkristo, ni mtu anayemfuata Yesu Kristo katika tabia, na utumishi wake kwa Mungu.  Mkristo, ni mtu aliyezaliwa mara ya pili, mtu aliyeokoka.  Watu ambao hawajaokoka, siyo Wakristo kwa msingi wa Biblia.  Katika somo la leo la Kuichambua Biblia, tutatafakari kwa makini YOHANA 15:18-27; 16:1-4.  Katika mistari hii, pamoja na mambo mengine kadha, tunajifunza kipekee juu ya “CHUKI NA MAUDHI KWA MKRISTO“.  Tutayagawa mafundisho yote tunayoyapata katika mistari hii katika vipengele kumi na viwili:-

 

 

 

(1)      MAANA YA “ULIMWENGU“ (15:18);

 

(2)      ULIMWENGU HUWAPENDA WALIO WAKE (15:19);

 

(3)      ULIMWENGU HUWACHUKIA WATU WASIO WA ULIMWENGU (15:19);

 

(4)      ULIMWENGU HUWACHUKIA NA KUWAUDHI WATUMISHI WA MUNGU  

 

      (15:19-20);

 

(5)      MTUMWA SI MKUBWA KULIKO BWANA WAKE (15:20);

 

(6)      ULIMWENGU KUTOKULISHIKA NENO (15:20);

 

(7)      SABABU YA ULIMWENGU KUTUCHUKIA NA KUTUUDHI (15:21; 16:3);

 

(8)      WAJIBU WA KUONDOA UDHURU WA WENYE DHAMBI (15:22);

 

(9)      WALINICHUKIA BURE (15:23-26);

 

(10)       ROHO MTAKATIFU HUMSHUHUDIA YESU PAMOJA NASI (15:26-27);

 

(11)       SABABU YA KUELEZWA MAPEMA JUU YA KUCHUKIWA NA   

 

       KUUDHIWA   (16:1,4);

 

(12)       KUTENGWA HATA KUUAWA KWA WAKRISTO (16:2)

 

 

 

 

 

(1)            MAANA YA “ULIMWENGU“ (15:18)

 

Ni muhimu kufahamu maana ya neno “Ulimwengu“, kabla ya kuendelea kujifunza somo hili.  Neno “Ulimwengu“, kama linavyotumika katika mistari hii, linamaanisha watu wa Ibilisi yule mwovu, watu ambao hawajaokoka; pamoja na mkuu wa ulimwengu Ibilisi mwenyewe.  “Ulimwengu“, pia unawajumuisha watu wanaojiita wameokoka, wakati bado ni watu wanaoipenda dunia na marafiki wa dunia, yaani wanafanya mambo yote tu kama mataifa (1 YOHANA 5:18-19; YOHANA 14:30; YAKOBO 4:4; 1 YOHANA 2:15-17).  Watu waliookoka wanaoishi maisha yaliyo tofauti na ulimwengu, hawa si wa ulimwengu huu (YOHANA 17:14,16).

 

 

 

(2)              ULIMWENGU HUWAPENDA WALIO WAKE (15:19)

 

Watu wanaonena ya dunia, husikiwa na dunia na kupendwa na ulimwengu (1 YOHANA 4:5; YOHANA 7:7).  Shetani, pamoja na watu ambao hawajaokoka, na pia watu wanaojiita wameokoka lakini wanfanya mabo yote kama mataifa, huwapenda wanaofanana nao, watu wa ulimwengu.  Watu wanaofanya dhambi na kuipenda dunia, hupendwa na ulimwengu, kwa sababu hawana tofauti nao.  Tukidai kwamba tumeokoka, huku ulimwengu unatupenda, madai yetu si ya kweli.

 

 

 

(3)            ULIMWENGU HUWACHUKIA WATU WASIO WA ULIMWENGU (15:19)

 

Ulimwengu, huhukumiwa sana unapowaona watu wanaoishi maisha ya utakatifu; kwa sababu hiyo huwachukia.  Shetani, mkuu wa ulimwengu, hujawa wivu mwingi anapowaona watu wanaoishi maisha ya utakatifu, kwa sababu anajua kwamba hawa wanakwenda mbinguni, mahali asipoweza kuingia, na hivyo huwachukia.  Kwetu Wakristo, hatuapswi kustaajabu, tukiona ulimwengu unatuchukia (1 YOHANA 3:13).  Ikiwa tunaushuhudia ulimwengu ya kuwa kazi zake ni mbovu, ulimwengu lazima utuchukie na kutuudhi.  Tangu mwanzo, Mungu aliweka uadui kati ya nyoka (shetani) na mwanamke pamoja na uzao wake (MWANZO 3:14-15).  Warithi wa mbingu, siku zote ni maadui wa watu wa ulimwengu huu.  Watu wasio haki huwachukia wenye haki sikuzote.  Kaini kwa msingi huu alimchukia habili mwenye haki; akamwua.  Baba yetu wa mbinguni akitupenda kwa kuwa tunazishika amri zake wale tunaokaa nao dunia wenye dhambi, hutuchukia.  Kwa msingi huu, Yusufu alichukiwa na nduguze (MWANZO 37:3-4).  Sauli alipooona na kutambua ya kwamba Bwana alikuwa pamoja na Daudi, Sauli akawa adui yake Daudi SIKU ZOTE ( 1 SAMWELI 18:28-29).  Ndivyo ilivyo hata leo, Bwana akiwa pamoja nasi, ulimwengu huwa adui kwetu (WAGALATIA 4:28-29).

 

 

 

(4)            ULIMWENGU HUWACHUKIA NA KUWAUDHI WATUMISHI WA MUNGU

 

             (15:19-20)

 

       Watumishi wa Mungu wanaohubiri kweli ya Neno la Mungu na kussshuhudia

 

ulimwengu ya kuwa kazi zake ni mbovvvu, ulimwengu huwachukia.  Mfalme Ahabu,

 

mtu wa ulimwengu, kwa msingi huu, alimchukia Nabii Mikaya mwana wa Imla

 

aliyehubiri kweli (YOHANA 7:7; 2 NYAKATI 18:6-7).  Watu vuguvugu wanaojiita

 

wameokoka, huku wanaipenda dunia, kwa jinsi hiihii, kama Ahabu huwachukia

 

Watumishi wa Mungu wanaoihubiri kweli.  Hatupaswi kuona ajabu.

 

 

 

(5)            MTUMWA SI MKUBWA KULIKO BWANA WAKE 15:20

 

Watu tuliookolewa, ni watumwa wa Bwana wetu Yesu Kristo.  Tunapokuwa Watumishi wa Mungu, tunapaswa kufahamu kwamba mafanikio yetu katika huduma zetu, hayana budi kufuata misingi aliyoitumia Yesu hata kupata mafanikio.  Yesu aliomba hata kulia sana na machozi (WAEBRANIA 5:7).  Sisi, siyo wakubwa kuliko Yeye, hivyo tusitazamie mafanikio bila maombi.  Yesu alikuwa mchapakazi (YOHANA 9:4), sisi nasi hatuna budi kuwa wachapakazi au siyo hatuwezi kufanikiwa.  Siyo hayo tu.  Yesu aliudhiwa na kudhihakiwa.  Aliambiwa amerukwa na akili, ana pepo tena ni Msamaria yaani mtu asiye na Mungu (MARKO 3:21; YOHANA 8:48).  Nasi tutaudhiwa vivyo hivyo.

 

 

 

(6)            ULIMWENGU KUTOKULISHIKA NENO (15:20)

 

Ikiwa watu wa ulimwengu walilipuuza Neno lake Yesu mwenyewe, sembuse neno letu tutakalolihubiri na kuwafundisha?  Hatupaswi kuona ajabu tukiwahubiria walimwengu, wengine wakakata shauri na wengine wakatutukana.  Ynapotupata haya tuendelee tu kuhubiri kama Mtume Paulo (MATENDO 19:8-10; 28:23-24, 30-31).

 

 

 

(7)            SABABU YA ULIMWENGU KUTUCHUKIA NA KUTUUDHI (15:21; 16:3)

 

Sababu kuu ya ulimwengu kutuchukia na kutuudhi baada ya kuokoka na kuishi maisha ya utakatifu, ni kwa kuwa hawamjui Mungu Baba wala hawamjui Yesu (1 YOHANA 2:3-4).  Tukiwa tumeokoka na kukaa katika mapenzi ya Mungu, waume zetu, wazazi wetu, marafiki zetu wa zamani, Boss wetu kazini, wote hawa watatuchukia ikiwa wao hawajaokoka, kwa sababu hawamjui Yesu.  Tunapaswa kuwasamehe tu na kusonga mebele.  Kamwe tusiache wokovu kwa sababu ya maudhi haya.  Kuna baraka au heri tele tukifanya hivi ( 1 PETRO 4:12-16).

 

 

 

(8)            WAJIBU WA KUONDOA UDHURU WA WENYE DHAMBI (15:22)

 

Pamoja na maudhi na dhihaka za wenye dhambi, kila mtu aliyeokoka anawajibika KUSEMA NAO, na kuwahubiria juu ya wokovu.  Wakikataa kuacha dhambi, hawana udhuru siku ya mwisho.

 

 

 

(9)            WALINICHUKIA BURE (15:23-25)

 

Yesu alitnda kwao kazi asizozitenda mtu mwingine, hata hivyo walimchukia.  Wao wenyewe walisema, “Namna hii hatujapata kuiona kamwe“.  Aliponya vilema, vipofu, na viziwei wao, hata hivyo, walimchukia bure.  Hayo pia yatatupata sisi.  Tunaweza tukawafanyia yote mema waume zetu au wazazi wetu ambao hawajaokoka, lakini bado watatuchukia.  Hatupaswi kuonaajabu.  Mtumwa si mkubwa kuliko Bwana wake.  Vivyo hivyo, leo, mtu yeyote anayemchukia Yesu na kukataa kuokoka, wakati aliteswa na kufa kwa ajili ya dhambi zetu, kufanya hivyo, ni kumchukia bure.  Kwa nini tufanye hivyo?  Kumchukia Yesu, ni kutafuta madhara makubwa siku ya hukumu.

 

 

 

(10)                   ROHO MTAKATIFU HUMSHUHUDIA YESU PAMOJA NASI (15:26-27)

 

Faida kubwa ya kujazwa nguvu ya Roho Mtakatifu, ni kuwa na Msaidizi anayemshuhudia Yesu pamoja nasi.  Mtu aliyejazwa nguvu ya Roho Mtakatifu, anapokuwa anahubiri, Roho Mtakatifu huhubiri pamoja naye, na hivyo matokeo yake kuwa makubwa, na rahisi, maana huyo Roho humhakikishia mtu tunayemhubiri kwamba ni mwenye dhambi na tunayosema ni haki na ni kweli na kwamba kuna hukumu inayomsubiri (YOHANA 16:7-8).  Sisi hatuwezi kufanya hayo.  Yeye atanishuhudia, nanyi pia mnashuhdia!

 

 

 

(11)                   SABABU YA KUELEZWA MAPEMA JUU YA KUCHUKIWA NA

 

            KUUDHIWA (16:1,4)

 

“Nimewaambia, msije mkachukizwa, nimewaambia haya, ili makusudi saa ile

 

itakapokuja mayakumbuke ya kuwa mimi naliwaambia“.  Makusudi ya Yesu

 

kutueleza mapema kwamba tutachukiwa na kuudhiwa, ni ili yatakapotokea tusione

 

ni mageni, na tena tushinde na kusonga mbele.  Hapa pia tunajifunza wajibu wa

 

Mwalimu wa Biblia.  Inatupasa kufundisha masomo ya kinga kwa Wakristo,

 

tukiwafundisha mapema mambo ambayo watayasikia au kukutana nayo.

 

Wakikutana na mafundisho potofu baada ya sisi kuwafundisha mapema kwa Biblia,

 

ni vigumu kwao kupotezwa.

 

 

 

(12)                   KUTENGWA HATA KUUAWA KWA WAKRISTO (16:2)

 

Watu waliookolewa walitengwa na masinagogi yao baada ya KUPIGWA (MATHAYO 10:17).  Hapa Yesu anasema hiyo haitoshi.  Watatuua wakidhani ni thawabu kwao.  Ndivyo ilivyo leo kwa watu wanaosema Yesu siyo Mwana wa Mungu.  Wakimwua Mkristo kwa jambia, wanadhani ni thawabu, wanadhani wamemtolea Mungu ibada.  Pamoja na haya yote, hatupaswi kubabaika (WARUMI 8:35-39). FULL GOSPEL

 

 

No comments: